Mkurugenzi Mkuu wa NSSF: Dhamira ya Serikali ni Kuhakikisha Wananchi Walioajiriwa Wananufaika na Hifadhi ya Jamii

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF: Dhamira ya Serikali ni Kuhakikisha Wananchi Walioajiriwa Wananufaika na Hifadhi ya Jamii

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MKURUGENZI MKUU WA NSSF: DHAMIRA YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA NI KUHAKIKISHA WANANCHI WALIOJIAJIRI WANANUFAIKA NA HIFADHI YA JAMII.

Awapongeza wananchi kwa muitikio wa kujiunga na kuchangia ili kujiwekea akiba kwa maisha bora ya sasa na ya baadaye kupitia kampeni ya NSSF Star Mchezo

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Bw. Masha Mshomba, amesema katika Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa fursa kwa Wananchi Waliojiajiri kujiunga na kuchangia NSSF ili wanufaike na huduma na mafao mbalimbali yanayotolewa.

Bw. Mshomba amesema hayo tarehe 7 Machi, 2025 katika soko la Kilombero, Jijini Arusha, wakati akizungumza na Mastaa wa Mchezo wa NSSF waliojiajiri ambao ni wakulima, wafugaji, wavuvi, wachimbaji wadogo wa madini, machinga, bodaboda, wasani mbalimbali, biashara nyingine ndogo ndogo (wasusi, wachuuzi wa masokoni, mamalishe na baba lishe).

"Kwa muda mrefu Mastaa wa Mchezo wa NSSF ambao ni wananchi waliojiajiri walikuwa hawanufaiki na hifadhi ya jamii kwa kujiwekea akiba, lakini Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ilitoa nafasi kwa Wananchi waliojiajiri kujiunga na kuchangia NSSF ili wanufaike na mafao yote yanayotolewa pamoja na mafao la matibabu," amesema Bw. Mshomba.

Amempongeza Rais Mhe. Dkt. Samia kwa kutoa nafasi kwa Wananchi Waliojiajiri kujiunga na kujiwekea akiba kwa ajili ya maisha yao ya sasa na ya baadaye.

Bw. Mshomba ametumia fursa hiyo kuwasihi wananchi waliojiajiri kujiunga kwa wingi NSSF ili iweze kuwahifadhi wanapopata majanga kama ya uzee, maradhi na ulemavu ambapo kwa wanaojiunga na kuchangia NSSF itakuwa Staa wa Mchezo wa baadaye kwa kuwapa mafao na huduma nyingine.

Amesema dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ni kuhakikisha wananchi waliojiajiri wananufaika na hifadhi ya jamii kwa kujiunga na kuchangia NSSF ambapo umewekwa utaratibu mzuri kwani huko huko waliko wakibofya *152*00# wanaweza kujiunga na kuchangia kidogo kidogo kwa siku bukubuku, kwa wiki, kwa mwezi au muhula.
 

Attachments

  • GlrkZ9pWEAAfBoY.jpg
    GlrkZ9pWEAAfBoY.jpg
    895.8 KB · Views: 1
  • GlrkZ9iW0AAYfQu.jpg
    GlrkZ9iW0AAYfQu.jpg
    1.3 MB · Views: 1
  • GlrkZ9yXoAAlsCV.jpg
    GlrkZ9yXoAAlsCV.jpg
    556.6 KB · Views: 1
  • GlrkZ9yXUAACCDc.jpg
    GlrkZ9yXUAACCDc.jpg
    566.6 KB · Views: 1
  • GlrkBwCX0AAwMma.jpg
    GlrkBwCX0AAwMma.jpg
    679 KB · Views: 1
  • GlrhrewXAAAVVtY.jpg
    GlrhrewXAAAVVtY.jpg
    885.3 KB · Views: 1
  • GlrhrfAXAAAbS3s.jpg
    GlrhrfAXAAAbS3s.jpg
    1 MB · Views: 1
  • Glrhre-XUAAayP8.jpg
    Glrhre-XUAAayP8.jpg
    1.2 MB · Views: 1
  • Glrhre_WkAAkAxP.jpg
    Glrhre_WkAAkAxP.jpg
    1.3 MB · Views: 1
  • Glre0PjXMAE0juY.jpg
    Glre0PjXMAE0juY.jpg
    133.1 KB · Views: 1
  • Glre0PVWEAAoE3C.jpg
    Glre0PVWEAAoE3C.jpg
    107.7 KB · Views: 1
  • Glre0PdW0AEyLam.jpg
    Glre0PdW0AEyLam.jpg
    115.6 KB · Views: 1
  • Glre0PWXcAEmWwv.jpg
    Glre0PWXcAEmWwv.jpg
    117.7 KB · Views: 1
Back
Top Bottom