Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Kuna sheria gani inaruhusu kuingilia faragha ya mtu
upload_2016-12-14_9-16-34.png
 
Melo yuko salama..wala hakuna jambo jipya kaitwa kuhojiwa tuu.
Lakini walio sababisha kuitwa kuhojiwa ni wale waleta habari za uzushi ambazo serikali inalazimika kuhangaika kuzikanusha kila leo...
sheria ile ya mitandao ina ipa mamlaka polisi kupata taarifa za mtu kutoka kwa mtu na inawezekana hata kuchukua vifaa husika...
Melo yuko salama salimini.
salama salmini lakini yupo lupango....hivi lupango ni salama au unamaanisha nn
 
Watumiaji wa mtandao wa JamiiForums wako huru kuweka mijadala, kuanzisha mijadala, kuchangia chochote pasipo kuvunja sheria za nchi au kuhatarisha usalama wa taifa.

Hiyo Sentensi nimelipenda. Mahakama ndiyo ipewe Nafasi katika kuamua maana ndiyo walinzi wa mambo ya Sheria kupitia Katiba na Sheria zenyewe.
 
Mungu akulinde Max. Naamini kwa leo utapata dhamana na maisha lazima ya endelea. Hata Martin Luther King toka wakati huo aliamini pamoja na ukandamizaji na utumwa wa enzi zile USA bado ndoto ya ilikuwa iko siku Black atakuwa President of USA.
 
duuuh hii nchi hii kweli nilishasema tunaelekea kubaya mno
 
THE GUARDIAN
"THE founder and managing director of popular social online platform JamiiForums, Maxence Melo, was yesterday arrested by the police in Dar es Salaam for allegedly refusing to divulge user data to the authorities".

JamiiForum is an internet forum where anybody can contribute his/her thoughts, the problem with this country is that we are living in 21st century but we still think as though we are practising Azimio la Arusha.

I believe there is another forum in Africa which I can describe it as a global one in terms peoples' contributions, you can read what they are talking about Muhammad Buhari.

Search
 
View attachment 445795
Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo, ameitwa na baadaye kuwekwa ndani, Central Police.

Polisi wanaeleza muda huu kwamba leo atalala ndani hadi kesho atakapofikishwa mahakamani.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi namba 9 ya mwaka 2016 dhidi ya Jamii Media dhidi ya polisi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

=====================

MKURUGENZI Mtendaji wa Jamii Media na mwanzilishi wa mtandao maarufu wa JamiiForums, anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo kuu cha polisi, Dar es Salaam, kwa madai ya kugomea agizo la muda mrefu la jeshi hilo.

Polisi wamekuwa wakiagiza na kuamuru kupewa taarifa za watumiaji wa JamiiForums bila mafanikio.

Maxence alipigiwa simu leo akiwa ofisini kwake asubuhi akitakiwa kufika kituoni hapo na alitekeleza mwito huo.

Baada ya kufika polisi kati, akiwa ameongozana na mhariri na mwanaharakati wa uhuru wa mawasiliano, Simon Mkina na mwanasheria, Nakazael Tenga, Maxence alinyimwa dhamana ya polisi.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa Maxence atafikishwa makahamani kesho asubuhi kujibu mashitaka ya kuzuia upelelezi wa polisi dhidi ya makosa ya mtandao.

JamiiForums imekuwa na msimamo wa kutotoa habari za wachangiaji wake kwa yeyote, kwani kufanya hivyo ni kuingialia uhuru na faragha ya wateja wake.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2006, msingi mkuu wa mtandao wa JamiiForums umekuwa kulinda faragha ya watumiaji wake.

Watumiaji wa mtandao wa JamiiForums wako huru kuweka mijadala, kuanzisha mijadala, kuchangia chochote pasipo kuvunja sheria za nchi au kuhatarisha usalama wa taifa.

Kampuni ya Jamii Media, inayoendesha mitandao ya JamiiForums.com na FikraPevu.com imejijengea heshima na umaarufu kwa muda mrefu kutokana na namna inavyoendesha na kusimamia shughuli zake ambazo kwa kiwango kikubwa ni za kimtandao.

Mtandao wa JamiiForums ni mtandao mkubwa wa Kiswahili kwa Afrika Mashariki na duniani ukiwa na wasomaji wasiopungua Milioni 2.5 kwa mwezi ambapo kwa mwaka 2016, mtandao huu unatimiza rasmi miaka 10 tangu uanzishwe.

Mtandao huu unasifika kwa kutoa fursa ya kipekee kwa watumiaji wake kutoa yaliyo mioyoni mwao huku wengine wakijifunza mbinu kadha wa kadha za kijasiriamali, afya, elimu na hata kuibuka wanasiasa wapya waliofundwa na wanajumuia ya JamiiForums.

Pamoja na kuendelea kutoa huduma hata katika nyakati ngumu, mtandao wa JamiiForums unakumbana mara kwa mara na changamoto nyingi zinazosababisha waanzilishi na waendeshaji wake kuwa katika misukosuko mara kwa mara, hasa na polisi.

Kwa muda mrefu tangu kuanzishwa kwa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, Jeshi la Polisi limekuwa likiushinikiza mtandao wa JamiiForums (kwa njia ya barua rasmi) kutoa taarifa za baadhi ya wateja wake.

JamiiForums katika kuhakikisha inasimamia usiri wa wateja wake, imekuwa ikihoji shinikizo kutoka Polisi yanazingatia sheria gani na kutaka kujua ni vifungu gani vya sheria ambavyo wadau wa mtandao huo wamevivunja bila kupewa maelezo yanayoridhisha zaidi ya kuelezwa kuwa hatua zaidi zitachukuliwa kama ushirikiano hautatolewa kwa Jeshi la Polisi.

Tayari Jamii Media imefungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania (Kesi namba 9 ya mwaka 2016); kutaka Sheria ya Makosa ya Mtandao, kifungu cha 32 na 38 viangaliwe upya kwa kuwa vinapelekea kuvunjwa kwa haki za msingi za watanzania watumiao mitandao ili kulinda maslahi ya umma kwa kuzingatia vifungu 26(2) na 30(3) vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.




Baada ya kufungua kesi hiyo Serikali, kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliweka mapingamizi sita ikitaka kesi nzima ifutwe na Jamii Media walipe gharama zilizoingiwa.

Lakini mnamo tarehe 4, Agosti 2016 Mahakama Kuu ya Tanzania baada ya kuzipitia hoja zilizowasilishwa na Serikali na Wanasheria wa Jamii Media iliamua kuwa mapingamizi yote sita ya Serikali hayana mashiko na hivyo kesi ya msingi itaendelea kusikilizwa.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi hiyo ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

Chanzo: FikraPevu

Wakuu moderators tunaomba mfungue uzi wa kutupa updates za mahakamani leo
 
jamani niliimisi sana Jf,imenisaidia vitu vingi sanaaaa ambavyo nlikua busy navyo hadi nikapotea humu jukwaani.
habari hii imenishitua sanaaaa........
ni mwendo wa kuzidisha maombi tu,haya yote yatakwisha.....
Hizi dhana za maombi Tanzania huwa sinanifurahisha sometimes. Naona Mungu tunamtwisha hata mambo yasiyomuhusu. Tumepewa uhuru wa kutawala na kujitawala tangu uumbaji, let fight for our right tuache kumchosha Mungu
 
Mpaka hapo alipofikia Max ni shujaa, angekua mwingine Jf ingepoteza dira siku nyingi. Natumai Sheria itachukua mkondo wake haki itapatikana. Dua zetu kwako Max.
 
Ndugu wanajamvi;

Naandika haya nikiwa nina maswali tata kadha wa kadha kichwani mwangu lakini majibu yake naona hakuna wa kunipa kwa sasa!

Suala la Ben sanane kupotea katika mazingira ya kutatanisha siyo jambo nzuri kwa afya ya siasa zetu ilo tulijue wote siyo upinzani siyo chama tawala. Ni vizuri kuhoji amepoteaje kuliko kuchukulia uepesi kama wengine ninavowaona humu ndani au kushangilia moyoni.

Ni lazima tujue wote kuwa Ben sanane ni mtu na ana haki zake kama mimi kama wewe hivyo basi tuachilie mbali harakati zake za kisiasa labda alikuwa anakosoa upande fulani ni haki yake kikatiba kama mimi kama wewe tunavoona makosa ya mbowe na kukosoa ! Hii ndio aina ya siasa ambayo tumelelewa na tumekulia.

Ukweli utuweke huru kuliko chuki kutamalaki kwenye mambo yenye maslahi ya taifa, ni vyema vyombo vinavohusika vifanye uchunguzi wa haraka na umakini utawale ili kuuondoa minong'onong'o na taharuki katika jamii yetu.

Mimi ni miongoni mwa wale wanaoamini kuwa waziri wa mambo ya ndani juzi alilitoea majibu mepesi kwenye maswali magumu na ata yeye akiitafakari nahisi atajua hilo ni mda huu wa kujisahisha na kuja na majibu yanayoridhisha kuuhusu ile miili saba iliyozikwa kinyemela! Nashukuru angalau PM ameagiza uchunguzi lakini katika hili angeongezea neno huru iwe "IWE UCHUNGUZI HURU" ili kuondoa taharuki hii kwa wananchi .

DUKUDUKU LANGU KWA CHADEMA KUHUSU BEN SANANE:

Naomba Ukweli utuweke huru kabsaa! Ben kathibitika amepotea ndani za siku ishirini tena kwa kutooenaka mtandaoni maswali ya kujiuliza ni mengi hapa na mengine yawezekana tusipate majibu yake lakini turudi kwenye hoja ya msingi!

Chama kikubwa kama chadema inakuja kutoa tamko juu ya hili jambo baada ya wadau wa kawaida tyuu kuhoji na kupaza sauti zao usiku na mchana nahisi ata kikatiba ya chama kila mtu ni sawa bila kujali ushawishi au cheo chake. Je angepotea Tundu Lisu ata kwa wiki mmoja chama kisingetoa tamko? tukumbuke Ben saanane naye ni kada kindakindaki wa chadema ni Afisa kwenye ngazi ya uongozi ndani ya chama.

Ni maoni yangu kuwa Freeman Mbowe kama Mwenyekiti wa taifa na anayejipambanua kuwa ni mzalendo na mpigania haki za watanzania alivyosikia hii habari ya ben sanane kupotea angesitisha ziara yake kwa heshima yake ndani ya chama na ndani ya nchi kuja kufuatilia na kuongoza uchunguzi kuhusu hili jambo na ata zile maiti waliozikwa kimyakimya.

Hapa ndipo tukubali, tukatae siasa zetu bado zipo nyuma sanaa hii issue ingetokea ata kwa majirani wetu kenya ingekuwa hot kwelikweli lakini mkuu wa upinzani yeye yupo ulaya hana mda na haya mambo kwangu mimi napatwa na ukakasi mkubwa! Wewe ndiye mpambaji mkuu halafu upo nyuma kabsaa la jambo gumu kama hili sisi wapambanaji wa kawaida tukuchukuliaje?

Katibu mkuu Dk. Mashinji anaongea kwenye gazeti la mtanzania halafu la kwake limeishia kiivo! Ni watanzania wangapi wana acces kusoma gazeti la mtanzani? Haya ndiyo majibu mepesi kwenye mambo magumu kama haya! Hapa ndipo tukubali tukatae DK. Slaa bado ataonekana kuwa mpambanaji bora kwenye vita katika mda wote.

Ni wale wanaoamini Ben yupo hai ata kama yupo mikononi mwa majasusi au la ni vyema apatikane akiwa hai kwa haraka hili mambo kadha wa kadha yaendeleee katika nchi yetu, Na siamini katika nchi yetu tumeshafika kwenye siasa za kutekana mimi naamini nchi yetu bado ni huru na wananchi wanatakiwa kuwa huru.

KUHUSU CEO WA JAMIIFORUMS, MAX:

Kama kichwa changu cha habari tuache na kuweka itikadi zetu vya vyama pembeni tuweke maslahi ya taifa kwanza kwenye hili jambo!

Ila swali kwenu je Jamii forum ikizimwa nani atafaidika???? ndipo tuanze hapo kutafakari kwa kina kuliko kubishana na ukweli!

Ni wako kijana mtiifu, Mwanaharakati na mzalendo wa kweli katika taifa hili.
Mungu ibariki Tanzania.
 
Huku zanzibar kuna mazombi zaid ya miaka 20 hajakamatwa hata mmoja. Tanganyika inahitajika uhuru mpya
 
Back
Top Bottom