Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

JF ina rensponsibility kubwa sana, kama vivlivyo vyombo vingine vya Habari, kuna mambo mengi ya uongo na uzushi huletwa humu na kuachwa, ikumbukwe kwamba nchi nyingi kama Kenya, Rwanda, Burundi n.k Vita ililetwa na Vyombo vya Habari kama redio na TV, hivyo JF ina jukumu la kulinda amani ya nchi, kama ni kweli amekamatwa, na kama siyo kweli basi wajifunze na wabadilike, watambue jukumu lao kwenye Jamii!

CEO wa JF asipumbazwe na watu wanaosapoti kwenda kinyume na Serikali hapa, wengi wao wana maisha yao na wala hawaishi TZ, na JF ikifa kesho, au ofisi ya JF kunyimwa kibali cha kufanya kazi TZ hawana cha kupoteza, zaidi ya kuhamia kwenye mtandao mwingine na kuendeleza wanayoyafanya, hivyo angalia maisha yako na familia yako, fanya lililo sahihi na jinsi Serikali inavyokutaka kwani mwisho wa siku Serikali ndiyo yenye nchi, watakushauri wanachama wa JF wanavyotaka lkn Serikali ndiyo wasimamizi wa hii nchi!
Facebook watapafanyaje?
 
Hivi ushajiuliza ni matukio mangapi yanatokea nchi nzima kwa siku na polisi inabidi wadili nayo. Mambo mazito ya forgery kama yapi? Hivi unajua kuwa mumewe yule kajala masanja muigizaji mpaka leo hii yupo jela kwa ajili ya gorgery. Hujiulizi kina shose sinare na sioi sumari wako rumande na moja ya kosa lao ni forgery.

Mnachotetea ni hawa wahalifu wanaharibu taswira ya JF wasichukuliwe hatua wao ni kina nani?

Inawezekana isiwe ni approach nzuri kumkamafa maxence mello na kumlaza ndani ila kesi ya msingi hapo ipo.

Information za wale wavunjifu wa amani wanapost matamko ya kufoji ya serikali lazima zitolewe na wachukuliwe hatua ili ku maintain Law and Order.

Ujinga tu kama ujinga mwingine. Mkitaka msisemwe mnakuja na gear ya law and order. Ujinga tu.
 
View attachment 445795
Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo, ameitwa na baadaye kuwekwa ndani, Central Police.

Polisi wanaeleza muda huu kwamba leo atalala ndani hadi kesho atakapofikishwa mahakamani.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi namba 9 ya mwaka 2016 dhidi ya Jamii Media dhidi ya polisi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

=====================

MKURUGENZI Mtendaji wa Jamii Media na mwanzilishi wa mtandao maarufu wa JamiiForums, anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo kuu cha polisi, Dar es Salaam, kwa madai ya kugomea agizo la muda mrefu la jeshi hilo.

Polisi wamekuwa wakiagiza na kuamuru kupewa taarifa za watumiaji wa JamiiForums bila mafanikio.

Maxence alipigiwa simu leo akiwa ofisini kwake asubuhi akitakiwa kufika kituoni hapo na alitekeleza mwito huo.

Baada ya kufika polisi kati, akiwa ameongozana na mhariri na mwanaharakati wa uhuru wa mawasiliano, Simon Mkina na mwanasheria, Nakazael Tenga, Maxence alinyimwa dhamana ya polisi.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa Maxence atafikishwa makahamani kesho asubuhi kujibu mashitaka ya kuzuia upelelezi wa polisi dhidi ya makosa ya mtandao.

JamiiForums imekuwa na msimamo wa kutotoa habari za wachangiaji wake kwa yeyote, kwani kufanya hivyo ni kuingialia uhuru na faragha ya wateja wake.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2006, msingi mkuu wa mtandao wa JamiiForums umekuwa kulinda faragha ya watumiaji wake.

Watumiaji wa mtandao wa JamiiForums wako huru kuweka mijadala, kuanzisha mijadala, kuchangia chochote pasipo kuvunja sheria za nchi au kuhatarisha usalama wa taifa.

Kampuni ya Jamii Media, inayoendesha mitandao ya JamiiForums.com na FikraPevu.com imejijengea heshima na umaarufu kwa muda mrefu kutokana na namna inavyoendesha na kusimamia shughuli zake ambazo kwa kiwango kikubwa ni za kimtandao.

Mtandao wa JamiiForums ni mtandao mkubwa wa Kiswahili kwa Afrika Mashariki na duniani ukiwa na wasomaji wasiopungua Milioni 2.5 kwa mwezi ambapo kwa mwaka 2016, mtandao huu unatimiza rasmi miaka 10 tangu uanzishwe.

Mtandao huu unasifika kwa kutoa fursa ya kipekee kwa watumiaji wake kutoa yaliyo mioyoni mwao huku wengine wakijifunza mbinu kadha wa kadha za kijasiriamali, afya, elimu na hata kuibuka wanasiasa wapya waliofundwa na wanajumuia ya JamiiForums.

Pamoja na kuendelea kutoa huduma hata katika nyakati ngumu, mtandao wa JamiiForums unakumbana mara kwa mara na changamoto nyingi zinazosababisha waanzilishi na waendeshaji wake kuwa katika misukosuko mara kwa mara, hasa na polisi.

Kwa muda mrefu tangu kuanzishwa kwa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, Jeshi la Polisi limekuwa likiushinikiza mtandao wa JamiiForums (kwa njia ya barua rasmi) kutoa taarifa za baadhi ya wateja wake.

JamiiForums katika kuhakikisha inasimamia usiri wa wateja wake, imekuwa ikihoji shinikizo kutoka Polisi yanazingatia sheria gani na kutaka kujua ni vifungu gani vya sheria ambavyo wadau wa mtandao huo wamevivunja bila kupewa maelezo yanayoridhisha zaidi ya kuelezwa kuwa hatua zaidi zitachukuliwa kama ushirikiano hautatolewa kwa Jeshi la Polisi.

Tayari Jamii Media imefungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania (Kesi namba 9 ya mwaka 2016); kutaka Sheria ya Makosa ya Mtandao, kifungu cha 32 na 38 viangaliwe upya kwa kuwa vinapelekea kuvunjwa kwa haki za msingi za watanzania watumiao mitandao ili kulinda maslahi ya umma kwa kuzingatia vifungu 26(2) na 30(3) vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.




Baada ya kufungua kesi hiyo Serikali, kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliweka mapingamizi sita ikitaka kesi nzima ifutwe na Jamii Media walipe gharama zilizoingiwa.

Lakini mnamo tarehe 4, Agosti 2016 Mahakama Kuu ya Tanzania baada ya kuzipitia hoja zilizowasilishwa na Serikali na Wanasheria wa Jamii Media iliamua kuwa mapingamizi yote sita ya Serikali hayana mashiko na hivyo kesi ya msingi itaendelea kusikilizwa.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi hiyo ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

Chanzo: FikraPevu

Pole sana bro. Tunatambua na kuheshimu kazi kubwa unayoifanya. Ni kazi ambayo inastahili sio sifa na pongezi pekee, bali ni kazi ambayo inataka uwe mzalendo na jasiri. Kuna mengi yanaweza kukukuta kwa kuwa mzalendo na jasiri, kati yake ni DISCRIMINATION na VICTIMIZATION. Kwa wanaharakati wa haki za binadamu, hayo si mambo ya kuogopa hata kidogo kwa sababu kuwa mwanaharakati ni haki yako pia kama binadamu.
Unawasaidia na umeendelea kuwasaidia wengi. Wengi wemetoa stress zao hapa, wengi wameumbuliwa hapa, na wataendelea kuumbuliwa.
Hili ni moja ya mabaraza bora zaidi kwa wanaharakati. Kamanda Max, together we stand bro.
 
Hivi atakubali kweli tumbadilishe mwingine baada ya miaka yake mitano? Naona kama sasa amezidi, hataki kukosolewa, kusemwa vibaya, mbona katika jamii zetu sijawahi kuona mtu anasemwa kwa mazuri tu, hata ufanye mazuri mwingine anaweza kuona ni mabaya kwa mtazamo wake, yani leo wote tuwe na mtazamo sawa inawezekana kweli? Mbona mke kila mtu anachagua anayempenda iweje kwa kiongozi kulazimishana kumpenda wote?!!!! anyway duniani kuna kuzaliwa na kufa, yote ni maisha, hakuna atakayeishi milele, Hitler alikua mbabe kweli lakini mwisho wa siku alikufa.
Very Correct, hapo kwenye red
 
Ndugu wanajamvi;

Naandika haya nikiwa nina maswali tata kadha wa kadha kichwani mwangu lakini majibu yake naona hakuna wa kunipa kwa sasa!

Suala la Ben sanane kupotea katika mazingira ya kutatanisha siyo jambo nzuri kwa afya ya siasa zetu ilo tulijue wote siyo upinzani siyo chama tawala. Ni vizuri kuhoji amepoteaje kuliko kuchukulia uepesi kama wengine ninavowaona humu ndani au kushangilia moyoni.

Ni lazima tujue wote kuwa Ben sanane ni mtu na ana haki zake kama mimi kama wewe hivyo basi tuachilie mbali harakati zake za kisiasa labda alikuwa anakosoa upande fulani ni haki yake kikatiba kama mimi kama wewe tunavoona makosa ya mbowe na kukosoa ! Hii ndio aina ya siasa ambayo tumelelewa na tumekulia.

Ukweli utuweke huru kuliko chuki kutamalaki kwenye mambo yenye maslahi ya taifa, ni vyema vyombo vinavohusika vifanye uchunguzi wa haraka na umakini utawale ili kuuondoa minong'onong'o na taharuki katika jamii yetu.

Mimi ni miongoni mwa wale wanaoamini kuwa waziri wa mambo ya ndani juzi alilitoea majibu mepesi kwenye maswali magumu na ata yeye akiitafakari nahisi atajua hilo ni mda huu wa kujisahisha na kuja na majibu yanayoridhisha kuuhusu ile miili saba iliyozikwa kinyemela! Nashukuru angalau PM ameagiza uchunguzi lakini katika hili angeongezea neno huru iwe "IWE UCHUNGUZI HURU" ili kuondoa taharuki hii kwa wananchi .

DUKUDUKU LANGU KWA CHADEMA KUHUSU BEN SANANE:

Naomba Ukweli utuweke huru kabsaa! Ben kathibitika amepotea ndani za siku ishirini tena kwa kutooenaka mtandaoni maswali ya kujiuliza ni mengi hapa na mengine yawezekana tusipate majibu yake lakini turudi kwenye hoja ya msingi!

Chama kikubwa kama chadema inakuja kutoa tamko juu ya hili jambo baada ya wadau wa kawaida tyuu kuhoji na kupaza sauti zao usiku na mchana nahisi ata kikatiba ya chama kila mtu ni sawa bila kujali ushawishi au cheo chake. Je angepotea Tundu Lisu ata kwa wiki mmoja chama kisingetoa tamko? tukumbuke Ben saanane naye ni kada kindakindaki wa chadema ni Afisa kwenye ngazi ya uongozi ndani ya chama.

Ni maoni yangu kuwa Freeman Mbowe kama Mwenyekiti wa taifa na anayejipambanua kuwa ni mzalendo na mpigania haki za watanzania alivyosikia hii habari ya ben sanane kupotea angesitisha ziara yake kwa heshima yake ndani ya chama na ndani ya nchi kuja kufuatilia na kuongoza uchunguzi kuhusu hili jambo na ata zile maiti waliozikwa kimyakimya.

Hapa ndipo tukubali, tukatae siasa zetu bado zipo nyuma sanaa hii issue ingetokea ata kwa majirani wetu kenya ingekuwa hot kwelikweli lakini mkuu wa upinzani yeye yupo ulaya hana mda na haya mambo kwangu mimi napatwa na ukakasi mkubwa! Wewe ndiye mpambaji mkuu halafu upo nyuma kabsaa la jambo gumu kama hili sisi wapambanaji wa kawaida tukuchukuliaje?

Katibu mkuu Dk. Mashinji anaongea kwenye gazeti la mtanzania halafu la kwake limeishia kiivo! Ni watanzania wangapi wana acces kusoma gazeti la mtanzani? Haya ndiyo majibu mepesi kwenye mambo magumu kama haya! Hapa ndipo tukubali tukatae DK. Slaa bado ataonekana kuwa mpambanaji bora kwenye vita katika mda wote.

Ni wale wanaoamini Ben yupo hai ata kama yupo mikononi mwa majasusi au la ni vyema apatikane akiwa hai kwa haraka hili mambo kadha wa kadha yaendeleee katika nchi yetu, Na siamini katika nchi yetu tumeshafika kwenye siasa za kutekana mimi naamini nchi yetu bado ni huru na wananchi wanatakiwa kuwa huru.

KUHUSU CEO WA JAMIIFORUMS, MAX:

Kama kichwa changu cha habari tuache na kuweka itikadi zetu vya vyama pembeni tuweke maslahi ya taifa kwanza kwenye hili jambo!

Ila swali kwenu je Jamii forum ikizimwa nani atafaidika???? ndipo tuanze hapo kutafakari kwa kina kuliko kubishana na ukweli!

Ni wako kijana mtiifu, Mwanaharakati na mzalendo wa kweli katika taifa hili.
Mungu ibariki Tanzania.
.
Nina wasi wasi na hawa waliomkamata Max , walifanikiwa kumnanga Ben ila wakashindwa kuwapata wakosoaji wengine waliokuwa na ID za kificho. Ben yeye alikua anaingia jamii forum na jina lake kamili.
Ona sasa madhara yaliyompata.
 
View attachment 445795
Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo, ameitwa na baadaye kuwekwa ndani, Central Police.

Polisi wanaeleza muda huu kwamba leo atalala ndani hadi kesho atakapofikishwa mahakamani.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi namba 9 ya mwaka 2016 dhidi ya Jamii Media dhidi ya polisi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

=====================

MKURUGENZI Mtendaji wa Jamii Media na mwanzilishi wa mtandao maarufu wa JamiiForums, anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo kuu cha polisi, Dar es Salaam, kwa madai ya kugomea agizo la muda mrefu la jeshi hilo.

Polisi wamekuwa wakiagiza na kuamuru kupewa taarifa za watumiaji wa JamiiForums bila mafanikio.

Maxence alipigiwa simu leo akiwa ofisini kwake asubuhi akitakiwa kufika kituoni hapo na alitekeleza mwito huo.

Baada ya kufika polisi kati, akiwa ameongozana na mhariri na mwanaharakati wa uhuru wa mawasiliano, Simon Mkina na mwanasheria, Nakazael Tenga, Maxence alinyimwa dhamana ya polisi.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa Maxence atafikishwa makahamani kesho asubuhi kujibu mashitaka ya kuzuia upelelezi wa polisi dhidi ya makosa ya mtandao.

JamiiForums imekuwa na msimamo wa kutotoa habari za wachangiaji wake kwa yeyote, kwani kufanya hivyo ni kuingialia uhuru na faragha ya wateja wake.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2006, msingi mkuu wa mtandao wa JamiiForums umekuwa kulinda faragha ya watumiaji wake.

Watumiaji wa mtandao wa JamiiForums wako huru kuweka mijadala, kuanzisha mijadala, kuchangia chochote pasipo kuvunja sheria za nchi au kuhatarisha usalama wa taifa.

Kampuni ya Jamii Media, inayoendesha mitandao ya JamiiForums.com na FikraPevu.com imejijengea heshima na umaarufu kwa muda mrefu kutokana na namna inavyoendesha na kusimamia shughuli zake ambazo kwa kiwango kikubwa ni za kimtandao.

Mtandao wa JamiiForums ni mtandao mkubwa wa Kiswahili kwa Afrika Mashariki na duniani ukiwa na wasomaji wasiopungua Milioni 2.5 kwa mwezi ambapo kwa mwaka 2016, mtandao huu unatimiza rasmi miaka 10 tangu uanzishwe.

Mtandao huu unasifika kwa kutoa fursa ya kipekee kwa watumiaji wake kutoa yaliyo mioyoni mwao huku wengine wakijifunza mbinu kadha wa kadha za kijasiriamali, afya, elimu na hata kuibuka wanasiasa wapya waliofundwa na wanajumuia ya JamiiForums.

Pamoja na kuendelea kutoa huduma hata katika nyakati ngumu, mtandao wa JamiiForums unakumbana mara kwa mara na changamoto nyingi zinazosababisha waanzilishi na waendeshaji wake kuwa katika misukosuko mara kwa mara, hasa na polisi.

Kwa muda mrefu tangu kuanzishwa kwa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, Jeshi la Polisi limekuwa likiushinikiza mtandao wa JamiiForums (kwa njia ya barua rasmi) kutoa taarifa za baadhi ya wateja wake.

JamiiForums katika kuhakikisha inasimamia usiri wa wateja wake, imekuwa ikihoji shinikizo kutoka Polisi yanazingatia sheria gani na kutaka kujua ni vifungu gani vya sheria ambavyo wadau wa mtandao huo wamevivunja bila kupewa maelezo yanayoridhisha zaidi ya kuelezwa kuwa hatua zaidi zitachukuliwa kama ushirikiano hautatolewa kwa Jeshi la Polisi.

Tayari Jamii Media imefungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania (Kesi namba 9 ya mwaka 2016); kutaka Sheria ya Makosa ya Mtandao, kifungu cha 32 na 38 viangaliwe upya kwa kuwa vinapelekea kuvunjwa kwa haki za msingi za watanzania watumiao mitandao ili kulinda maslahi ya umma kwa kuzingatia vifungu 26(2) na 30(3) vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.




Baada ya kufungua kesi hiyo Serikali, kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliweka mapingamizi sita ikitaka kesi nzima ifutwe na Jamii Media walipe gharama zilizoingiwa.

Lakini mnamo tarehe 4, Agosti 2016 Mahakama Kuu ya Tanzania baada ya kuzipitia hoja zilizowasilishwa na Serikali na Wanasheria wa Jamii Media iliamua kuwa mapingamizi yote sita ya Serikali hayana mashiko na hivyo kesi ya msingi itaendelea kusikilizwa.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi hiyo ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

Chanzo: FikraPevu

"Maendeleo ni kupanuka kwa uchumi na uhuru," Mwalimu Julius Nyerere.
 
Since the beginning of the 21st Century, authoritarian regimes have been shaking in their pants from a looming danger. Don’t think that the danger has anything to do with “Nuclear stockpiles” or “Dinosaur apocalypse”. The danger is in “you”: Social Media users, for instance JF in our context. Why? Because social media is a powerful tool that can invoke “synchronized public actions, resulting from “synchronized public awareness.” This is why so much time and resources is often spent on controlling the Media. Daunting challenge however arises from the fact that unlike traditional media, social media is much more unpredictable, hence uncontrollable. For instance, passing of information via ‘JF’ has freed many Tanzanians from relying on traditional media outlets, which are increasingly becoming state controlled. Also with the advent of ‘JF’, the influence of State Propaganda is becoming severely limited as vast sources of information which are beyond government’s control are now easily accessible by ordinary Tanzanians.

You are a nightmare to the regime.
You're writing leaning on the easy side. I hope you are a learned person who understands that, rights go hand in hand with responsibility. As much as we dearly need media freedom, the media houses and other stakeholders must be aware of their responsibility to uphold professionalism and ethical conduct in their writings/reporting. Media shouldn't be used as a platform for propagation of lies and hatred, both of which are good catalyst for chaos.
 
Ujinga tu kama ujinga mwingine. Mkitaka msisemwe mnakuja na gear ya law and order. Ujinga tu.
Ushapigwa na maisha wewe. Njaa zenu za kutaka kujifanya kujua kusema mmemtafutia mwenzenu matatizo.

Kusema hamjakatazwa. Ila zingatieni sheria sio tu za nchi hata humu JF kuna sheria zake
 
You're writing leaning on the easy side. I hope you are a learned person who understands that, rights go hand in hand with responsibility. As much as we dearly need media freedom, the media houses and other stakeholders must be aware of their responsibility to uphold professionalism and ethical conduct in their writings/reporting. Media shouldn't be used as a platform for propagation of lies and hatred, both of which are good catalyst for chaos.
Media freedom and freedom of expression can't bring about chaos,but help the sustainability of national unity as everyone is free to speak what he/she believes. Don't tell me about the current Newspaper Act.[emoji12]
 
Back
Top Bottom