Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Daktari Profesa Janabi ana hofu na nini hadi awe na ulinzi mkubwa namna ile?

Ni usalama
 
Sawa!! Lakini iweje leo ndio awekewe ulinzi wote ule, mbona miaka yote ile haikuwa hivyo?!!
Fafanua huo ulinzi uliouona ukoje? Mimi niliwahi kwenda pale JKHI na ikatokea daktari wetu ameingia theater Kumhudumia mgonjwa mwingine aliyezidiwa. Huyo Dr Janabi akapita na kuona foleni yetu haiendi na kuna bibi mmoja alikuwa hoi, to my surprise alimuita nesi kujua daktari wetu yuko wapi na baada ya kuelezwa tuu akaingia mwenyewe mzigoni pale pale akamhudumia yule bibi na watu wengine watatu ambao nao walikuwa wamezidiwa, kiukweli jamaa ni very humble and simple.
 
Kumbe ameanza kulindwa kwa ulinzi mkali. Wamlinde ili kumzuia Mungu asimguse kabisa maana ni Mtakatifu na msafi sana.
 
Hivi ni Mhindi au Mbantu? Huyo Janabi
 
Shukrani Sana mkuu. Mwambie tu kuwa Dr. Sarungi alikuwa na visiting hospital kubwa nchini na baadhi nje ya nchi. Cases ngumu zilikuwa zinawekwa pending mpaka aende. Kiasi kwamba alipoingia kwenye Siasa malalamiko yalikuwa mengi Sana toka Kwa madaktari na wadau wa Afya. He is a renown Surgeon.
 
Wakati wa sarungi hapakuwa na hospitali kubwa nchini
 
Janabi alimsaidia sana Mzee wangu mshipa unaopeleka damu kwenye moyo uliziba alimtibia.
Kwahyo mkuu aongezewe ulinzi mkali uzidishwe kwake siyo

Pia sasa HV lemutuz amemtangaza kuwa Ni dkt wake binafsi

Pia Ni mjumbe wa bodi ya Simba sports club
Manar pia aliropoka hili mahali
 
NI DAKTARI BINGWA MUHIMU MNO NDANI YA TAALUMA HIYO NI MTU AGHALI SANA HATA KUMTENGENEZA MWINGINE.
Kabisa. Hivi unafikiri wale Wahindi waliokuwa Wana organise safari za India wakijua kuna commission watafurahi kuona wagonjwa wanatibiwa humu nchini? Tena walikuwa na grant kabisa inachangwa ndani na nje ya nchi ili kusaidia wagonjwa waende India na walikuwa wanakula vibaya na bado India kuna commission. Lazima alindwe Sana
 
Kwahyo mkuu aongezewe ulinzi mkali uzidishwe kwake siyo

Pia sasa HV lemutuz amemtangaza kuwa Ni dkt wake binafsi

Pia Ni mjumbe wa bodi ya Simba sports club
Manar pia aliropoka hili mahali
Haaa mkuu taraatibu basi, wakati mzee anatibiwa na huyo Dr hakuwa hivyo na ulinzi mambo yalikuwa mwayangu mwayangu tuu. Hata hivyo mzee wangu ameshatangulia mbele ya haki Ameeen Ameen.
 
Wakati wa sarungi hapakuwa na hospitali kubwa nchini
Aisee. Zilikuwepo kwa ukubwa wake kipindi hicho. Alikuwa Visiting Bugando na KCMC. Nairobi na kwingine. Hivyo kwetu Tanzania enzi hizo kulikuwa na Muhimbili Refferal Hospital ikisaidiwa na Bugando kanda ya Ziwa na KCMC kaskazini japo nayo ilibeba wagonjwa Tanzania nzima mpaka nchi jirani. Hizo zimeendelea kukua mpaka zilipo na zimeibuka nyingine sasa za mikoa na nyinginezo. KCMC wakati huyo ikiwa full chini ya🍾Samaritan/Lutheran na Bugando kanisa Katoliki. Kwa sasa Serikali inahudumia kiasi Fulani cha bajeti hospital hizi na watumishi wako wa Aina mbili ambao ni serikali full wanalipwa na full Kwa hao mashirika.
 
Haaa mkuu taraatibu basi, wakati mzee anatibiwa na huyo Dr hakuwa hivyo na ulinzi mambo yalikuwa mwayangu mwayangu tuu. Hata hivyo mzee wangu ameshatangulia mbele ya haki Ameeen Ameen.
Pole Sana mkuu mm sijakudhiaki kwa mzee kutibiwa na pro janabi nilikuukiza tu Haina Mana kuwa siyo Ni atabaki kuwa dkt. Had mwishi hapa yanaletwa hoja ya kwann anapewa ulinzi mkali
 
Pole Sana mkuu mm sijakudhiaki kwa mzee kutibiwa na pro janabi nilikuukiza tu Haina Mana kuwa siyo Ni atabaki kuwa dkt. Had mwishi hapa yanaletwa hoja ya kwann anapewa ulinzi mkali
Haina shida si unajua hapa hatufahamiani mitandao isituletee uadui mkuu. Mimi nimeeleza nilivyomjua na alivyosaidia mzee wangu na ugonjwa wake. Amani tuu iendelee pamoja.
 
Prof Jamani ni mtu mmoja very social. Mwaka Jana tulimwalika kwenye kikao chetu Cha kazi kuja kutoa mada, aiseee!!! Tuliinjoy Sana. Jamaa ana madini hatari. Lakini pia huwezi kuchoka kumsilikiza Make Ana vichekesho vya hapa na.pale Hadi rahaaaa
 
Halafu eti MTU anahoji ulinzi. Ile ni tunu. Kuipoteza hatutakaa tupate mwingine. Ni international figure. Mijitu mingine inawaza tu mtu kuuliwa wakati tayari hata ukimwangalia usoni alishajifia. Magari tu ya kampeni au safari yalijazwa viokozi kibao. Kampeni hakuweza kukamilisha zote na nyingine tarehe zilisogezwa au kufutwa walipoona Hali ya Afya ni mbovu. Corona akafichwa msituni kwao maana alikuwa delicate Ila kilichotokea baada ya kubeza mask ni sidiria kinajulikana wazi. Wasije kutuletea mitungo ya hadithi za kufikirika.
 
Mwaka 2016/17 sikumbuki exactly ni mwaka gani ktk hii miwili nilikuwa na mgonjwa wangu alilazwa pale MNH ukitoka zilipo ward za wagonjwa wa moyo kwa mbele kuna cafeteria nakumbuka kama mara mbili au tatu nimekaa na huyu professor meza moja na tulikuwa hatujuani.

May be protocol zimebadilika?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…