Mkurugenzi wa Jiji Dodoma amefeli zoezi la urasimishaji makazi Nzuguni A

Mkurugenzi wa Jiji Dodoma amefeli zoezi la urasimishaji makazi Nzuguni A

Mdomowabata

Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
19
Reaction score
47
Mheshimiwa Rais sisi wakazi wa Nzuguni A tunakuomba uingilie kati zoezi hili lisiloisha kwa wenye makazi na viwanja katika eneo la Nzuguni A.

Zoezi hili linakaribia mwaka wa tatu lakini imekuwa linaenda kwa kusuasua sana urasimu umekuwa ni mwingi l, ubabaishaji na Rushwa imekithiri kupelekea watu kupoteza haki zao na kupelekea malalamiko mengi yasiyoisha kupelekea kukwamisha ukamilikaji wa mradi huo.

Binafsi ni mmiliki wa ardhi katika eneo hilo pindi nilipotaka kuanza ujenzi baada ya kukopa katika vikoba kulitolewa katazo la kutoendeleza chochote kwa miezi sita mpaka zoezi litakapokamilika basi nilivulia kwa kipindi hicho na sasa ni mwaka wa 3 hakuna kinachoeleweka kwa asilimia kubwa ya milimiki tuliozuiwa kuendelea kwa ujenzi, kwani maeneo mengi ya viwanja walivyopima wameweka maingiliano yaliyosababisha watu kushikiana mapanga,wengine viwanja kumegwa kutokana na miundombinu bila kuainisha utafidiwa vipi, asilimia kuwa tulionunua ardhi huku ni masikini basi imekuwa ni uonevu kupata haki na wale wanaojiweza wamejenga kwa kutumia nguvu zao.

Baada ya malalamiko mengi tuliadiwa kufanyiwa marekebisho kwa wale walikuwa na matatizo katika maeneo yao tokea mwaka Jana mwezi wa kumi lakini mpaka leo ni hadithi na mwenye pesa ndie atakamilishiwa haki ya kupata ardhi yake na sie masikini hatujui hatma yetu tunakuomba mama yetu uingilie kati mradi huu uweze kuisha ili tuendelee na shughuli nyingine za maendeleo ikiwepo ujenzi maana kodi zinatushinda watoto wanakuwa kwenye nyumba za kupanga zilizo finyu kwa kipato chetu.

Kuna wengine walichoka na zoezi hili lisiloisha wameendelea kujenga kukiuka maelekezo ya jiji ya kusimamisha ujenzi wakijiandaa kwa vita yoyote Sie wanyonge tunakuomba uingilie kati mama yetu kutuletea mkurugenzi mwingine huenda akawa na dawa kututatulia changamoto hiyo,asante.
 
Ni kweli mkuu! hata Mimi Nina kakibanda kangu huko,hao wapimaji wamenitengenezea mgogoro na jirani yangu wametuahidi marekebisho tokea mwaka Jana mwezi wa kumi mpaka Leo hakuna majibu ni sarakasi weekend hizi mbili zilizopita aliahidi kuja lkn wapi kifupi mkurugenzi nae ni sehemu ya tatizo.
 
Hapo Kuna matatizo makubwa mawili, Kwanza ni eneo lililopimwa viwanja la nzuguni A wananchi wamedai kudhulumiwa na kutokufidiwa, pili ni eneo la nzuguni A( la wenyeji) ambalo limeshindikana kurasimishwa na kila siku njia zinazibwa na makazi ya watu! Tarehe 19/06/2021 mwenyekiti wa mtaa wa nzuguni A alihairisha mkutano wa Kijiji kwa kinachodaiwa kutokufika kwa mkurugenzi wa jiji katika mkutano na badala yake akatuma wawakiloshi wasioweza kutatua kero za wananchi.
 
Hapo Kuna matatizo makubwa mawili, Kwanza ni eneo lililopimwa viwanja la nzuguni A wananchi wamedai kudhulumiwa na kutokufidiwa, pili ni eneo la nzuguni A( la wenyeji) ambalo limeshindikana kurasimishwa na kila siku njia zinazibwa na makazi ya watu! Tarehe 19/06/2021 mwenyekiti wa mtaa wa nzuguni A alihairisha mkutano wa Kijiji kwa kinachodaiwa kutokufika kwa mkurugenzi wa jiji katika mkutano na badala yake akatuma wawakiloshi wasioweza kutatua kero za wananchi.
Ni kweli mkuu! tatizo lilianzia jiji kuamua kulipima eneo la Nzuguni A
kama pori baada ya kulirasimisha
hali ya kuwa walikuta watu wameshajenga,walianza kuweka maingiliano ya mipaka kati ya mtu mmoja na mwingine kitu kinachopelekea ugomvi baina yao mpaka kushikiliana mapanga watu wanashindwa kupaendeleza kwa mujibu wa taratibu mwisho Siku wengine wengi wameamua kujijengea bila taratibu
za viwanja vilivyogawanywa,lkn pia kuna
Dada pale ofisa ardhi anayejulikana kama Oliver huyu ni 75% ya mgogoro katika eneo hilo kauza viwanja vya watu wengi,Rushwa kaiweka mbele
matokeo yake zoezi haliishi kwa mwaka wa tatu sasa,ila Jana nimesikia tangazo la mkutano wa mkurugenzi kesho jumatano ngoja tuone kitakachofanyika lkn kwa Mkurugenzi huyu hakuna hitimisho yangu macho.
 
Ni kweli mkuu! tatizo lilianzia jiji kuamua kulipima eneo la Nzuguni A
kama pori baada ya kulirasimisha
hali ya kuwa walikuta watu wameshajenga,walianza kuweka maingiliano ya mipaka kati ya mtu mmoja na mwingine kitu kinachopelekea ugomvi baina yao mpaka kushikiliana mapanga watu wanashindwa kupaendeleza kwa mujibu wa taratibu mwisho Siku wengine wengi wameamua kujijengea bila taratibu
za viwanja vilivyogawanywa,lkn pia kuna
Dada pale ofisa ardhi anayejulikana kama Oliver huyu ni 75% ya mgogoro katika eneo hilo kauza viwanja vya watu wengi,Rushwa kaiweka mbele
matokeo yake zoezi haliishi kwa mwaka wa tatu sasa,ila Jana nimesikia tangazo la mkutano wa mkurugenzi kesho jumatano ngoja tuone kitakachofanyika lkn kwa Mkurugenzi huyu hakuna hitimisho yangu macho.
Mkurugenzi alifika
 
Mheshimiwa Rais sisi wakazi wa Nzuguni A tunakuomba uingilie kati zoezi hili lisiloisha kwa wenye makazi na viwanja katika eneo la Nzuguni A.

Zoezi hili linakaribia mwaka wa tatu lakini imekuwa linaenda kwa kusuasua sana urasimu umekuwa ni mwingi l, ubabaishaji na Rushwa imekithiri kupelekea watu kupoteza haki zao na kupelekea malalamiko mengi yasiyoisha kupelekea kukwamisha ukamilikaji wa mradi huo.

Binafsi ni mmiliki wa ardhi katika eneo hilo pindi nilipotaka kuanza ujenzi baada ya kukopa katika vikoba kulitolewa katazo la kutoendeleza chochote kwa miezi sita mpaka zoezi litakapokamilika basi nilivulia kwa kipindi hicho na sasa ni mwaka wa 3 hakuna kinachoeleweka kwa asilimia kubwa ya milimiki tuliozuiwa kuendelea kwa ujenzi, kwani maeneo mengi ya viwanja walivyopima wameweka maingiliano yaliyosababisha watu kushikiana mapanga,wengine viwanja kumegwa kutokana na miundombinu bila kuainisha utafidiwa vipi, asilimia kuwa tulionunua ardhi huku ni masikini basi imekuwa ni uonevu kupata haki na wale wanaojiweza wamejenga kwa kutumia nguvu zao.

Baada ya malalamiko mengi tuliadiwa kufanyiwa marekebisho kwa wale walikuwa na matatizo katika maeneo yao tokea mwaka Jana mwezi wa kumi lakini mpaka leo ni hadithi na mwenye pesa ndie atakamilishiwa haki ya kupata ardhi yake na sie masikini hatujui hatma yetu tunakuomba mama yetu uingilie kati mradi huu uweze kuisha ili tuendelee na shughuli nyingine za maendeleo ikiwepo ujenzi maana kodi zinatushinda watoto wanakuwa kwenye nyumba za kupanga zilizo finyu kwa kipato chetu.

Kuna wengine walichoka na zoezi hili lisiloisha wameendelea kujenga kukiuka maelekezo ya jiji ya kusimamisha ujenzi wakijiandaa kwa vita yoyote Sie wanyonge tunakuomba uingilie kati mama yetu kutuletea mkurugenzi mwingine huenda akawa na dawa kututatulia changamoto hiyo,asante.
Mmeshapimiwa mkuu mbona kimya
 
Back
Top Bottom