Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke aache kutisha na kufedhehesha Waandishi wa Habari

Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke aache kutisha na kufedhehesha Waandishi wa Habari

alexander paulo

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2011
Posts
492
Reaction score
155
Jana wakati nafuatilia taarifa ya habari ITV saa mbili usiku niliona mgogoro ulipo katika kiwanja mojawapo kilichopo Yombo wilaya ya Temeke lakini wakati mwandishi wa habari anatafuta ukweli wa jambo hilo alipojaribu kumpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ajulikanaye kwa jina la Lusubilo Mwakabibi nataka ufafanuzi wa mgogoro huo kwa kuomba nafasi ya kuonana naye ofisi kwake aliishia kujibiwa kuwa huyo mwandishi hana hadhi ya kuonana naye! Swali ni je wenye hadhi ya kuonana na viongozi hawa ni waandishi wa namna gani?

MKURUGENZI WA MANISPAA YA TEMEKE AACHE KUTISHA NA KUFEDHEHESHA WAANDISHI WA HABARI!

Tarehe 2 Desemba 2020, ITV ilikuwa na taarifa kuhusu kero ya wananchi katika Manispaa ya Temeke. Mkurugenzi wa Manispaa ambaye ni Mteule wa Rais anapigiwa simu na mwandishi wa habari wa ITV kutaka ufafanuzi kuhusu jambo muhimu la kijamii lenye masilahi kwa taifa. Badala ya kujibu au kutoa ushirikiano kwa mwandishi wa habari, yeye anaamua kumfokea mwandishi wa habari kwa kumwambia kuwa, yeye (Mkurugenzi) siyo saizi yake (mwandishi wa Habari), hivyo aliyetakiwa kumpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ni Mkurugenzi [wa ITV?] na wala siyo mwandishi yule wa habari.


Vyombo vya Habari na Waandishi wa Habari katika nchi hii wasipozinduka watakuwa wanakaripiwa na kila Mtendaji wa Serikali. Uhuru wa Vyombo vya Habari katika nchi hii umewekwa mfukoni mwa Serikali na hili la Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke kumfokea mwandishi wa Habari wa ITV ni kielelezo kimojawapo!

Tunamuonya Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, ndugu Lusubilo Mwakabibi, kuacha tabia ya kuwafokea, kuwadharau na kuwatisha waandishi wa habari. Anahitaji kuwa mnyenyekevu kwa kuwa anakalia ofisi ya umma inayoendeshwa kwa kodi za Watanzania! Kama tuliwahi kuwakemea na kuwaonya wengine, ni wajibu wetu kumkemea na kumuonya na yeye pia! Tunaomba rehema kwake ili atambue kuwa alilofanya halikuwa jema machoni pa Watanzania.

Tunaishauri Serikali isianze kumfuatilia Mwandishi wa ITV aliyeripoti tukio lile na wala ITV isifuatiliwe kwa kurusha hewani tukio lile. Badala yake Serikali ijikite katika kuwaonya na kuwaelekeza watendaji wake kujirekebisha. Tunamshauri pia Mwakabibi asianze kumfuatilia mwandishi, bali ikiwezekana amuombe msamaha mwandishi yule na ITV yenyewe kwa kumnyanyasa mwandishi wake!

Tunatimiza wajibu wetu wa kikuhani kwa Serikali na jamii kwa ujumla (Ezekieli 33:1-20)!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
 
Jana wakati nafuatilia taarifa ya habari ITV saa mbili usiku niliona mgogoro ulipo katika kiwanja mojawapo kilichopo yombo wilaya ya Temeke lakini wakati mwandishi wa habari anatafuta ukweli wa jambo hilo alipojaribu kumpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ajulikanaye kwa jina la lusubilo mwakabibi nataka ufafanuzi wa mgogoro huo kwa kuomba nafasi ya kuonana naye ofisi kwake aliishia kujibiwa kuwa huyo mwandishi hana HADHI ya kuonana naye! swali ni je wenye hadhi ya kuonana na viongozi hawa ni waandishi wa namna gani?
Malaika
 
Jana wakati nafuatilia taarifa ya habari ITV saa mbili usiku niliona mgogoro ulipo katika kiwanja mojawapo kilichopo yombo wilaya ya Temeke lakini wakati mwandishi wa habari anatafuta ukweli wa jambo hilo alipojaribu kumpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ajulikanaye kwa jina la lusubilo mwakabibi nataka ufafanuzi wa mgogoro huo kwa kuomba nafasi ya kuonana naye ofisi kwake aliishia kujibiwa kuwa huyo mwandishi hana HADHI ya kuonana naye! swali ni je wenye hadhi ya kuonana na viongozi hawa ni waandishi wa namna gani?
Nadhani ni kulewa tu kamshahara na tuposho ambatwo wamepata hapo juzijuzi
 
Mwaka 2015 aligombea ubunge Rungwe akashindwa kura za maoni.

Akateuliwa kuwa mkurugenzi wilaya fulani huko Kigoma.

Baada ya uchaguzi mdogo huko ambao ulotokana na kifo cha Kasuku Bilago wa CHADEMA, na CHADEMA kupoteza Jimbo wakiwa na Eliya Michael wao, ambaye kwa sasa nasikia ni kada kindakindaki na mtendaji kata, Mwaka alihamishiwa TMK
 
Mwaka 2015 aligombea ubunge Rungwe akashindwa kura za maoni.

Akateuliwa kuwa mkurugenzi wilaya fulani huko Kigoma.

Baada ya uchaguzi mdogo huko ambao ulotokana na kifo cha Kasuku Bilago wa CHADEMA, na CHADEMA kupoteza Jimbo wakiwa na Eliya Michael wao, ambaye kwa sasa nasikia ni kada kindakindaki na mtendaji kata, Mwaka alihamishiwa TMK
Kada kindakindaki wa chama gani
 
Nadhani ni kulewa tu kamshahara na tuposho ambatwo wamepata hapo juzijuzi
Sio kweli huyo jamaa pesa anayokitambo tu na sio mtu wa njaa sema Ni amezaliwa hivyo Ni mtu mpenda sifa na utani wa hapa na pale .

Namjua kwa kias chake coz tunatoka sehem moja huko Budokelo -Mbeya .

Kwanza jamaa wanadai Ni kitengo.

Pia huyu jamaa kudhihirisha kuwa hana njaa huko kijijin kwao amejenga bonge moja la bangaloo Ni hatar na nusu .

So elewa jamaa hana njaa kabisa wala hawez kulewa kamshahara ka Uded so uelewe jamaa ndivyo alivyo zaliwa ,utani mwingi ,vituko vya hapa na pale ,sifa za hapa na pale ,pia Ni mtu wa watu sana hana shida.
 
Jana wakati nafuatilia taarifa ya habari ITV saa mbili usiku niliona mgogoro ulipo katika kiwanja mojawapo kilichopo Yombo wilaya ya Temeke lakini wakati mwandishi wa habari anatafuta ukweli wa jambo hilo alipojaribu kumpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ajulikanaye kwa jina la Lusubilo Mwakabibi nataka ufafanuzi wa mgogoro huo kwa kuomba nafasi ya kuonana naye ofisi kwake aliishia kujibiwa kuwa huyo mwandishi hana hadhi ya kuonana naye! Swali ni je wenye hadhi ya kuonana na viongozi hawa ni waandishi wa namna gani?
Mitano tena, hii ndiyo CCM halisi
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Sio kweli huyo jamaa pesa anayokitambo tu na sio mtu wa njaa sema Ni amezaliwa hivyo Ni mtu mpenda sifa na utani wa hapa na pale .

Namjua kwa kias chake coz tunatoka sehem moja huko Budokelo -Mbeya .

Kwanza jamaa wanadai Ni kitengo.

Pia huyu jamaa kudhihirisha kuwa hana njaa huko kijijin kwao amejenga bonge moja la bangaloo Ni hatar na nusu .

So elewa jamaa hana njaa kabisa wala hawez kulewa kamshahara ka Uded so uelewe jamaa ndivyo alivyo zaliwa ,utani mwingi ,vituko vya hapa na pale ,sifa za hapa na pale ,pia Ni mtu wa watu sana hana shida.
Hasafishiki hata kwa jiki acha kumpaisha huyo mlevi ma madaraka. Eti huna hadhi ya kuonana na mimi. Yeye kama nani? Wameondoka waliokuwa na mamlaka kina mkapa na wakawekwa uwanjani siku karibia tatu akina mahiga waliokuwa na heshima zao lakini uliona msiba wake ulivyokuwa

Aache dharau.
 
Nadhani ni kulewa tu kamshahara na tuposho ambatwo wamepata hapo juzijuzi

Kama ni kweli basi huyu Lusubilo Mwakabibi atakua amepoteza hadhi ya kuwa mkurugenzi sasa
Halafu kitu cha kawaida sana alichoulizwa kwanini amepanick kama mwizi?

Maendeleo hayana vyama
 
Hasafishiki hata kwa jiki acha kumpaisha huyo mlevi ma madaraka. Eti huna hadhi ya kuonana na mimi. Yeye kama nani? Wameondoka waliokuwa na mamlaka kina mkapa na wakawekwa uwanjani siku karibia tatu akina mahiga waliokuwa na heshima zao lakini uliona msiba wake ulivyokuwa

Aache dharau.
Naomba unielewe Ndugu sipo hapa kumsafisha huyo jamaa .ila nimekwambia ndivyo alivyo hayupogo sirias sana Ni mropokaj sana .

Sasa nimsafishe kwa kipi ,nimeongea ivo coz namjua kwa kiasi maana natoka nae sehem moja japo vijiji tofaut huko Busokelo-Mbeya .

Hata huko home Ni maaluf sana sabab ya vituko vyake vya hapa na pale ,lakin tukirud kwenye ukwel jamaa hana shida kabisa na Ni mtu wa watu sana
 
Jana wakati nafuatilia taarifa ya habari ITV saa mbili usiku niliona mgogoro ulipo katika kiwanja mojawapo kilichopo Yombo wilaya ya Temeke lakini wakati mwandishi wa habari anatafuta ukweli wa jambo hilo alipojaribu kumpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ajulikanaye kwa jina la Lusubilo Mwakabibi nataka ufafanuzi wa mgogoro huo kwa kuomba nafasi ya kuonana naye ofisi kwake aliishia kujibiwa kuwa huyo mwandishi hana hadhi ya kuonana naye! Swali ni je wenye hadhi ya kuonana na viongozi hawa ni waandishi wa namna gani?
Huyu Mkurugenzi ni kiongozi wa hovyo kuwahi kutokea. Nilisikia mbwembwe zake. Hana sifa ya kuwa kiongozi bali jambazi. Nafikiri ana backup nzuri ya kufanikisha yakiyofanikishwa hivyo ndiyo maana alipayuka hovyo. Kiongozi hana maadili. Very poor communication skills.
 
Back
Top Bottom