Mkurugenzi wa VODACOM, TIGO, ZANTEL, TTCL, AIRTEL pitieni hapa, huwenda kukawa kuna faida kwenu

Mkurugenzi wa VODACOM, TIGO, ZANTEL, TTCL, AIRTEL pitieni hapa, huwenda kukawa kuna faida kwenu

Wazo ni zuri, lakini ili liwe na ufanisi kuwe na mtu wa kati ambaye kazi yake itaakuwa akuwaunganisha muuzaji na mnunuzi, huyu mtu wa kati atatengeneza regulations zitakazo linda pande zote mbili, pia atahold fedha mpaka muuzaji atakapo tuma mzigo kikamilifu na mnunuzi atakapo pokea mzigo ukiwa sawa.

Huyu midle atapata cammision tu.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Wazo zuri...ila badi halijakidhi haja 100% ya lengo tarajiwa.

1. Vipi pale mnunuzi anapokuwa hana uamjnifu na hatumi hizo namba za uthibitisho kwa muuzaji baada ya kupokea bidhaa??

2. Mtandao wa simu unakuwa na uthibitisho gani wa kuwa bidhaa imefika au haijafika pale mnunuzi unapoamua kutotuma code ya uthibitisho ??

3. Mitandao ya simu inakuwa inabeba dhamana ya mtu wa kati kati..Je,wanafaidikaje na muamala huu ukiacha ada za kawaida za utumaji na kupokea ??
Ukijibiwa naomba unitag kiongozi
 
LIPA KWA UTHIBITISHO

Kutokana na wimbi kubwa la utapeli mitandaoni, kundi hili hupelekea biashara zingine za mtandaoni zilizo halali kufifizwa na kutoaminiwa. Hivyo kuwakosesha riziki wale wafanya biashara waaminifu mtandaoni. Kwasababu maisha ya sasa hayawezi kwenda bila mitandao ya kijamii, bishara na huduma zote zimehamia huko.

Hii ni njia ambayo itawasaidia wanunuzi na wauzaji wa bishara kwa njia ya mtandao, ambapo muuzaji atapoakea pesa ya muamala wa malipo lakini hataweza kuitoa pesa hiyo mpaka ithibitishwe na mnunuzi au mlipaji baada ya kupokea mzigo husika.

Jinsi mfumo ulivvyo

Mnunuzi amekiona kitu mtandaoni, kisha anatakiwa akilipie hicho kitu kwa njia ya muamala kabla ya kukipokea au kabla hakijamfikia, sasa njia hii itamruhusu mnunuzi kulipia hiyo bidhaa bila hofu, na muuzaji atapokea muamala wa malipo kutoka kwa mnunuzi ili kuweka uwaminifu baina ya muuzaji na mnunuzi.

LAKINI, muuzaji hatoweza kuitoa pesa hiyo mpaka apate namba ya uthibitisho kutoka kwa mnunuzi, na vilevile mnunuzi akishalipa hatoweza kuitoa au kuirejesha pesa hiyo kwenye account yake mpaka apate namba ya uthibitisho kutoka kwa muuzaji. Kwa maana yake watategemeana.

Kwa mfano

Mnunuzi
ameona TV ikitangazwa instagram inauzwa Tsh 500,000/=, lakini yeye yuko Dodoma, na Muuzaji yuko Dar es salaam.

Kwenye menu ya M PESA wekeni kipengele kinaitwa Lipa kwa uthibitisho.

Mnunuzi ataingia kwenye kipengele cha Lipa kwa uthibitisho kisha atatuma pesa taslim TSH 500,000/= kwenda kwenye namba ya Muuzaji 07567563890 kwa ajili ya ununuzi wa TV

Mnunuzi atapokea meseji ya uthibitisho kwamba muamala umefika kwa muuzaji, meseji itaambatana na namba ya uthibitisho labda 7689

Huku kwa Muuzaji, nayeye atapokea muamala wa TSH 5000000/= kutoka kwenye namba ya Mnunuzi 06517271992
Muamala huo utaambatana na namba ya uthibitisho, labda 8126

Sasa, Mnunuzi baada ya kupokea mzigo na kuhakikisha ni wenyewe kwa uhakika, atamtumia namba yake ya uthibitisho yule muuzaji ambayo ni 7689 kwa njia ya kawiada yaani sms,

Kisha huyu Muuzaji nayeye atamatumia mnunuzi namba yake ya uthibitisho ambayo 8126 kwa njia ya kawaida.

Ambapo Muuzaji ataingia kwenye menu ya M PESA kipengele cha Liba kwa uthibitisho kisha ataingia kipengele Thibitisha muamala ulio tumiwa kisha weka namba ya uthibitisho kutoka kwa mnunuzi,ataweka 7689 , akishaweka ataambiwa subiri muamala kuthibitishwa.

Kwa upande wa Mnunuzi, ataingia tena kwenye menu ya M PESA kipengele cha Lipa kwa uthibitisho kisha Thibitisha muamala ulio tuma kisha weka namba ya uthibitisho kutoka kwa muuzaji 8126, akishaweka tu, Muuzaji kule atapokea meseji ya muamala kamili yaani muamala wa kawaida ambao ataweza kuitoa hiyo pesa kwa wakala au kumtumia mtu au kufanya vyovyote vile. (Yaani kwa kifupi ndio inakuwa imeingia rasmi kwenye account yake)

ENDAPO MNUNUZI AKIKATAA KUWKEA HIYO NAMBA YA UTHIBITISHO KUTOKA KWA MUUZAJI, HIYO PESA INABAKIA VODACOM. AMBAPO MNUNUZI NAYEYE HATAWEZA KUITOA.

Kwa mfumo huu, hakuna mtu atakaye uziwa au kuagiziwa bidhaa hewa au yenye utofauti, pia utapeli wa uuzaji na ununuzi utapungua.

Vingine mtaongezea kutokana na Dira niliyoitoa kama nimeelewa.
Hata mimi hili wazo la escrow account nilitaka kulifanya mimi ila nilikuwa nawaza vibali nitapewa. Wenzetu kenya wana makampuni binafsi wanafanya hii kitu.

wanakupa hadi code ya kuintergrate na online shop yao. Mfano mtu kapenda kitu analipia, muuzaji anaona kuwa mzigo umelipiwa pesa anaiona lakini iko kwenye escrow account, mzigo ukimfikia mteja ataruhusu pesa iende kwa muuzaji aitoe. Kama akisema mzigo haujafika, pesa hairudi kwa muuzaji bali kinachotokea ni kwamba hapo mnarise mgogoro, kila mtu atatuma ushahidi wake, assume labda muuzaji atatuma ushahidi wa kusafirisha mzigo kwa kuonyesha lisit ya basi namba ya kampuni na kadhalika ushaidi wa msg na kila kitu, sasa itakuwa kazi ya watoahuduma kujua nani anasema ukweli ndo muamala uende kwake.

Hata bitcoin local bitcoin iko hivyo, unachagua wa kununua bitcoin kwake, assume za dollar mia, automatically bitcoin zinatoka kwake zinaingia kwenye escro account, anapokea alert, anakuja hewani unafanya malipo assume kwa paypal, then unarudi unabonyeza nimelipa yeye kule anaconfirm zinakuja kwenye wallet yako, in case akigoma basi hairudi kwake mnaingia kwenye mgogoro, wewe kama kweli ulilipa utawatumiaushahidi wa screenshot ya muamala na ushahidi mwingine watajua kama anadanganya waziachai zije kwako.
 
Wazo ni zuri, lakini ili liwe na ufanisi kuwe na mtu wa kati ambaye kazi yake itaakuwa akuwaunganisha muuzaji na mnunuzi, huyu mtu wa kati atatengeneza regulations zitakazo linda pande zote mbili, pia atahold fedha mpaka muuzaji atakapo tuma mzigo kikamilifu na mnunuzi atakapo pokea mzigo ukiwa sawa.

Huyu midle atapata cammision tu.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Inabidi itengenezwe system kabisa ya escrow account Kenya wanafanya hiki kitu hata mimi lilikuwa wazo langu muda sema nilijua itahitajivibari na capital kufanya hii kitu. Hili wazo nililitoa kwa PayPal to Mpesa within 5 minutes maana nafanya nao transactions sana na moja ya huduma wanazotoa ni hii kwa wafanyabiashara wa kenya
 
Wazo ni zuri, lakini ili liwe na ufanisi kuwe na mtu wa kati ambaye kazi yake itaakuwa akuwaunganisha muuzaji na mnunuzi, huyu mtu wa kati atatengeneza regulations zitakazo linda pande zote mbili, pia atahold fedha mpaka muuzaji atakapo tuma mzigo kikamilifu na mnunuzi atakapo pokea mzigo ukiwa sawa.

Huyu midle atapata cammision tu.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Idea ya another middle-person mbali na makampuni ya mitandao yenyewe ni unnecessary addendum & retarding bureaucracy.
 
wazo zuri ila halitekelezeki sababu kuna mambo yanafanyika nje ya mfumo na inahitaji tena uaminifu wa muuzaji na mnunuzi kukamilisha, chukua mfano wa aliexpress ukilipia kitu pesa wanakaa nayo wao mzigo ukifika seller ndio analipwa hii njia kwao inawezekana sababu wana tracking system ya kujua mzigo ulipo toka umetumwa.
Njia rahis ini kumtuma mtu aukague mzigo kabla hujanunua au tuwe na mfuoma kama wa amazoni au aliepress katika kufanya manunuzi.

Kabisa, hapa ni kutengeneza namna ya kusajili sellers/suppliers kwenye mfumo fulani ambao wao watalipia usajili na vile vile hawa wasajili ndio watakuwa washika dhamana ya hizi transactions. Making sure the buyer is buying from a credible, verified and certified seller.
 
Japan kwenye mitandao kuna kitu kinaitwa paytrade ambapo ukilipa unamlipa mwenye web kisha saler anakutumia gari akishakamlisha process zote na gari ikaingia kwenye meli na docs zote ukitumiwa ndio mwenye web anarelease pesa kwa saler.
 
Mnunuzi akiwa hana uwaminifu ni kwamba hiyo pesa aliyotuma hataweza kuitoa wala kuirejesha kwenye accounta yake. Sasa sidhani kama mtu umepokea mzigo ambao ni wenyewe, na pesa umeshalipa inachobakia ni kuthibitisha ili mtu apokee, kwasababu hata usipo thibitisha pesa hairudi kwako inabakia kwa mtandao husika.
Lakini mzigo ameshachukua.
 
hiyo njia ni ndefu, pia itahitaji mpesa wapate commission.

Kuibiwa hakuwezi kwepeka. inategemea na inteligensia ya muuzaji na mnunuaji.

kitu ninachokiona ni kibaya ni pale unauza kitu, unatumiwa muamala feki au unatumiwa pesa inaingia halafu mtu anapiga simu kuomba irudishwe as if amekosea muamala.

cha kufanya ni issue moja.

Muuzaji awe na uwezo wa kutengeneza quote. ambayo ina maelezo na bei ya huduma au bidhaa inayouzwa na kisha kisha mlipaji atapewa quote ya namba kisha itakuwa reference wakati analipa pesa.

So hapa tutaepuka miamala feki ike inayokujaga na Msg ya Mpesa/ Tigopesa pia pesa ikiingia kwenye hiyo quote, mnunuaji hawezi reverse muamala mpaka makubaliano maalum
Hii dawa mbona ipo? Biashara yeyote inayofanyika kimtandao lazma uwe na namba ya lipa na ...njia hii muamala haurudishwi mpaka voda wakupigie simu kwanza
 
Nani anayesimamia njia ya usafirishaji wa bidhaa mpaka kumfikia mteja na kuna ushahidi upi unaothibitisha kuwa bidhaa imefika?.
 
Kenyaa wameshaanzaa kutumia hii mifumo, kuna kitu wanakiita pay protect... Mtoa wazo huko sahihi sana nadhan hili linawezekana sn linahitaji vinyama nyama kidogo.

Narudi.
 
Nani anayesimamia njia ya usafirishaji wa bidhaa mpaka kumfikia mteja na kuna ushahidi upi unaothibitisha kuwa bidhaa imefika?.
Bila shaka wewe ni miongoni mwa wanaokomenti ama bila kusoma mada au kutoielewa. Hata ungezuga kupitia komenti kadhaa ungepata majibu ya kina kuliko hata swali lako lenyewe. Alisemaaa, alisema, alisema Jumbe alisema, vijana wangu wote wamelegea! Uvivu ni ugonjwa mbaya & hatari sana.
 
Ahsante, yani hapa mtu wa kati ni M PESA yenyewe, lakini wao hawaingilii mifumo yenu ya biashara. Kwa mfano una mwanao ambae ni mfujaji wa pesa, sasa unataka kumtumia ada ya semister II, lakini muda wa semister II haujafika na unajua dhahiriri nikimpa hii pesa cash ataisambaratisha, sasa unamtumia kwa njia hii, kwasababu hataweza kuitoa mpaka apate namba ya uthibitisho kutoka kwako nawewe hii pesa haitarudi kwako. Kwa maana yake hautakuwa na matumizi nayo tena.. kwasababu lengo lake ni aipate mwano kwa ajili ya ada ya chuo, muda ukifika unamtumia namba ya uthibitisho akaitoe.
Huo ni mfano nimekupa ili uelewa namna mfumo unafanya kazi
Mfano umeeleweka vizuri. Lakini kama mantiki ni kutuma pesa kwa mfumo huu ili ikawe withheld kwa muda hadi wakati wa kulipa "ada," why usimtumie tu kwa muda mwafaka wa ulipaji???
 
Ishu ninayoiona anahitajika wakala a-konfirm kama mzigo umechukua au la.Wenye mabasi na posta wana nafasi ya kuthibitisha na kukupa confirmation recept no. ambayo utaituma kwa mnunuzi ili atoe hela yake, au u maduka ya uwakala wa mtandaoni yaanzishwe na yapewe nguvu ya kisheria bila kuathiri utaratibu uliopo.
 
Bila shaka wewe ni miongoni mwa wanaokomenti ama bila kusoma mada au kutoielewa. Hata ungezuga kupitia komenti kadhaa ungepata majibu ya kina kuliko hata swali lako lenyewe. Alisemaaa, alisema, alisema Jumbe alisema, vijana wangu wote wamelegea! Uvivu ni ugonjwa mbaya & hatari sana.
Haya sasa!.
 
Back
Top Bottom