Uchaguzi 2020 Mkutano Mkuu wa CCM 2020 wamchagua John Magufuli kuwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Amteua Samia Suluhu kuwa Mgombea Mwenza

Nilikosea ni Jim Brown hivi huyu. Ni ndugu yako,? Sisi tunamwita Truck turner? Tusalimie Bashite na Kardinali wako pengo

Tatizo lako hutaki mjadala wenye afya....nimeshafafanua mengi tena vya kutosha,lakini kwa kuwa "unapigana jihadi isiyoeleweka" inakufanya utamalaki na ARGUMENTUM AD HOMINEM....Umekuwa ukipotosha hata KUHUSU asili yangu......Basi endelea kufika "orgasm" kwa KUPWAGAPWAGA maneno......
 
Hii Ndiyo Raha ya kuwepo mawazo mbadara (upinzani)

Uzushi na uzandiki uko siasani, Kesho tukutane Church ama Masjid Ijumaa ili kutubia huu uwongo wa kizembe
 
Mkuu, utaratibu huu WA hawa Jamaa CCM ndio umeanza mwaka huu wa kuwa na mchukua fomu ya Uraisi mmoja tu ambapo mgombea hajakamilisha vipindi vyake viwili, binafs sikumbuki kama kumewahi Kutokea kushindanishwa na mgombea mwingine Kwa anayeendelea hajakamilisha awamu zake 2
 

Kutokana na sifa za ccm ya awamu hii, ni kuwa ccm hii ni mpya na haifanyi mambo yake kwa mazoea. Na kama ulimsikia Bashiru leo akiongea, anasema walitarajia kuwe na wagombea watatu safari hii, lakini watu hawakujitokeza kuchukua fomu. Sasa ili na ww uwe unacheza vizuri na upepo, tafuta uje na hoja ipi ya utetezi kati ya hizo. Kinyume na hapo utachekesha hapa.
 
Sasa wewe unabisha nini mkuu? Je, kuna mtu alienda kucbukua form akanyimwa?

Sent from my SM-T585 using JamiiForums mobile app
 


Nafasi za WALIONUNULIWA zilikuwepo...Waliwatenga
 
Na Emmanuel J. Shilatu

Napenda niungane na Mamilioni ya Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Watanzania kwa ujumla kumpongeza Mwenyekiti CCM Taifa na Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuandika historia ya aina yake kwenye mkutano Mkuu wa CCM Taifa uliofanyika leo Julai 11, 2020 mjini Dodoma.

Kwanza, Dkt. Magufuli amethibitishwa kwa kupigwa kura ya ndio na Wajumbe 1822 wote sawa na asilimia 100 kupeperusha bendera ya CCM kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka huu utakaofanyika mwezi Oktoba, 2020.

Haijawahi kutokea katika historia ya miaka yote ndani ya CCM Mgombea kwa nafasi ya Urais kupitishwa kwa asilimia 100. Mwaka 2015 Dkt. Magufuli alipitishwa kwa asilimia 87. Ongezeko hili ni ishara ya kubaliko la uadilifu, uzalendo, ufuatiliaji, uchapa kazi, ukweli na ucha Mungu alionao Dk. Magufuli kiuongozi.

Pili, Dk. Magufuli akiwa Mwenyekiti wa Kikao amewadhihirishia Watanzania na Dunia kwa ujumla juu ya Demokrasia iliyokomaa, uwazi na Uhuru wa uchaguzi ndani ya CCM kwa kura kupigwa wazi wazi na kuhesabiwa wazi wazi tena ikionyeshwa mubashara (live) na vyombo vya habari. Hii rekodi ameivunja na haijawahi kutokea katika historia ya Miaka yote ya chaguzi za CCM kwenye nafasi ya kumpata Mgombea Urais.

Hakika, Dk. Magufuli alivyosema uchaguzi wa mwaka huu atahakikisha unakuwa wa huru na haki alimaanisha na anaonyesha kivitendo kuanzia ndani nyumbani kwake (CCM).

Narudia tena kusema historia aliyoiandika Dkt. Magufuli ni ya aina yake inayompambanua kivitendo kuwa Mwamba na mkufunzi wa Dunia juu ya siasa safi, Demokrasia ya kweli na Uhuru wa uchaguzi.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki CCM
Mungu Mbariki Dk. Magufuli

*Shilatu E.J*
 
Kwa uwoga wa ccm ile hata angetaka asilimia 500 angepata.
 
Nani alithibitisha kuwa wote walimpigia kura ya NDIYO?
 
Mtapinga sana lakini -Chanda chema huvikwa pete. Rais amefanya mengi makubwa.Hii ni ishara tosha kwenye uchaguzi wa oktoba si chini ya asilimia 98. Mtaona.Viva JPM VIVA TZ VIVA CCM. God bless our country
 
Kungekuwa na wagombea wawili au zaidi alafu angepata aslimia 💯 hapo ndio ingekuwa historia sasa.
 
Hiyo ridhaa hatuwapi ng'oo, tushawashitukia, kwanza hamjui mnataka nini! Kila siku kudandia hoja, mnasubili CCM waseme ndo nanyie mapovu yawatoke! Mawakala wakubwa wa Beberu nyie, mtasubili sana kuwaachia hii nchi. Shubamiti
Cdm haishindani kukupita chama fulani, bali cdm inasaka ridhaa ya wananchi kukaa madarakani kwa ridhaa yao. Idadi ya wabunge wanashindania vyama vilivyoamua kuwa michepuko ya ccm.
 
Kwani magu alikuwa na mpinzani kweli yaani unajitekenya unacheka mwenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…