Uchaguzi 2020 Mkutano Mkuu wa CCM 2020 wamchagua John Magufuli kuwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Amteua Samia Suluhu kuwa Mgombea Mwenza

Tushawazoea kila siku ngonjera, na visingizio kibao! Ushindi wa wabunge na madiwani hadi upinzani uliongoza baadhi ya halmashauri na majiji ulikuwa ni tume ipi? Kipindi bunge halijavunjwa ndo mngekaa wabunge na kutunga sheria ya hiyo tume huru ila kwa ujinga wenu badala ya kukaa bungeni mjadili vya maana mkakalia migomo ya kutokuingia Bungeni na kujadili vitu vya kijinga, eti kuikwamisha serikari. Kipindi hiki cha uchaguzi eti mnataka tume huru, itoke wapi sasa? Subilini uchaguzi uishe ndo hayo mkajadili bungeni sio sasa!
 
Unaongea na mimi utafikiri mimi ndo mbunge, mi ni mwanchi tu apart from that sio mwanasiasa wa chama chochote zaidi zaidi ninayo kadi ya ccm. Mkuu acha kujitoa ufahamu we unajua jinsi badiriko ya sheria yanavyopelekwa bungeni, unafahamu anayeanzisha mchakato na kuuwasilisha bungeni na jinsi unavyopitishwa. Unafikiri upinzani hata wakiwa woote hapo bungeni wanauwezo wa kupendekeza na kupitisha mabadiliko wanayoyataka?
 
Wanafiki tuko wengi duniani, hawa wenzangu wanaotoa 100% kesho wakiukwaa utawasikia wakitoa yao ya moyoni kuhusu JPM, it si a matter of time.
Baraka Obama alisema ukisikia mtu kapata 100% basi ujue....................
 
We unafikili wakitoka nje ya bunge ndo dawa?
 
We ni mgumu kuelewa, nilikuwa namaanisha chama tawala ndo kinachoweza kufanya mabadiliko yoyote ya kisheria wanayohitaji lakini upinzani hawawezi kufanya chochote hata wafanyeje.
Wananchi pia mafuvu yakirudishiwa akili, kwasasa tunaishi kwenye jamii ya kanyaga twende yaani jamii ya bora liende jamii ambayo haiwezi kuchakata fikra chanya na hasi pia unaweza kuisafisha ubongo ikafikiri unavyotaka wewe
 
Haya mambo hayapo tena CCM, wamebaki kujiteua na kujipitisha wenyewe, huku wakiwa hawafuati tena Katiba Yao.

Aibu Sana kwa Chama kilichokuwa kinajinasibu kuwa na mfumo wa kidemokrasia na Uteuzi.

Ni wakati sasa CCM kujaribu kuiga na kujifunza kutoka CHADEMA.
 
Huyu wa sasa amejichagua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…