Mkutano wa CPA toka ndani ya AICC

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Salaam,

Niko ndani ya ukumbi huu wa AICC unapofanyika mkutano wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola. CBA.

Kinachoendelea sasa ni wajumbe wameshakaa sehemu zao, unasubiriwa ujio wa Rais Kikwete kuja kufungua rasmi.
 
Last edited by a moderator:
Maandalizi yalikuwa kabambe sio shaghala baghala kama Sullivan. CBA jamaa wamejipanga vizuri. Usajili umefanyikia mahotelini wageni walikofikia hivyo hapa ukumbini ni kuingia tuu sio kama lile zogo la Sullivan usajili ukumbini.
 
Hali ya hewa huko nje ni vimanyunyu . Hapa ndani wajumbe wanapata burudani ya Brass Band ya polisi huku wakisindikizwa na filamu za vivutio mbalimbali vya utalii kwenye big screen mbili kubwa zilizomo ndani ya ukumbi.
 
Vipi wabunge wetu wamevaa suti au batiki na vitenge...lol
 
Maandalizi yalikuwa kabambe sio shaghala baghala kama Sullivan. CBA jamaa wamejipanga vizuri. Usajili umefanyikia mahotelini wageni walikofikia hivyo hapa ukumbini ni kuingia tuu sio kama lile zogo la Sullivan usajili ukumbini.


Sulllivan iliboa kupita maelezo, naona hawa wamejitahidi sana,hata huku juu wanapoandaliwa kwa ajili ya chakula napo pamependeza sana, kwa ujumla jamaa wameiandaa vya kutosha.....nitaingia Simba hall mida mida.
 
Ni CPA (Commonwelath Parliamentary Association)
 
Kama kawaida ya shughuli yoyote inayoandaliwa na waSwahili, Mswahili kamwe haachi asili yake. Lazima aingize uswahili japo kidogo. Ratiba inaonyesha mambo yanaanza saa tatu kamili. Mpaka saa nne na nusu kulikuwa hakuna taarifa yoyote ya kinacho endelea.

Ni saa nne na nusu ndipo MC akaibuka kuomba excuse ya JK kuchelewa. Kusema ukweli JK ni Mswahili tuu, hana excuse yoyote kuchelewa. Mkapa pamoja na maroroso yake, alikuwa serious. JK ni total lack of seriousness.
 
Na atachelewa sana kwa sababu ndege yake hata KIA haijatua na haijulikani itafika saa ngapi. si ajabu wakakaa humo ndani hadi jioni
 


nilikuwa nackia ngoma ngoma mfululizo nikajua mzee mzima ndio anaingia....kumbe holaaa!...
 
tunashukuru mkuu kwamba upo hapo ...embu tupe kinachoendelea sasa hivi. jee mkuu ameshaingia?
 


Na atachelewa sana kwa sababu ndege yake hata KIA haijatua na haijulikani itafika saa ngapi. si ajabu wakakaa humo ndani hadi jioni
Nawaza, kisha nawaza na kisha nawaza....
 
Makubwa madogo yana afadhali kumbe inji hii inaendeshwa na waganga waliokatazwa
 
JK ndio anaingia sasa saa hizi saa 5: 10 Watu wanasimam nyimbo ya taifa inimbwa. Wenye ukumbi wao wamewasha mtambo wa kuzuia mawasiliano. Naombeni samahani,wanajamvi wenye accses na ITV naomba muendeleze update.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…