Mkutano wa G20 ni Tanzania pekee imepeleka wajumbe wengi sana, watu 100+kuliko hata wajumbe wa Brazili mwenyeji

Sema tripu za mwisho wa mwaka zina raha yake, unanunua hata vizawadi vya Krismasi mapema vya kupelekea watoto na unauanza mwaka ukiwa umeshasevu per diem ya kutosha😏
 
Mkuu
Hivi tunasubiri waiuze Tanzania yote kwa wageni ndipo tuzinduke.

Ngoja tumalizie usingizi kwanza
 
Walikua wanatafuta record kama ile ya malandrova kule Arusha. Usikute na machawa akina Steve mengele walipewa shavu. Çcm ni laana ya hili taifa
 
Tunataka wanaccm wote waende nchi za nje ili waone Tanzania tulivyoweza kuwa na treni ya SGR nzuri ya kisasa kuliko Ujerumani(kwa mujibu wa profesari Kabudi akiwa kanisani Musoma).
TUMIA PESA IKUZOWEE.
 
Unatumia pesa zako hovyo halafu unaenda kuomba mikopo na kufutiwa madeni. Huyu rais anatakiwa kupumzishwa haraka.
Jpm alikataa mikutano ya nje lakini huyu hajui pesa ya masikini inauma
Kukosa Dira ni janga sana. Watanzania hata hatuelewi tunataka nini. Wakati wa Utawala wa Mheshimiwa Kikwete watu walimdhihaki sana kuwa ni mzee wa disco anachekacheka hovyo na wabadhirifu. Wengi tukaenda mbali zaidi inatakiwa apatikane rais Dikteta na mwenye maamuzi magumu nchi ikae sawa.

2015 Mh. Kikwete akimtambulisha mgombea urais kupitia CCM kwenye makao makuu yake alitamka maneno haya, " Tumewaletea mtu mwenye magumu ni chuma kwelikweli" . Chuma kikaingia madarakani. Maamuzi magumu tuliyaona na baadhi ya mambo aliyofanya hakuna Rais ataweza kumfikia Chuma wa Chato. Alikata safari zote nje ya nchi ili kubana matumizi.

Maajabu yakatokea tena . Tuhuma zikaja tena Rais gani anakuwa kama fundi saa hataki kutoka nje ya nchi. Tanzania sio kisiwa lazima ijiimarishe kidiplomasia. Alipoondolewa misaada watu wakawa wanamtuhumu kuhusu hali ya utengamano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na nchi nyingine kuzorota. Wengi wakalalamika kuhusu maamuzi magumu anayofanya yanaighalimu nchi kwa kulipa fidia za kesi ambazo nchi imeshtakiwa na kushindwa. Watu wakasema bora mzee wa msoga maisha yalikuwa mazuri sana pesa ilikuwepo. Alipoondoka chuma kipenzi cha wanyonge kuna watu walishangilia.

Leo imerudi version ya Kikwete lawama zimerudi tena. Kuna maamuzi anakumbukwa chuma.

Watanzania hatujui tunataka nini. Hatuna msimamo na yale tunayotaka. Tunayumbayumba kama bendera. Tumuache Rais aongeze nchi amalize muda wake
 
Hivi mnajua per diem za huko

Imagine Afisa anayeambatana na Mama analipwa Per diem ya dollar 500 Kwa Siku.

Wakikaa Siku 6 ni almost milioni 7.8 hivi za Tanzania.

Wakienda safari 70 hivi Kwa Mwaka ni almost milioni 100 hiyo nje ya Mshahara wake.

Ndiyo baadaye mnakuta watu wanajenga nyumba Madale zinaota kama Uyoga vile 🙌

#Shamba la Bibi
 

Mama ABDUL naye anakula kutokana na UREFU WA KAMBA yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…