Mkutano wa REDET: Zanzibar Tuitakayo, Ujenzi wa Uvumilivu wa Kisiasa Zanzibar

hii ndiyo ninayoitaka
 
Mada 2 zimeshashuka. Sasa ni majadiliano. Hamad Rashid kasema Zanzibar yataka genuinity at heart ili kujenga kuaminiana.Aakaonge mama mmoja mwenye umbo la jimama alipanda na mafumbo ya kimipasho mipasho na vidole juu. Sio siri nimetoka kapa ila wenyewe wamemshangilia sana. Prof. Lipumba naye amezungumza na kupiga nyundo sheria ya Uzanzibari Ukaazi ni bad law.
 
Wakati mkutano ukiendelea, nilipata fursa ndogo ya man to man na Maalim Seif nikamtupia dukuduku langu la moyoni kuhusu uchaguzi mkuu ujao, nilimuuliza nimekwenda Pemba, nimeshuhudia wafuasi wake wakiendelea kususia zoezi zima lauboreshaji wa daftari la kudumu la kupiga kura, maadam yeye na Karume weshamaliza tofauti zao, kwanini mpaka sasa hatatoa tamko rasmi kuwataka wafuasi wake wakajiandikisha?.

Seif akajibu, ni kweli yeye na Karume, wamemaliza kabisa tofauti zao, kinachoendelea sasa, tuvute subra tuone mambo yanivyokwenda, ndipo atawahimiza wafuasi wake wakajiandikishe., hawawezi

Seif amesema, matatizo ya uandikishaji ni moja ya maeneo viiini vya mgogoro, kama walisusia kutokana na matatizo, hawawezi kwenda kujiandikisha ili hali matatizo yangalipo.

Pia alininong'oneza kwa sauti ndogo ' mambo mazuri sana yanakuja, tuvute tuu subra tuone'

Huu ni uthibitisho kuwa mazungumzo ya Seif na Karume, was not only a handshake, but there is a undisclosed substance in it, only time will tell.
 
DAH!naomba mungu wasije hawa sisiemu wakawa wameshacheza ''ka-mchezo kao'' kama wanavyofanya kwenye vyama vingine vya upinzani
 
DAH!naomba mungu wasije hawa sisiemu wakawa wameshacheza ''ka-mchezo kao'' kama wanavyofanya kwenye vyama vingine vya upinzani

I think Seif kafungwa goli la kisigizo halafu hana habari. Eti Wamemaliza tofauti zao......!!! Kuona ni kuamini.......Tusubiri tuone kwani subira yavuta heri.
 
Mchezo gani? wewe subiri tu...!
tunajua!hehehe!WE KNOW YOU GUYS!lakini i won't blame you.nitawalaumu ''wao''!wamekosa msimamo,wamekuwa ''so cheap'',wamenunulika!SHAME ON THEM!
 
I think Seif kafungwa goli la kisigizo halafu hana habari. Eti Wamemaliza tofauti zao......!!! Kuona ni kuamini.......Tusubiri tuone kwani subira yavuta heri.
achana na ccm ndugu!hawa jamaa ''wamejipanga''
 
Baada ya hapo ni majadiliano ya Mustakabali Zanzibar, na Zainzibar Tuitakayo

Hii ndio nini sasa hapo juu?

Hao wanaosema tuitakayo ni kina nani?..Wazanzibari au wa-Tanzania?
Huu muafaka una maneno maana hapa naona kana kwamba wa
Zanzibari si wa-Tanzania au nimekosea?

Hebu nielimisheni.
 
Saa hizi ni lunch break, wajumbe wameombwa wajitegemee, halafu Redet, watarekebisha. Hawa Redet, ni wazuri sana kwa vile vi little brown envelopes.

Kutokana na kuwepo kwa mikutano mingi sana jiji Dar es Salaam, mawarsha, masemina, makongamano ambavyo vyote huendana na free lunch ikifuatiwa na ka brown envelope jioni, kumepelekea kuhudhuria mikutano, semina, warsha na makongamani ni profesion ya baadhi ya watu, tena wanakuwa na data ajabu, akiamka asubuhi, ni anajua kuna mkutano wapi, warsha wapi, semina wapi na kongamano wapi, hivyo ni kujipanga tuu, breakfast hapa, lunch pale, coctail kule, na dinner wapi, muhimu hasahauri registration, hivyo ni kupitia mafao yake kila kona na kurudi kwake kashiba, kalewa pombe za bure na vibahasha kadhaa, hiyo ni bara, huku Zenj no, ile kusikia tuu, watu wajitegemee, mwenzenu nimeanza kupiga miayo...
 
Hii ndio nini sasa hapo juu?

Hao wanaosema tuitakayo ni kina nani?..Wazanzibari au wa-Tanzania?
Huu muafaka una maneno maana hapa naona kana kwamba wa
Zanzibari si wa-Tanzania au nimekosea?

Hebu nielimisheni.

Its the other way round, Watanzania ndio sio Wanzanzibari, lakini Wanzazibari ni Watanzania. Kwa vile Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT, inayojiwala kwa mambo yake ya ndani, then wote tunahaki ya kuchangia kuhusu 'Zanzibar Tuitakayo'.

Kabla ya Muungano, kulikuwa na Tanganyika na Zanzibar, Tanganyika died and Tanzania was born, Zanzibar did not die, it only surendered its outomy to Tanzania and maintained its minority stake kwenye mambo yake ya jikoni na chumbani, sebuleni ni Tanzania.

Tujadili kwa uhuru tuu.
 
Ya CCM itakuwa na nondo za haja!
Kibunango, Ni kweli pepa yenu ina nondo ila pia kuna manondo ya kufa mtu, na kuna watu wanapiga nyundo!, nina kabrasha lenye mada zote kumi kwa lugha ya Kiswahili, ila sio busara, kupriempty.

Tena maada hawa ni Redet, nyie CCM hamna haja ya kuwa na shaka yoyote, always on your side, hata ikitolewa michango mizito vipi, at the end of the day maazimio ni on your (ccm)favour.
 
DAH!naomba mungu wasije hawa sisiemu wakawa wameshacheza ''ka-mchezo kao'' kama wanavyofanya kwenye vyama vingine vya upinzani
Kama ni kweli CCM wanafanyaga haka kamchezo, then hivyo vyama vya upinzani vinakafurahia hako kamchezo, ndio maana vinakubali kuchezewa, Mzee Mwanakijiji alisema mahali Watanzania 'we are screwed!' and we let the scerwer screw us more and more!, signifying we either enjoy the screwing, or we let the screwer keep on screwing us because we have no way out, hivyo anatubaka, jee vyama vya upinzani vinabakwa, ama vinafurahia ubakaji?.

Mikoa ya Kaskazini, 'first time', ni lazima ubakaji tena migombani au mikahawani, ni mikiki mikiki ila anaebakwa hapigi kelele, anabana tuu mwisho anaachia kwa mawili, ama she has no way out, akipiga kelele itakuwa aibu kwake, so she let you in, or she enjoys it and pretend to protest,

Jee vyama vyetu vya upinzani viko upande gani on the games that CCM plays?.
 
Vyama vyetu vya upinzani viko upande gani on the games that CCM plays?.
swali zuri sana!ngoja lunyungu atalijibu!......

sasa leo nimemuelewa mwanakijiji vizuri zaidi!
 
swali zuri sana!......

sasa leo nimemuelewa mwanakijiji vizuri zaidi!
.
Mwanakijiji, we achana nae, hii ni habari nyingine, hata mimi mwanzo nilikuwa simuelewi elewi, na kusema kweli, kama una kichwa chepesi, waweza toka kapa?.

Huko nyuma aliwahi kupost thread yenye kichwa cha habari PE. No 1-Sir Andy Chande, kukawa hakuna details, nikamlalamikia kuwa it was unfair, he just ignored me mpaka nliposoma mfululizo wa several threads nikaweza to connect the dots.

Ndio maana hata zile nondo zake za kazi za ka inzi, lazima uwe kichwa fulani kuzama, vinginevyo utaishia hewani.
 
Vipi suala la CUF kuikubali SMZ halijaibuka?
 

Shukran mkuu Pasco kwa jibu.

Swali lengine: Je. does Zanzibar want to increase its minority stake to equal partnership?
 
Shukran mkuu Pasco kwa jibu.

Swali lengine: Je. does Zanzibar want to increase its minority stake to equal partnership?
.
Muungano wetu sio parneship, ni annextation, yaani ni muungano wa aina yake kabisa duniani, Tanzania tumeianex Zanzibar under apron strings, hapa hakuna cha kuincrease its minority stake, but towars absolute surender into one government, not now, in future.

Zanzibar imejipanga kutingisha kibiriti kwenye suala la mafuta, eti wanayataka mafuta yaondolewe kwenye mambo ya Muungano!. Hii inahusisha kubadili katiba, kwa mujibu wa sheria yetu, mambo ya muungano yanaongezekeka tuu lakini hayapunguziki kirahisi kama uwezo wa rais kumteua tuu jaji mkuu lakini hawezi kumfuta kazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…