Mkutano wa waandishi: Lipumba, Shelukindo, TANESCO na PPRA

Mkutano wa waandishi: Lipumba, Shelukindo, TANESCO na PPRA

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, William Shellukindo alisema asingependa kuona malumbano yanayoendelea baina ya wabunge hao yanaihusisha kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.


"Tukianza kuhoji kwa nini Dk Mwakyembe ana endelea kuwa kwenye kamati yangu, kama Makamu Mwenyekiti wakati ana hisa katika kampuni hiyo, itabidi tupitie kamati zote na kuwaondoa wafanyabiashara wote," alisema Shellukindo na kuongeza:


"Kuna baadhi ya wafanyabiashara wakubwa ambao ni wajumbe katika kamati ya Viwanda na Biashara, lakini sisi hatuwasemi hata kidogo" aliongeza Shullukindo.


Aliwataja baadhi ya wafanyabiashara hao kuwa ni pamoja na Joseph Mungai, Nazir Karamagi, Rostam Azizi na Basil Mramba.


"Kama wataamua kuwa Mwakyembe atoke katika kamati hiyo, basi wengine pia waondoke kwa sababu huwa wanashiriki kutoa maamuzi mazito, yanayohusu wafanyabiashara wakati na wao ni wafanyabiashara," alifafanua Shellukindo.
Source: Mwananchi.
 
Huu sasa ndio real mgongano wa maslahi,wale waliokuwa wakipata shida ya tafsiri hiyo basi wamepata mfano mzuri zaidi.
 
tena kwa hili halina ubishi,kwani haliitaji hata kuwa na elimu ya chuo kikuu kung'amua kuwa hapa kunamgongano wa kimaslahi,na tukumbuke point moja muhimu ni kwamba,kila mbunge huwa anajipendekeza mwenyewe kuwa mjumbe wa kamati anayoitaka kutokana na mapenzi yake na ujuzi wake katika hiyo sekta....nchi ikiendeshwa kwa unafiki basi mwisho wake si mzuri
 
Conflict of interest haikulazimishi utoke kwenye kamati. Unaweza ukatoka ukitaka lakini pia unaweza uka declare tu your interests kwenye jambo linalojadiliwa.

Tatizo hawa waheshimiwa wanajadili hili jambo kisiasa badala ya kujadili sheria inasemaje.

Mwenyewe Shelukindo amesema Dr. Mwakyembe aliwahi kukataa kushiriki kwenye mjadala kuhusu kampuni yao ulipoletwa kwenye kamati. Huo ulikuwa ni mfano mzuri sana.

Kikawaida watu wakijua wewe ni mdau kwenye jambo husika, wanaangalia mchango wako mara mbili mbili.

Japo mshiriki wa jambo fulani kwenye hizo kamati inaweza kuleta conflict of interest lakini pia inaweza kuleta faida kubwa kwa kamati maana huyo mjumbe anaweza kutumia mifano halisi ya experience yake. Kwa mfano kwasababu Dr. ameanza kujishughulisha na hayo mambo ya umeme wa upepo, angeweza kutumia hiyo knowledge yake ku challenge baadhi ya mambo ya Tanesco. Lakini pia lazima awaambie ukweli kwamba na yeye ni mdau huko.
 
Mtanzania,
Mkuu wangu ktk swala la mgongano wa Maslahi nadhani hatutakubaliana kabisa kama tutaendelea kutumia mfano wa Mwakyembe ktk sakata la Richmond..Huyu jamaa hana sababu kabisa ya kufanya yanayotakiwa kisheria ikiwa hana mahusiano na Richmond..ama shirika lake haliku bet ktk tender moja na Richmond, hivi ni vitu viwili na case tofauti ingawa vi/zinafanana..
Na ndio maana kisheria alijitoa ktk kamati siku kampuni yao ilipo kuwa ilipokuwa ikijadiliwa..kwani ana interest ktk mradi uliokuwa ukijadiliwa.

Isipokuwa mimi kidogo nimeingiwa na uatata na statement ya Shelukindo alipowataja hao watu wengine ndani ya kamati zingine.. majina yao tu kuyaweka pamoja na Mwakyembe imenitisha na bila shaka... kama utaniuliza mimi Mwakyembe atolewe ktk kamati hiyo kwa sabau ya hawa watu bila shaka nitasema atolewe mara moja.. Nipo radhi kumtoa mhanga Mwakyembe kwa ajili ya kundi hilo hapo juu.. sitaki kabisa kusikia majina yao kama Mwalimu alivyokataa miaka yote kuwasikia wala kuwa karibu nao..
 
Last nails in Dowans as Tanesco shifts gear

Senior officials of the Tanzania Electric Supply Company (Tanesco) said in Dar es Salaam yesterday that the two new power-generating plants would be installed in Dar es Salaam (100MW) and Mwanza (60MW).

The company had been making losses because the cost of production did not correspond with the electricity tariffs, he added.

However, the altercation has turned ugly with Mr Aziz accusing Dr Mwakyembe of resorting to a racist campaign.

Guys, this is utterly illusion, TANESCO is not making loses because the cost of production did not correspond with the electricity tariffs as reported. The first power crisis if you can trace back your memories as emanated from severe rain shorted in TZ and thus calling for feki Richmond generator deals, the University of Dar es Salaam conducted a workshop to deliberate on the consequences of themal generation including pollution effect as hydro-generation were not more feasible. Data analysis from TANESCO showed that, thermal generation costs a maximum of Tshs. 45/- per unit and by then the tariff rates were around Tshs. 120/- per unit. This was not something of interest to the workshop as the focal point was the pollution effect due to thermal generation in Tanzania as a result of shwitching from hydro-generation to thermal following rain shorted.

For sake of this thread, this means that TANESCO was getting 62.5% profit per unit sold. Worse enough, tarif rates has never went down which I presume TANESCO is still not making loses based on weak urgument stated in that report.

Confusingly, these guys came up with the so called long term investment Plan, which needed Tshs. 300billion. Luck enough it was succesful still their giving excuses for poor performance. I thought this could lead into ecomies of scale and scope in additional to monopoly advantage the company could slash down tariff rates and extend power supply in rural areas something they have not and not thinking of.

Honestly, if TANESCO are to tell the truth, the company has never mad losses in real sense, but the dubious contracts and the government are the one draining money and thus making it unprofitable.
 
Hi uchaguzi ni miezi mingapi kuanzia sasa??????

Najaribu tu kuconnect dots.....

BM21
Ukisoma hii tarifa kuna mambo mengi sana. mfano wanapoteza 24% which is around 100plus MW eti mitambo chakavu na ndio sababu ya loss lini watafanya matengenezo hatujui more loss na eti watapata profiti next year.

wamekuwa na Deni kubwa na sasa wanapunguza deni then bado wataka kukopa 500million USD za nini????? na Kama wanatarajia kupata faida next year, kwa nini wasiwe na gradual investment plan partly financed by profit na partly financed by loan kuavoid costs of financing ambayo ndio imekuwa chanzo kikubwa cha kuerrode revenue zao???????

Dr. unatia shaka sana jinsi unavyoliendesha shirika. Mwaka huu tuhakikishe sheria inapitishwa kuhusu hela zote za compaign zinakuwa declared sources, matumizi na hata kuwe na limit ambazo mtu mmoja anaweza kuchangia chama kuondoa haya maswala ya kina RA et al kumonopolise utawala wa nchi

ni hayo tu


WAZEE WA KUCHOMA NDIZI
 
- Haya sasa a very simple hoja mnataka kulumbana bila sababu, wabunge wote wenye mgongano wa masilahi watoke mara moja kwenye kamati za bunge, kama ni muhimu kwao kuwemo kwenye kamati basi wapewe kamati ambazo hawatakuwa na mgongano wa masilahi,

- Kamati za bunge zilazimishwe kisheria kuwatumia wataalamu katika maamuzi yake muhimu kwa sababu as a nation tunao wengi sana, hoja ikiwa kamatini ipitiwe na wataalamu ambao watapewa muda wa kuipitia na kutoa mapendekezo mbadala ya kitaalamu kwa wanasiasa (wabunge) ambao ni wajumbe wa kamati, kamati itaamua ni pendekezo lipi linafaa kwa maoni yao, na then watapeleka mapendekezo yote mbadala yaliyopendekezwa na wataalamu kwenye full bunge ikiwa ni pamoja na lile walilo lipitisha kwa uamuzi wa mwisho.

- Ninasema hawa wabunge wenye mgongano wa masilahi watoke sasa, ili tuanze upya, kwenye hili tusioneane aibu wala kuangaliana usoni, dawa ni watoke mara moja!.


William.
 
Nan ndio maana tulisema wazi kuwa tatizo liko kiujumla na hivyo basi ku cherry pick ilikuwa ni sababu za kisiasa,kama tuiangalia maslahi ya Taifa tatizo litashughulikiwa as a whole,na ndio exactyly nilichokuwa nikisisitiza toka awali kwamba ubepari yumeuvamia...Angalia issue moja tu a conflict of ineterest ilivyogawanya watu hapa huku wengine wakidai wenzao hawajui maana ya conflict of interest,ndo tukasema kwamba uamuzi wa mwisho ni lazima uzingatie maslahi ya Taifa,at the same time sheria na kanuni zenye kusimamia migongano ya ki maslahi zirekebishwe ili maslahi ya watu binafsi yasije kuchanganywa na yale ya Taifa...Ila la kuzingatia ni kuwa katika mpango wowote ule hauwezi kuepeua maslahi amabyo yatakuwa ni binafsi endapo tunafuata mfumo wa kibepari...Si kila kitu anachofanya mzungu hakihitaji marekebisho, everything has to stand corrected at the time being until proven otherwise,na ndio maana unaona sciebtific theories zinabadilika kila wakati kwasababu ya new innovations,evidence etc...So wakuu mliokuwa mkitaka kumchinjia Mwakyembe baharini mnaweza kuona kuwa ni makosa makubwa na si namna ya kudeal na issue hii unless uongozi wote ujiuzuru tuanze upya.
 
..."Tukianza kuhoji kwa nini Dk Mwakyembe ana endelea kuwa kwenye kamati yangu, kama Makamu Mwenyekiti wakati ana hisa katika kampuni hiyo, itabidi tupitie kamati zote na kuwaondoa wafanyabiashara wote," alisema Shellukindo na kuongeza:


"Kuna baadhi ya wafanyabiashara wakubwa ambao ni wajumbe katika kamati ya Viwanda na Biashara, lakini sisi hatuwasemi hata kidogo" aliongeza Shullukindo.


Aliwataja baadhi ya wafanyabiashara hao kuwa ni pamoja na Joseph Mungai, Nazir Karamagi, Rostam Azizi na Basil Mramba....
Source: Mwananchi.

haya mambo hayo "ukipiga ngoma uwe tayari watu wengine wacheze". natumaini ujumbe wa shellukindo umefika kwa walengwa.
 
Katika mjadala kuhusu Richmond, ilielezwa bungeni kuwa Rostam Aziz alikwepa kuhojiwa. Lakini taarifa ilipowasilishwa bungeni, ilielezwa kuwa alichangia mjadala wa maandishi baada ya ripoti ya Mwakyembe kusema kwamba richmond ilikuwa ni mradi wa wakubwa.

Hata hivyo, katika mchango wake Rostam hakutangaza maslahi kwa kuwa yeye ni sehemu ya wanufaika wa Dowans ambayo ilikuwa imefanya biashara na Richmond.

Sasa inabidi turudi nyuma Rostam ashatakiwe kwa kulidanganya bunge na pia kukwepa kutangaza maslahi aliyokuwa nayo katika mjadala aliochangia.



Asha
 
Mtanzania,
Mkuu wangu ktk swala la mgongano wa Maslahi nadhani hatutakubaliana kabisa kama tutaendelea kutumia mfano wa Mwakyembe ktk sakata la Richmond..Huyu jamaa hana sababu kabisa ya kufanya yanayotakiwa kisheria ikiwa hana mahusiano na Richmond..ama shirika lake haliku bet ktk tender moja na Richmond, hivi ni vitu viwili na case tofauti ingawa vi/zinafanana..
Na ndio maana kisheria alijitoa ktk kamati siku kampuni yao ilipo kuwa ilipokuwa ikijadiliwa..kwani ana interest ktk mradi uliokuwa ukijadiliwa.

Isipokuwa mimi kidogo nimeingiwa na uatata na statement ya Shelukindo alipowataja hao watu wengine ndani ya kamati zingine.. majina yao tu kuyaweka pamoja na Mwakyembe imenitisha na bila shaka... kama utaniuliza mimi Mwakyembe atolewe ktk kamati hiyo kwa sabau ya hawa watu bila shaka nitasema atolewe mara moja.. Nipo radhi kumtoa mhanga Mwakyembe kwa ajili ya kundi hilo hapo juu.. sitaki kabisa kusikia majina yao kama Mwalimu alivyokataa miaka yote kuwasikia wala kuwa karibu nao..

Mkuu Mkandara,

Kwenye hili la Dr mimi nimemaliza na nimekubaliana kutokukubaliana na watu wengi sana.

Hapo juu nilikuwa natoa clarification tu ya kwamba kuwa na conflict of interest kwenye jambo fulani sio lazima ujitoe kabisa, unaweza kuendelea kuwemo ila inatakiwa useme.

Sijaona mapambano ya hoja kama kwenye hili suala kwa muda mrefu sana hapa JF. Hii ni dalili nzuri sana, pia sikuona matusi mengi, hii inaonyesha watu walikuwa serious na hii issue.

Wote tumejifunza na nakuhakikishia hata Wabunge wamejifunza na watakuwa waangalifu zaidi.
 
Hi uchaguzi ni miezi mingapi kuanzia sasa??????

Najaribu tu kuconnect dots.....

BM21
Ukisoma hii tarifa kuna mambo mengi sana. mfano wanapoteza 24% which is around 100plus MW eti mitambo chakavu na ndio sababu ya loss lini watafanya matengenezo hatujui more loss na eti watapata profiti next year.

wamekuwa na Deni kubwa na sasa wanapunguza deni then bado wataka kukopa 500million USD za nini????? na Kama wanatarajia kupata faida next year, kwa nini wasiwe na gradual investment plan partly financed by profit na partly financed by loan kuavoid costs of financing ambayo ndio imekuwa chanzo kikubwa cha kuerrode revenue zao???????

Dr. unatia shaka sana jinsi unavyoliendesha shirika. Mwaka huu tuhakikishe sheria inapitishwa kuhusu hela zote za compaign zinakuwa declared sources, matumizi na hata kuwe na limit ambazo mtu mmoja anaweza kuchangia chama kuondoa haya maswala ya kina RA et al kumonopolise utawala wa nchi

ni hayo tu


WAZEE WA KUCHOMA NDIZI

Kichakoro, hawawezi kutengeneza hiyo mitambo kwani Karamagi alipokuwa Waziri alisema Bungeni kuifanyia matengenezo mitambo yao yote na kuirudisha katika superb condition itachukua dola bilioni 1.3. Wakati huo huo kujenda bwawa la Stielgers lenye uwezo wa kutoa 2100MW inagharibu kama dola bilioni 2 hivi.

Sasa itakuwa ni ukichaa kutumia bilioni 1.2 kuwezesha kupata 100MW ambazo zinapotokea kuliko kutumia bilioni 2 kupata 2100MW. Lakini sitashangaa wakatengeneza bajeti ya hilo la kwanza na hilo la pili wakasema hawana fedha.
 
angalia hapa



then hapa.


Tender haijatolewa hivyo hakuna aliyetoa bid kuonyesha time frame lakini wao tayari wameshafanya conclussion na hata investors wanajulikana.



sababu ya kupata hasara ni high operating costs na kumekuwa na jitihada za kupunguza gharama za uendeshaji ikiwa ni pamoja na kutumia gas inayozalishwa hapa nchi ambayo ni nafuu na kusave forex but soma hapa

.

Not gas anymore WHYYYYYYYYYYYY?????????????? Tumeona trend ya bei ya mafuta inaongeza kidogo kidogo je Tanesco itaweza kufikia lengo lake la kupata faida???? Ama itaweza kupunguza bei yake kwa mlaji????

Sipendi kuita ni ufisadi lakini naona uzembe, uzalendo hakuna na labda hujuma inatengenezwa kama retaliation measure ya kukosa kununua generators za Dowans.


kwa nini miezi minne??? kama kuna tatizo la umeme, wangefanya week moja si pesa zipo $60million walizotaka kununulia Mitambo ya Dowans, kuna kampuni ambazo tayari zinazo hizo mitambo hata kama wanataka 500MW brand new leo bei yake ni $30-40million kwa 100MW plus additonal cost ya shipping na installation. Tena hii mitambo inatumia natural gas tuliyonayo hapa Tanzania.
 
Kufa ni kufaana.

Wenzetu akina Rostam Azizi na timu yake nzima wanatumia utatuzi wa matatizo yetu ya umeme ya tangu tupate Uhuru kutatua matatizo yao binafsi.

Hata rais wetu juzi pale kwenye mkutano wa alishindwa kujibu swali jepesi kuhusu uwekezaji wa kampuni binafsi na hatua ambazo serikali inachukua kuimarisha sekta hiyo.

Nilimuonea huruma sana Rais mzima wa nchi mwenye Digirii ya Political Science/ Political economy kutoka UDSM akinasa kiurahisi sana kwenye nyavu za ujinga wa kuweka wazi mwelekeo wake.
Rais hajui nini ni cha muhimu kwanza ili kujenga na kuvutia sekta binafsi katika uwekezaji nchini Tanzania.
Jibu sahihi MH Rasi Jakaya Mrisho Kikwete lilikuwa.
1 Tumejiwekea lengo ndani ya miaka(... Unataja miaka..) la kuwa na uwezo wa kudumu wa kuzalisha nguvu za nishati za kutosheleza mahitaji ya wananchi wote wa Tanzania na wawekezaji wote watakao ingia

2 Tumetenga eneo la Ukanda wa Mtwara ili liwe eneo maalumu kwa wawekezaji wote kutoka nje na wa ndani, ili kuondoa msongamano wa wawekezaji hapa Dar, kuruhusu urahisi wa kila muwekezaji kuweza kukua na kupanua eneo lake na kurahisisha serikali kuratibu na kusimamia uwekezaji huo kirahisi na kuondoa ukiritimba wote usio wa lazima.

3 Kuhakikisha tuna zalisha maji safi ya kutosha na kujenga miundombinu ya kusafisha maji taka.

4 Kumarisha mawasiliano yote kwa ujumla, ya simu( landline na zile za mkononi) pia Internet ambayo ni muhimu sana katika karne hii ya 21. tayari tumeanza kuweka mkonga wwenye uwezo wa juu zaidi katika mawasiliano mkonga wa Fiber Optic.


Kma kiingereza hakipandi isingekupa shida hiyo, unapiga Kiswahili au hata Kikwele wakwele wenzio ambao kizungu na lugha nyingine zinapanda wangetafsiri.

IZI KABISA HANARABO PREZIDENTI, A I EMU STEEL WANDARING WATI WENTI RONG APUSTEAZI THE MOMENTI THE YANGI LEDI FINMISHIDI ASIKINGI YU E KWESHENI!!!??

WERE YU STANED BY HER BUTIFU DENTO GAP (MWANYA) hIIII HIII!!!! BIKOUZI I NOO YUA WIKINESI.

Akijuacho Rais wetu ni kitu kimoja, kwamba matatizo siku zote huleta mlo lakini pia anajua wazi kwamba ni ukengeufu mkubwa kutangaza hivyo hadharani.
 
Last edited:
Taarifa:

"Tumezungumza na watu wa PPRA, TAnesco n.k tumeangalia njia mbalimbali mbadala za kuweza kuona kama tunaweza kupata umeme wa dharura kwa njia nyingine. bla bla bla

tumetambua kuwa nibora tuyanunue majenereta ya Dowans kwa sababu zifuatazo.

a. Bado ni mapya (yana umri mrefu)
b. Tayari yako nchini (hatuendi kutafuta kwingine)
c. Hakuna sheria yoyote ya manunuzi itakayokiukwa (ndiyo maana PPRA wapo hapa)
d. Dowans wako tayari kufuta kesi dhidi ya Tanesco (ndiyo maana Tanesco wako hapa)
e. Tunaamini ni kwa ajili ya maslahi ya Taifa (ndiyo maana Zitto yupo hapa)

Kwa hiyo tunaomba Watanzania watambue kuwa kununua majenereta haya ni kwa ajili ya maslahi ya taifa. Hakuna ufisadi wowote ule.

Jibu langu bado ni: HE....L.L TO THE NO!! WHY? who the f is dowans and how did they get in the country? why should a company that entered the country under false pretense be paid millions of dollars from Tanzanians taxpayers?

Kwa sababu kama wazazi wa Dowans Tanzania LImited hawakuzaliwa, Dowans haiwezi kuwepo! Otherwise, just seize and confiscate the damn turbines. Don't we have any bowls left/

Subutu, hukumbuki ya Nyerere kutaifisha kampuni ya kuunganisha materekta, ilimtokea puwani na ujanja wake wote ukamwisha, akairudisha kwa wenyewe (NADHANI WALIKUWA MAKABURU WALE), wanaume walimshika pabaya, mwenyewe akaamuwa airudishe.
 
Kufa ni kufaana.

Wenzetu akina Rostam Azizi na timu yake nzima wanatumia utatuzi wa matatizo yetu ya umeme ya tangu tupate Uhuru kutatua matatizo yao binafsi.

Hata rais wetu juzi pale kwenye mkutano wa alishindwa kujibu swali jepesi kuhusu uwekezaji wa kampuni binafsi na hatua ambazo serikali inachukua kuimarisha sekta hiyo.

Nilimuonea huruma sana Rais mzima wa nchi mwenye Digirii ya Political Science/ Political economy kutoka UDSM akinasa kiurahisi sana kwenye nyavu za ujinga wa kuweka wazi mwelekeo wake.
Rais hajui nini ni cha muhimu kwanza ili kujenga na kuvutia sekta binafsi katika uwekezaji nchini Tanzania.
Jibu sahihi MH Rasi Jakaya Mrisho Kikwete lilikuwa.
1 Tumejiwekea lengo ndani ya miaka(... Unataja miaka..) la kuwa na uwezo wa kudumu wa kuzalisha nguvu za nishati za kutosheleza mahitaji ya wananchi wote wa Tanzania na wawekezaji wote watakao ingia

2 Tumetenga eneo la Ukanda wa Mtwara ili liwe eneo maalumu kwa wawekezaji wote kutoka nje na wa ndani, ili kuondoa msongamano wa wawekezaji hapa Dar, kuruhusu urahisi wa kila muwekezaji kuweza kukua na kupanua eneo lake na kurahisisha serikali kuratibu na kusimamia uwekezaji huo kirahisi na kuondoa ukiritimba wote usio wa lazima.

3 Kuhakikisha tuna zalisha maji safi ya kutosha na kujenga miundombinu ya kusafisha maji taka.

4 Kumarisha mawasiliano yote kwa ujumla, ya simu( landline na zile za mkononi) pia Internet ambayo ni muhimu sana katika karne hii ya 21. tayari tumeanza kuweka mkonga wwenye uwezo wa juu zaidi katika mawasiliano mkonga wa Fiber Optic.


Kma kiingereza hakipandi isingekupa shida hiyo, unapiga Kiswahili au hata Kikwele wakwele wenzio ambao kizungu na lugha nyingine zinapanda wangetafsiri.

IZI KABISA HANARABO PREZIDENTI, A I EMU STEEL WANDARING WATI WENTI RONG APUSTEAZI THE MOMENTI THE YANGI LEDI FINMISHIDI ASIKINGI YU E KWESHENI!!!??

WERE YU STANED BY HER BUTIFU DENTO GAP (MWANYA) hIIII HIII!!!! BIKOUZI I NOO YUA WIKINESI.

Akijuacho Rais wetu ni kitu kimoja, kwamba matatizo siku zote huleta mlo lakini pia anajua wazi kwamba ni ukengeufu mkubwa kutangaza hivyo hadharani.

Hayo majibu yako, tuwekee na alivyojibu JK ili turidhike na kauli zako otherwise tutaona kama una chuki za ''agenda za siri''.
 
Kwa kweli Vodacom connection bado inafanya kazi na tutaona, Makamu Mwenyekiti wa CCM (alikuwa Vodacom), Dk. Rashid (alikuwa Vodacom), Ngeleja (alikuwa Vodacom), Lowassa (Dealer mkubwa, Alphatel), Peter Noni (Vodacom/EPA), Rostam (Vodacom/Kagoda?/Dowans) sasa tunategemea nini? Watanzania WATALIA SANA.

Source: ThisDay

Kaka Halisi kama nawe umeshaingia katika huu mkumbo wa ku-personalise haya mapambano basi kweli tupo hatarini kushindwa vibaya katika haya mapambano...

omarilyas
 
Back
Top Bottom