katika hali ya kushangaza mkuu wa chuo cha saut mwanza ameachia cheo hicho baada ya kuona wanafunzi nane wamefukuzwa chuo bila utaratibu wowote,sababu nyingine ni kuwatoza wanafunzi penalty ya laki moja wachelewapo kulipa ada ameuliza hyo penalty inaenda wap na kwanini wanafunzi wapigwe penalty,source mimi mwenyewe lecturer naitwa slaa
mtoa mada siamini kama wewe ni lecturer wa SAUT kama unavyojiita mwenyewe eti SLAA, hiki chuo hakina mhadhiri mwenye jina hilo bali hapo zamani alikuwepo mhadhiri akiitwa EMMANUEL SILAA alimaliza mkataba wake wa kufundisha SAUT tangu August 2013 kwa sasa anafanya shughuli zake binafsi mkoani mwanza na kilimanjaro.
Acha kudanganya bwana,mtoa mada.. nani kakudanganya kama mkuu wa chuo cha SAUT amejiuzuru kwa sababu za kijinga kama hizo. Kwa akili zako zilivvyo fupi,wewe ungeweza kuwatetea watu waliokamatwa wanaibia mitihani na wamekiri au unaweza kuwatetea watu wanaopewa ada na kwenda kufanyia biashara halafu hawalipi kwa wakati huku miradi ya chuo kama ukumbi na bweni la wasichana imesimama. Think twice bwana,yule ni dokta na padri pia. Sasa nakufahamisha usioyajua. Makamu mkuu wa chuo kabla hajateuliwa alikuwa Principal wa Bukoba,na Maprincipal wote wa vyuo vya SAUT ni members waalikwa wa BOARD OF TRUSTEE na UNIVERSITY SENATE ambayo ndo hupendekeza hiyo PENALTY na BOARD OF TRUSTEE ambayo ndo chombo cha mwisho cha maamuzi ndo walioamua hao 8 wafukuzwe chuo akiwemo VC wenyewe ambaye pia ni mwenyekiti wa Discipline commette. Sasa atapingaje kitu mbacho alishiriki kukiamua. Uwe unauliza kabla ya kuleta mada, fualitia mchakato uliofanyika kumpata VC na watu walipendekezwa halafu wakakatiliwa akapita yeye,hao ndio sababu ya yeye kujiuzuru sasabu wapo nae mpaka sasa na hawampi ushirikiano wa kutosha..kama upo SAUT unaweza kuwa shuhuda wa kutosha khsu kusimama kwa mambo mengi hasa majengo na kuongezeka kwa madeni ya chuo..na alishajiuzuru toka January ila alikuwa anasubiri idhini ya tume ya maaskofu 4 iliyoundwa kufanya uchunguzi wa sbb alizotoa..