Mkuu wa Mkoa wa Geita awafukuza kikaoni Maafisa wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita

Mkuu wa Mkoa wa Geita awafukuza kikaoni Maafisa wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigella amewamuru Watendaji watatu ambao ni Wafanyakazi wa Kampuni ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML) kutoka nje ya ukumbi wa kikao cha Kamisheni Cha Mkoa (RCC).

Uamuzi wa Shigela unakuja kufuatia kutoridhishwa na majibu ya maofisa hao wa GGML juu ya malipo ya malimbikizo ya fedha za Uwajibikaji wa Makampuni kwa Jamii (CSR) mwaka 2024, Tsh. Bilioni tisa.

Shigella alisema fedha za CSR ni pesa ya wananchi na siyo pesa za mtumishi wa GGML na haitolewi kama hisani bali ipo kwa mjibu wa sheria na kanuni za madini na hivo GGML haipaswi kuleta mzaha katika utekelezaji wa CSR.

Mbunge wa Jimbo la Chato, Dk Medard Kalemani alipongeza uamuzi wa mkuu wa mkoa na kueleza kuwa kanuni ya 140 ya sheria za madini inatambua CSR inatekelezwa kwa mjibu wa sheria na siyo hisani.
 
Back
Top Bottom