Mkuu wa Mkoa wa Tabora ameagiza kushushwa vyeo kwa Walimu Wakuu wa shule ambazo zimekuwa zikifanya vibaya katika mitihani

Mkuu wa Mkoa wa Tabora ameagiza kushushwa vyeo kwa Walimu Wakuu wa shule ambazo zimekuwa zikifanya vibaya katika mitihani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
MKUU wa Mkoa wa Tabora, Dkt. Philemon Sengati, ameagiza kushushwa vyeo kwa walimu wakuu wa shule ambazo zimekuwa zikifanya vibaya katika matokeo ya mitihani.

Alitoa kauli wilayani Urambo wakati wa mkutano na viongozi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kwenye ziara ya kikazi.

Dkt. Sengai alisema walimu wakuu wasiokuwa wabunifu wa kuziwezesha shule zao kupandisha ufaulu wa wananfunzi ili waweze kuondokana na daraja sifuri, la nne na tatu hafai kuendelea na nafasi zao.

Alisema ni vema wakaondolewa na nafasi zao kukabidhiwa walimu ambao wako tayari kufanyakazi kwa kujituma na uzalendo ili waweze kuchochea ufaulu katika shule zao na mkoa kwa ujumla.

“Tunataka walimu wale ambao wako ‘committed’ na willingness na wanafanyakazi kwa uzalendo mkubwa, hao ndio tuendelee kuwafanya kuwa wakuu wa shule ili waendelee kuwa injini ya ufaulu wa shule zetu,” alisema.

Alisema walimu lazima wasaidie kusimamia maadili na kuwahimiza wanafunzi kusoma kwa ushirikiano na kuwawezesha kuongeza ufaulu ili wautangaze kwa kushika nafasi za juu.

Alisema moja ya kipaumbele cha uongozi wake ni elimu kwa kuwa ndio itasaidia kuwapaisha wakazi wa Mkoa wa Tabora kiuchumi na maendeleo mbalimbali.


IPPMedia
 
Labda waondoe sifuri wanaweza kufanikiwa

Kwa shule za serikali daraja la 3 na 4 ni mlima itatuchukua make miaka

Pia serikali iboreshe miundombinu na maslahi ya walimu nadhani hapo itachangia kuboost kutokomeza zero na ufaulu mwingne usiofaa
 
Labda waondoe sifuri wanaweza kufanikiwa

Kwa shule za serikali daraja la 3 na 4 ni mlima itatuchukua make miaka

Pia serikali iboreshe miundombinu na maslahi ya walimu nadhani hapo itachangia kuboost kutokomeza zero na ufaulu mwingne usiofaa
Kwa ngaz ya advance hilo linawezekana, ila jitihada kubwa za waalim ndio znahtajka
 
MKUU wa Mkoa wa Tabora, Dkt. Philemon Sengati, ameagiza kushushwa vyeo kwa walimu wakuu wa shule ambazo zimekuwa zikifanya vibaya katika matokeo ya mitihani.

Alitoa kauli wilayani Urambo wakati wa mkutano na viongozi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kwenye ziara ya kikazi.

Dkt. Sengai alisema walimu wakuu wasiokuwa wabunifu wa kuziwezesha shule zao kupandisha ufaulu wa wananfunzi ili waweze kuondokana na daraja sifuri, la nne na tatu hafai kuendelea na nafasi zao.

Alisema ni vema wakaondolewa na nafasi zao kukabidhiwa walimu ambao wako tayari kufanyakazi kwa kujituma na uzalendo ili waweze kuchochea ufaulu katika shule zao na mkoa kwa ujumla.

“Tunataka walimu wale ambao wako ‘committed’ na willingness na wanafanyakazi kwa uzalendo mkubwa, hao ndio tuendelee kuwafanya kuwa wakuu wa shule ili waendelee kuwa injini ya ufaulu wa shule zetu,” alisema.

Alisema walimu lazima wasaidie kusimamia maadili na kuwahimiza wanafunzi kusoma kwa ushirikiano na kuwawezesha kuongeza ufaulu ili wautangaze kwa kushika nafasi za juu.

Alisema moja ya kipaumbele cha uongozi wake ni elimu kwa kuwa ndio itasaidia kuwapaisha wakazi wa Mkoa wa Tabora kiuchumi na maendeleo mbalimbali.


IPPMedia
Hizo shule na walimu wana wezeshwa? Au ndio kumfunga ng'ombe kwenye kisiki kutwa bila maji na kesho utegemee kupata Lita 10 za maziwa? Miondombinu mibovu, watoto madawati hakuna, shule vijijini walimu wachache, watoto wanasoma wakipiga miayo njaa, na mapungufu mengi mengine. Elimu bure zawadi ni poor performance.
 
Yenye anafikiri utoaji wa elimu una factor moja tu ya mwalimu. Huyu ni daktari wa falsafa?
 
Kwani tatizo ni walimu au wanafunzi ndio hawaelewi?
Na yeye amejuaje walimu ndio chanzo cha kufanya vibaya?

What the hell is this?
 
Ndiyo maana Msukuma na Kishimba huwa wanajivunia kutokupoteza muda wao kwenda shule.
 
suala la elimu linahitaji mikakati na pia kuwe na ushirikiano kati ya walimu, wazazi wadau wa elimu na wanafunzi, Matokeo mazuri mashuleni yanahitaji muda, mazingira mazuri kwa wanafunzi na walimu, ushirikishwaji kwa wote, na motisha
 
Back
Top Bottom