Tetesi: Mkuu wa Wilaya Mpya wa Kisarawe ni "Mtoto" wa Rais Magufuli

Tetesi: Mkuu wa Wilaya Mpya wa Kisarawe ni "Mtoto" wa Rais Magufuli

"conflict of interest" kibongobongo tunachukilia poa tu, hata kwenye tenders ni hivihivi tena serikali ikaamua kufwatilia watafungwa wengi sana kuhusu hili swala...ilaaa ndi hivo unatakiwa utulie tuliii ukileta nyenyenyeee..tunakufunga mpaka tukusahau
 
Kuna tatizo nimeligundua hapa,watu wamecomment pasi na kujua mantiki ya mleta mada ni ipi . Hii naifananisha na pale unapomuuliza mtu eti Tanzania ilipata uhuru mwaka gani,nae bila kujua mantiki ya swali akajibu 1961. Wakati kumbe Tanzania imekuwa Tanzania mwaka 1964 baada ya nchi mbili huru Tanganyika na Zanzibar kujiunga. Sasa nikirudi kwenye mada lazima tujue mleta hoja alilenga nini. Hoja hapa sio ya kichama,ni ya kitaifa,kila chama kina muongozo wake na hakina direct effect kwa taifa. Chama kina miongozo katika kupata viongozi na mara nyingi hutumia kura km njia ya kujipatia viongozi wao. Hvy kuwa na ndugu wa moja kwenye uongozi wa chama kimoja sio kosa la chama,kura imeamua,na hakuna direct cost kwa taifa. Ukija kiserikali,kuna nafasi za kugombea na kuteuliwa. Unapogombea ukachaguliwa na ukavurunda waliokuchagua itawa cost,ila unapoteuliwa na kuvurunda wakulaumiwa ni aliyekuteua. Mantiki ya mleta hoja ni je,ikiwa aliyeteuliwa ni mtoto wa kufikia wa aliyemteua,,ikifikia wakati wa kuwajibishana atamuwajibisha? Kuwa mtoto wa kufikia si sababu ya kupimia upendo wa kifamilia. Zipo familia nyingi wanathamini zaidi watoto wa kufikia kuliko wa kuwazaa . Sàsa je kama huyu nae ni kipenzi cha aliyemteua,atakapovurunda atawajibishwa? Hapa tunaangalia mustakabali wa nchi sio chama. Tusijenge hoja kwa mizuka ya kichama,tuwe wazalendo linapokuja suala la kitaifa. Vyama vipo na mtu unaweza kuhama muda wowote ila sio uraia/utaifa.Nimemaliza
 
Huu uzi baada ya miezi kadhaa kuna watu watajishangaa jinsi walivyokuwa na akili kijiko , tuvute muda.
 
CC: RC wa Pwani, W- TAMISEMI n.k uzi huu unaweza kuwasaidia kwenye utendaji wenu
 
Mara baada ya uteuzi wa wakuu wa Wilaya uliofanyika na kutangzwa leo, jamii imeanza kuwachambua na kujuwa historia zao na ushiriki wao katika kumasaidia kazi Mh Rais.

Wananchi wamekuwa na shauku ya kumfahamu na kuelewa historia ya Mkuu wao mpya wa Wilaya Mh. Happynes Senenda William. Kabla ya kuwa DC wa Kisarawe tunaambiwa dada huyu alikuwa Manager wa HR wa TANROADS Mkoa wa Tanga, ni mdada mdogo mwenye elimu ya Masters. Mwaka 2010 aligombea ubunge viti maalumu kupitia mkoa wa Geita lakini hakufanikiwa, mwaka 2015 alipumzika ili kuzunguka na baba kumtafutia kura

Habari zinazidi kupenyeza kuwa Mh.Happyness William ni mtoto wa kulelewa na Rais JPM, amesomeshwa na Rais na amekuwa akiishi na JPM kwa maisha yake mpaka alipopata kazi. Kifupi Mh.Happyness ni "mtoto" wa JPM na kwa sasa ni DC wa Kisarawe

Ama hakika huu ni msimu wa vijana...Vijana mjiibidishe ili muonekane na mpate Wilaya au Mkoa.
Lissu: Serikali hii ni ya hovyo
 
Usigeuze JF kuwa chungu cha majungu! Ongelea uwezo wake, sio uhusiano wake...ungejisikiaje kama ungekuwa wewe unaomba kazi sehemu afu unanyimwa simply because wewe una undugu na rais...tuletee CV na track record ya performance sio mijungu
Punguza povu, kwenye ukweli uongo hujitenga. Huwezi kukwepa mgongano wa kimaslahi hapo.
 
Mkuu wa wilaya anaweza akateuliwa mtu yeyote sidhani kama kuna sifa zilizoainishwa kuwa anapaswa kuwa nazo mtu anayeuliwa kuwa DC.
 
Isitoshe sio baba yake wa kumzaa shida iko wapi hapo?. Tatizo tunalolikataa wananchi ni kubeba mtu asiyebebeka...huyo dada anayo elimu nzuri tu...
elimu na utendaji kazi ni vitu viwili tofauti kaka
 
kwani we ukiwa na mwanao ambae anaweza kupiga mzigo hata sehemu nyeti huwez kumweka eti kwa kua watu watakusema vibaya???
wazungu wanasema '' charity begginz at home''
homme cwt hoome
 
Kweli tuna ishiwa hoja sasa.
Yaani mnataka nguvu wote Viongozi waka chunga Ng'ombe.
Mtoto ni mtoto hata kama wa Rais ni haki yake kupata ajira ili mradi anastahiki
 
Back
Top Bottom