DOKEZO Mkuu wa wilaya mstaafu anaambiwa ajiongeze ili apewe mafao yake aliyofuatilia kwa miaka kumi sasa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mkuu alianza U DC tangu enzi za chama kimoja ,hadi Miaka ya tisini.
Hakuwahi kulipwa kwa utaratibu huo unaousema na baada ya hapo alirudi wizara ya Maendeleo ya Jamii Kama umenisoma,so haiko hivyo unavosema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwache ateseke
Tanzania bado tuna safari ndefu sana kama mkuu wa wilaya mstaafu hajui hata haki zake , yaani mtu ambaye amekuwa kiongozi wa ulinzi na usalama kwa miaka 16 katika wilaya usika tuanze kumtetea je walimu na manesi itakuwajeView attachment 1061975

In God we trust
 
Alishawatumikia basi hawana haja naye tena hao ndio chama cha kijani , dhulma ,wizi na ufisadi ndio kazi zao .
 
Upo sahihi pensheni zao zipo kwenye political leaders pension scheme wao hulipwa kila baada ya miaka mitano kama wanavyolipwa wabunge labda atuambie ni lini mzee wake aliacha kuwa Mkuu wa wilaya kama ni kabla ya wakuu hawa kuingizwa kwenye political leaders pension scheme hapo HAZINA wanahusika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni Hazina Mkuu,ilikua kabla na baada ya hapa alihamishiwa wizara ya Maendeleo ya Jamii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alisaidia kuzuia mikutano mingapi ya hadhara au kuwaweka raia wangapi ndani masaa 48 wakati wa utendaji wake!?
Tuanzie hapo
Watu wa ccm mmetesa sana watu, malipo ni hapahapa duniani.

Tena huyo inaonekana alikuwa mnoko hadi kwa mashetani wenzake wa ccm na sasa wanamsomesha namba. Sina huruma na majitu ya ccm.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani mafao ya wastaafu wa vyeo vya kisiasa yako vipi?sio kwamba wanalamba lumpsum wanatambaa mbele?
 
Kikubwa muulize hakuonea watu wakati wa uongozi wake?
Hakuchukua vya watu wakati wa uongozi wake?
Maana kuna kitu kinaitwa laana kwasisi tunaoamini.
Kama alifanya hayo mwambie atubu kwa muumba wake,yeye ndio alioshika funguo za haki na stahiki zake.
Kuna eneo mzee wako alifanya ndivyo sivyo
Trust me!
 
Mimi kuna mmoja nilimsaidia. Alikuwa hajastaafu lakini akaumwa sana. Akaanza kuomba ruhusa kwenda matibabu India. Alikalishwa benchi utumishi, Afya, Tamisemi kwa miezi 3 ruhusa na fedha havitoki. Nikamhurumia na kuingilia kwa kutumia vijana hao wa Tugawane (Lakini mimi hatukugawana). Ruhusa ikatoka in two days. Akiwa njiani kwenda airport akafariki, tukazika.

Weee waone hawa wote wanaofoka foka na kutia ndani sasa hivi, lakini muda wao ukiisha, utawahurumia. Ukiwaona akina Hapi hawa utadhani watabaki ni vijana! Waambie wamtembelee Mzee Timothy Apiyo kama wanamfahamu! Alikuwa KM Kiongozi Ikulu. Aliogopesha kwa uadilifu kuliko Mwalimu mwenyewe. Sijui kama JPM anajua aliko au alifia wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…