Mkuu wa Wilaya Unguja avamia shuleni kusaka simu na shisha kwa wanafunzi

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Your browser is not able to display this video.

Mkuu wa Wilaya ya Mjini Unguja, Zanzibar, Rashid Simai Msaraka amefanya ziara ya kushtukiza katika Shule ya Sekondari ya Forodhani kwa lengo la kufanya msako wa Wanafunzi wanaotumia shisha zinazotumia umeme pamoja na simu.

DC huyo amefika Shuleni na kuamuru Wanafunzi wote washushwe parade na kusachiwa mmojammoja ambapo mabegi yao yaliyoachwa madarasani nayo yalisachiwa ndipo alipokutana na shisha ya umeme moja na simu.

Amesema huenda ziara yake ya kushtukiza ilishtukiwa kabla kwani katika baadhi ya Shule alizopita alifanikiwa kukamata simu na shisha zaidi ya moja.

DC Simai ametoa onyo kwa Wanafunzi kutokwenda Shuleni na shisha, simu, spika za bluetooth, manukato na kucha za rangi pamoja na vikuku.

Pia soma:

Zanzibar kupiga marufuku shisha na sigara za kielektroniki

Marufuku nyingine Zanzibar soma:

Yanayoendelea Zanzibar tusubiri majibu ya Wahanga na kuzaa gharika
 
Enzi zetu Tanzani ilikuwa na mikoa 25 Bara 23 na Visiwani Pemba na Unguja ikiwa mikoa pia. Ghafla imekuwa kiinchi na vijiwilaya vyake.
Daahh..kumaliza pesa tu !!!na gharama Kwa wananchi
 
Mkuu wa wilaya tena.

Mkuu wa shule na walimu wenzake wanafanya kazi gani hapo shule, afisa elimu wilaya, afisa elimu wa mkoa nk.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…