Mkuu wa wilaya ya Temeke aamlisha watakavaa nusu uchi wachapwe viboko hadharani

na mpa sapoti huyu kaona mengi, wengi wamevamia nguo za ndani na kuzifanya za nje, wengine za wadogo wao ili mradi tu wafoji kuonyesha sehemu zao za mwili.
 
Hii imeka vizuri.ila ingekuwa ni tamko la nchi nzima pia napendeza wote watakao kamatwa wapewe adhabu ya katika jamii.mf kufanya usafi hospitali.barabarani.mashulen.sokon.nk.namin ndio adhabu sahih ila sio viboko.mana maeneo meng ni machafu
yanahitaji watu wa kuyasafisha
 
hii kali. . . wapo wanaopinga na wapo wanakubali. . .
ukweli cjawahi kuona sheria hii ikitumika zaidi ya nchi zenye misimamo na itikadi za dini.
wakuu hawa wa wilaya/ mikoa wazingatie sheria za msingi zilizopo ndipo watoe maagizo au matamko yao.
mengine ni sumu
 
Samahani naomba kuuliza hii inawahusu na waigizaji na wasanii wa bongo fleva au??????
 


safi sana...! hatua na maamuzi ya busara aliyofanya bi sophia
 
mavazi ya kiafrica ni kuziba sehemu za siri tu,mbona siku hizi wanavaa nguo ndefu
 
hawa wakuu wa wilaya sijui wako vipi. mnamkumbuka yule aliyewachapa walimu viboko kule mkoa wa kagera?
 
sikubaliani na baadhi ya mavazi ila pia sijui kama hiyo adhabu ya kuchapa mtu viboko ipo kisheria.
halafu kubwa ni elimu itolewe ndani ya jamii hao wavaa nusu uchi wanakotokea.....................
pia inaonekana hawa wavaa nusu uchi wamevamia maslahi ya bi sofi maana amezaliwa tz na kila siku anayaona ila leo yamemkuta imebidi atumie ukubwa wake - pole mamito
 
Maadili ya Mtanzania ni yapi? Labda tuanzie hapo kwanza.
Kweli hata mimi huwa natatizika. Maadili ya mtanzania ni yapi? Kwa mfano kuna mambo ya ufisadi, polisi kuua raia bila hatia, rushwa, CCM na nyimbo zao za ukabila, udini, ukanda na vyeo kwa kujuana au kifamilia, kutorosha wanyama nje, kuwafurusha wananchi kutoka maeneo yao ya asili kisa wanyama watamalaki. Wakubwa kusema uongo. Mtu atokee atuorodheshee maadili ya mtanzania tuyajue. Mimi naona huu ni wimbo usio na kibwagizo kama ule wa kusaka vazi la taifa! alipoondoka Nyerere na baada ya waliomfuatia kuliua azimio la Arusha ndio ukawa mwisho wa hayo maadili ambayo Nyerere alisimamia. Sasa hivi ni utandawazi na uwekezaj maadili yatasimama wapi?!
 
Kuna mwandishi mmoja ameandika kitabu chake akakipa kichwa cha habari "Rulers of the law against rule of the law" u
kimsingi mwandishi anaongelea watu wa sampuli hii ya mheshmiwa wa wilaya ambao kwa utashi wanafikiri juu ya sheria na siyo kwa kufuata sheria, binafsi pia sipendezwi na mavazi ya vi-sister duu na vi- brotherman na wale wa kata k lakini nadhani ili kuwe na mizania sahihi ni vyema sheria itamke kipimo cha kutofautisha mavazi ya kimaadili na yale yasiyo ya kimaadili, lakini kubwa zaidi ni kupata watu safi watakao weza kusimamia sheria hiyo isiwe kama wanvyofanya polisi wao wanaendesha magari mabovuu kabisa tena yanatoa moshi balaaa lakini wakiona gari ya mwananchi wa kawaida wanaikamata na kutoa makosa kibao. maana yake ni kua makatazo ya mavazi hasi hayawezi kufanikiwa kama hakuna mfano wa mavazi sahihi na watu kama hawajui faida na hasara ya kuvaa nusu uchi wanakua kama wenda wazimu. angalia mfano uko kwenye daladala umebahatika kupata siti wengine wamekosa hivyo wamesimama mko kwenye foleni jua la dar linawaka kama kawaida yake joto kibao , asa mdada au mkaka aliyesimama karibu yako amevaa nguo inayoacha makwapa yake wazi , kwa sababu ya joto kwapa inatoa maji na maji yale yana kunakudondokea utajihisije ? nimeuliza hivi maana wengi wakigusia mavazi yasiyofaa watu wanakimbilia kufikiria matamanio ya sex , binafsi nafikiri kuna sababu ya watu kujirejesha kwenye mavazi yenye staha.
 
Ukiona hivi ujue huyo mama yenu bi sofia kazi ishamshinda! Kero zimejaa lukuki katika wilaya yake, lakini kwake mavazi ndio priority??? Awaache watoto wa wanawake wenzie, anadhani Tza ni kiislam, atangoja sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…