Mkuu, hao wana rekodi kumzidi wa kwetu.Maandalizi sio tu timu ya Taifa ila kuanzia penye vilabu vyetu je tunao hao wachezaji? Kocha wa taifa anakaa nao wiki mbili je huko vilabuni tunawalea vipi wachezaji wetu? Kuna hawa wawili mungu awa rehemu stiven kashi na shaibu amadou wa nigeria mbona walikuwa na rekodi nzuri tu.
Dhana ya uzawa tukiiendekeza hatufiki popote.Tumeshakuwa na makocha wageni wengi tu na hakuna sehemu nzuri tunayoweza kujivunia kuwa wametufikisha, mkwasa anaweza kuwa chaguzi sahihi tumpeni muda tu, kwanza ata record yake ninzuri ata ukifanya comparison na makocha waliopita, apewe muda kwanza nyie wenyewe mnajua wabongo walivyo wagumu kuelewa so tuwaachie huyu huyu mzawa anajua hadi kimakonde
Ni kweli ila walianzaje? ni kwamba lazima kwanza tuwe na wachezaji wa kimataifa au nusu ya hapo sidhani kama duniani kuna nchi ilifanikiwa bila kuwa na wachezaji wenye kiwango fulani hapo ndipo pa kuanzia. Ukisema dhana ya uzawa inatudondosha leo chagua world class kocha mpe timu yetu kama hatutamtimua.Mkuu, hao wana rekodi kumzidi wa kwetu.
Huu ndio uchawi, ufitini na ujuha.... Kuna forward wa Yanga aliyecheza timu ya Taifa au hata kuitwa tu kipindi cha ukocha wa mkwassa!!???Anajaza mafowadi wa Yanga ambao husugua benchi kila siku. Namba zao wanazo ma pro. Hii ni hujuma kwa Taifa.