Mlimani city waanza kubagua watanzania?

Mlimani city waanza kubagua watanzania?

Mama Lao

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2007
Posts
238
Reaction score
11
Hayawi hayawi yamekuwa..........yale yaliyokuwa yakisemwa na Kina Mar. Prof Seth Chachage sasa yanaanza kujionyesha.
Wageni wanaanza kuleta "ubaguzi wa kimatabaka" kwa watanzania.
Jana nilishangaa pale mlinzi wa Mlimani City alipomwambia dereva wa bajaj kwa "Uongozi wa Mlimani City hauruhusu Bajaj kuingia ndani ya eneo la Mlimani City". Maskini dereva asiyejua hili wala lile akwaomba samahani wateja na kuwashusha getini.
Uongozi wa Mlimani City una uwezo gani wakubagua....wanaoendesha bajaj wasiingie ndani ya eneo hilo. Je hawa nao sio watanzania wanaojitafutia riziki na isitoshe bajaj nyingi huingia pale kuleta wateja na kutoka nje.

Naona makaburu sasa wana "export" ile racism yao.
Nilifanikiwa kuongea na dereva mmoja wa bajaj naye akakiri hata wao wanashangaa juu ya uamuzi huu.

Mimi napendekeza iwapo hili litaendelea watanzania tuache kwenda Mlimani City.
Haina maana kwamba anayeingia na saloon car ndiye mwenye uwezo au anayeingia na bajaj ndio hana uwezo. Watanzania tuna uwezo wa kwenda sehemu yoyote mahali popote na kamwe hatujawahi kuwa graded kwa vyombo vya usafiri tunavyovitumia.
Kama kuna tatizo limetokea muhimu hapa ni kuwawekea wenye vyombo vya bajaj utaratibu wa kuingia na kutoka kwenye eneo hilo na sio "kuwazuia kuingia"
 
wewe mama kila sehemu kuna utaratibu wake na sheria zake walioweka utaratibu huo wana maana zao kwahiyo ungejaribu kuuliza basi kwanini wamepitisha sheria hiyo ya bajaj si unajua kwamba bajaj nyingi zinatumia petroli ? kulipuka ni kawaida au sio ? halafu kale ni kagari kadogo gaidi anaweza kuingia nacho mall
 
wewe mama kila sehemu kuna utaratibu wake na sheria zake walioweka utaratibu huo wana maana zao kwahiyo ungejaribu kuuliza basi kwanini wamepitisha sheria hiyo ya bajaj si unajua kwamba bajaj nyingi zinatumia petroli ? kulipuka ni kawaida au sio ? halafu kale ni kagari kadogo gaidi anaweza kuingia nacho mall
Shy mind your language kajifunze ku address watu properly....not starting with "wewe".

Inawezekana hiyo ni opinion yako.
Huu ni ubaguzi. Bajaj zilikuwa zina "drop" watu na kuondoka na parking za bajaj ziko nje ya eneo la Mlimani City.
Kwa hiyo gaidi hawezi kupakia "benzi"?????? Nipe mfano wa wapi Bajaj ilipolipuka???
Sasa utasikia ....hakuna kuingia na ndala....inaelekea Shy ubaguzi hujui unavyoanza.....sasa endelea kushangilia makaburu!
 
Mama Lao, Nadhani unachokiongea hapa kina mantiki.

Lakini kwa maoni yangu..umeendeleza ule ule mtindo wetu watanzania kuona kitu na kulalamika baadaye. wewe ulivyoona dereva wa Bajaji anaambiwa arudie getini, ulichukua hatua gani? kwa vigezo vyangu..mi sikujui lakini kama una uwezo wa kubonyeza keyboard..basi wewe ni middle class au zaidi kwa hiyo hata uelewa wako ni mpana.

Yes, from your story, alichofanyiwa mwenye Bajaji si sawa, lakini hata wewe ulichofanya si sawa. Kwenda kuongea na dereva wa Bajaji kweli ulitegemea nini? Kwanini hukwenda kuwaona wausika moja kwa moja?

Kwa maoni yangu: Ungeenda moja kwa moja ukaomba kumuona meneja wa Mlimani city na kumuuliza kama kuna sheria/utaratibu huo ambao umewekwa na wao. Au ni walinzi waliamua kuweka utaratibu wao. Iam sure huyo meneja angekupa jibu sahihi na wewe baada ya hapo ndo ungefanya conclusion kuwa either kuna ubaguzi au vipi.

So next time ukiona tatizo kama hilo..siyo kuja JF na kumwaga "the dataz za ubaguzi wa makaburu". Do something siyo kulalamika tuu. Huwezi jua hata huyo meneja wa Mlimani City anaweza kuwa hajui walinzi kama wanawanyanyasa watu wa bajaji... Kwa kufanya hivyo, ungekuwa umewasaidia madereva na perhaps yule boss angeona kwamba kuna watu waelewa kwenye nchi yetu ambao wanafuatilia mambo. Na indirectly, ungekuwa umesaidia wengi dhidi ya manyanyaso ya walinzi..

Jamani changes ni initiave zetu wenyewe...Tusipende kulaumu tuu kwa yale ambayo we can influence changes.

Mada yako hapo juu, inaweza kuwa na ukweli, lakini ukiangalia..ni ule ule mwendelezo wa watanzania wa "kupenda kulaumu"

NEXT TIME, DO SOMETHING!

Masanja,
 
Kwani nissan patrol nayo si inatumia petroli, tena nyingi kuliko bajaj?
 
wewe mama kila sehemu kuna utaratibu wake na sheria zake walioweka utaratibu huo wana maana zao kwahiyo ungejaribu kuuliza basi kwanini wamepitisha sheria hiyo ya bajaj si unajua kwamba bajaj nyingi zinatumia petroli ? kulipuka ni kawaida au sio ? halafu kale ni kagari kadogo gaidi anaweza kuingia nacho mall

Si lazima uwe unachangia kila hoja....kaa kimya wakati mwingine ufiche aibu yako...crap
 
Ush...usijali ilikuwa usiku kwa hiyo sikuweza kupata maelezo.
Dereva wa bajaj wa kituo cha Mlimani city aliniahidi kwamba leo atafanya initiative ya kwenda kwenye vyombo vya habari na mimi nikaahidi kucreate awareness through JF.
Of course kitakachofuata utakiona...huu ni mwanzo ....Ijumaa njema
 
Kuna sababu nyingi tu,mi nadhani hata kama Mlimani City ingekuwa inamilikiwa na Mtanzania angeweza kusema hivohivo.Maamuzi mengine yamekaa kibiashara zaidi kuliko tunavyoweza kuona.Labda vile vibajaj vilileta kero mule ndani,au labda kiligonga mtu,maana nao uendeshaji wao sometimes ni hatari.
 
A good point Masanja....
But on the other hand Mama Lao has done her(his) homework..
Hajaangalia tatizo kwa mtazamo wako, lakini ametupa mwanga kwamba kuna kitu kama hicho kinatokea.....basi yawezekana akaenda mwingine kupata maelezo zaidi. Didn't they say identified known is half solved? So Mama Lao has done half the job?
Au labda Mama Lao pia anaweza kwenda kuuliza zaidi?
 
Kuna sababu nyingi tu,mi nadhani hata kama Mlimani City ingekuwa inamilikiwa na Mtanzania angeweza kusema hivohivo.Maamuzi mengine yamekaa kibiashara zaidi kuliko tunavyoweza kuona.Labda vile vibajaj vilileta kero mule ndani,au labda kiligonga mtu,maana nao uendeshaji wao sometimes ni hatari.

Mkuu, sababu unazozitoa ndizo zinazofanya huu uonekane kuwa ni ubaguzi. Kuna haja gani ya kuwatenga watu namna hii? nadhani sehemu public kama ile inatakiwa iwe riksa kwa kila anayeweza kwenda kwa njia yoyote ile, hata mtembea kwa miguu
 
Mkuu, sababu unazozitoa ndizo zinazofanya huu uonekane kuwa ni ubaguzi. Kuna haja gani ya kuwatenga watu namna hii? nadhani sehemu public kama ile inatakiwa iwe riksa kwa kila anayeweza kwenda kwa njia yoyote ile, hata mtembea kwa miguu

Kama kumbukumbu zangu zitakua sahihi then nilishawahi kuona kibao kianchokataza baiskeli (labda na pikipiki) maeneo yale, nitajaribu kuangalia nikifika maeneo yale.
 
Hayawi hayawi yamekuwa..........yale yaliyokuwa yakisemwa na Kina Mar. Prof Seth Chachage sasa yanaanza kujionyesha.
Wageni wanaanza kuleta "ubaguzi wa kimatabaka" kwa watanzania.
Jana nilishangaa pale mlinzi wa Mlimani City alipomwambia dereva wa bajaj kwa "Uongozi wa Mlimani City hauruhusu Bajaj kuingia ndani ya eneo la Mlimani City". Maskini dereva asiyejua hili wala lile akwaomba samahani wateja na kuwashusha getini.
Uongozi wa Mlimani City una uwezo gani wakubagua....wanaoendesha bajaj wasiingie ndani ya eneo hilo. Je hawa nao sio watanzania wanaojitafutia riziki na isitoshe bajaj nyingi huingia pale kuleta wateja na kutoka nje.

Naona makaburu sasa wana "export" ile racism yao.
Nilifanikiwa kuongea na dereva mmoja wa bajaj naye akakiri hata wao wanashangaa juu ya uamuzi huu.

Mimi napendekeza iwapo hili litaendelea watanzania tuache kwenda Mlimani City.
Haina maana kwamba anayeingia na saloon car ndiye mwenye uwezo au anayeingia na bajaj ndio hana uwezo. Watanzania tuna uwezo wa kwenda sehemu yoyote mahali popote na kamwe hatujawahi kuwa graded kwa vyombo vya usafiri tunavyovitumia.
Kama kuna tatizo limetokea muhimu hapa ni kuwawekea wenye vyombo vya bajaj utaratibu wa kuingia na kutoka kwenye eneo hilo na sio "kuwazuia kuingia"


Kabla hatujasema ni ubaguzi mimi naomba zitafutwe sababu zilizofanya bajaj kukataliwa!! Inawezekana kukawa na reasons nzuri tu.....
 
Nina ka-personal theory kwamba walinzi wana kaji-inferiority complex saa nyingine they take it out on the wrong people. Mimi binafsi, nakwaruzanaga sana na walinzi. Kuna supermarket kila nikiingia lazma kuna jambo. Kwenye training zao wanahitaji na customer care kidogo
 
Kwa kweli hapa naona inawezekana ikawa ni swala la ubaguzi ama ni swala la njaa. nionavyo mimi askari wengi huwa wanalipwa mshiko kidogo na hivyo basi wameamua kukabana na waendesha Bajaj ukizingatia nyingi zipo kibiashara. Wanadhani kwa kufanya hivi basi next time mwenye kibajaji akipita atamwachia 100/= japo apate maji.

Japo sikumbuki vizuri ramani halisi ya mlimani city, Ila nadhani niliona kama kuna specific location kwa ajili ya watu wenye pikipiki. Na kama hii sehemu ipo inamaanisha kwamba bajaj hazijapigwa stop ila wajasiriamali wapo kazini.

Uchunguzi zaidi ufanyike kawaida walinzi huwa wana unoko fulani just kujijengea heshima kumbe wanaharibu zaidi
 
Kama kumbukumbu zangu zitakua sahihi then nilishawahi kuona kibao kianchokataza baiskeli (labda na pikipiki) maeneo yale, nitajaribu kuangalia nikifika maeneo yale.[/QUOTE]

Mimi sijawahi kuona hicho kibao na nimekuwa nikienda mara nyingi hapo. Ni vema, kama wameamua kupiga marufuku usafiri wa aina fulani wakatangaza wazi wazi ili kila mtu afahamu kwa sababu ni utaratibu wa kawaida kwa mtu kujipangia naowataka katika eneo lake.
Lakini hata hivyo,. bado nahoji, kwa nini kuwabagua watanzania kiasi hiki?
 
wewe mama kila sehemu kuna utaratibu wake na sheria zake walioweka utaratibu huo wana maana zao kwahiyo ungejaribu kuuliza basi kwanini wamepitisha sheria hiyo ya bajaj si unajua kwamba bajaj nyingi zinatumia petroli ? Kulipuka ni kawaida au sio ? Halafu kale ni kagari kadogo gaidi anaweza kuingia nacho mall

this is pure bull shit
 
Hata kwenye mabaa yetu ya mtaani wanawazuia machinga sembuse vibatavuzi kuzuiwa
 
Hayawi hayawi yamekuwa..........yale yaliyokuwa yakisemwa na Kina Mar. Prof Seth Chachage sasa yanaanza kujionyesha.
Wageni wanaanza kuleta "ubaguzi wa kimatabaka" kwa watanzania.
Jana nilishangaa pale mlinzi wa Mlimani City alipomwambia dereva wa bajaj kwa "Uongozi wa Mlimani City hauruhusu Bajaj kuingia ndani ya eneo la Mlimani City". Maskini dereva asiyejua hili wala lile akwaomba samahani wateja na kuwashusha getini.
Uongozi wa Mlimani City una uwezo gani wakubagua....wanaoendesha bajaj wasiingie ndani ya eneo hilo. Je hawa nao sio watanzania wanaojitafutia riziki na isitoshe bajaj nyingi huingia pale kuleta wateja na kutoka nje.

Naona makaburu sasa wana "export" ile racism yao.
Nilifanikiwa kuongea na dereva mmoja wa bajaj naye akakiri hata wao wanashangaa juu ya uamuzi huu.

Mimi napendekeza iwapo hili litaendelea watanzania tuache kwenda Mlimani City.
Haina maana kwamba anayeingia na saloon car ndiye mwenye uwezo au anayeingia na bajaj ndio hana uwezo. Watanzania tuna uwezo wa kwenda sehemu yoyote mahali popote na kamwe hatujawahi kuwa graded kwa vyombo vya usafiri tunavyovitumia.
Kama kuna tatizo limetokea muhimu hapa ni kuwawekea wenye vyombo vya bajaj utaratibu wa kuingia na kutoka kwenye eneo hilo na sio "kuwazuia kuingia"

Makaburu ni ma racist wakubwa ila naomba niulize Mlimani City ni ya makaburu?Na je Mlimani City siyo kitega uchumi cha Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ambacho ni mwekezaji Mwarabu anamiliki?
 
Back
Top Bottom