kuprove kitu gani...kwahiyo unataka kusema Messi sio bora kwasababu kacheza ligi moja....kwahiyo suarez..etoo..ibrahimovic na lukaku ni bora kuliko Messi.......unachekesha mzee.
Messi popote anaweza kucheza tena kikosi cha kwanza dakika zote...Mmeanza kuhamisha magoli..mlitaka ahame sasa kahama mnataka kuleta hoja mufu zingine...Timu ya taifa kashawazodoa mnabaki na hoja ambazo sio za kimichezo.
kwahiyo kwa maoni yako, unataka mchezaji ili awe bora acheze ligi ipi na ipi?
Mmebaki kusemal igi ya spain rahisi..mbona henry na hazard imewashinda?...Hebu kati ya timu za england na spain zipi zimebeba mara nyingi makombe ya ulaya (UEFA NA EUROPA) Kuanzia 2008 - 2021?......kama ligi ya england ni ngumu, kwanini haijatoa mchezaji bora wa dunia kwa miaka 10 iliyopita?
Acheni chuki binafsi....angeenda Man city bado mngesema kaenda timu yenye wachezaji bora...Ongea kama shabiki wa soka usiongee kama mshangiliaji wa soka.
Top six ya epl ni city, united, liverpool, chelsea, spurs na arsenal (nimewaweka tu kutokana na brand yao)......Hebu niambie nani kati ya hawa hajakutana na shuruba za Messi?
sasa hao akina villa, leicester, everton na wengine ndio wangemuweza...Fikiria upya mkuu.