Mliokuwa mnahoji kuhusu Tigo kubadilisha jina, Mwigulu amewajibu "Kubadilisha majina ya makampuni hakuathiri mchakato wa kodi"

Mliokuwa mnahoji kuhusu Tigo kubadilisha jina, Mwigulu amewajibu "Kubadilisha majina ya makampuni hakuathiri mchakato wa kodi"

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Hapa juzi juzi tuliona Tigo imebadilisha jina kuwa Yas na kukawa na tetesi kuwa wanakwepa kodi.

Akijibu swali bungeni kuhusu makampuni yanayobadilisha majina ili kukwepa kodi Mwigulu amesema

"Kupitia sheria ya usimamizi wa kodi ya 238, serikali imeweka sharti kwamba mamalaka ya mapato Tanzania itahakikisha namba ya utambulisho wa kodi yaani TIN inabaki ile ile hata kama kampuni imebadilisha jina. TIN inatumika kufatilia historia yote ya ulipaji wa kodi wa kampuni hivyo mabadiliko ya jina hayaondoi wajibu wa kodi"


 
Sasa kwanini baadhi ya makampuni kirahisi kabisa, bila sababu za msingi yakimbilie kubadili majina wakati sote tunajua kibiashara ni hatari na hasara?
 
Wakuu,

Hapa juzi juzi tuliona Tigo imebadilisha jina kuwa Yas na kukawa na tetesi kuwa wanakwepa kodi.

Akijibu swali bungeni kuhusu makampuni yanayobadilisha majina ili kukwepa kodi Mwigulu amesema

"Kupitia sheria ya usimamizi wa kodi ya 238, serikali imeweka sharti kwamba mamalaka ya mapato Tanzania itahakikisha namba ya utambulisho wa kodi yaani TIN inabaki ile ile hata kama kampuni imebadilisha jina. TIN inatumika kufatilia historia yote ya ulipaji wa kodi wa kampuni hivyo mabadiliko ya jina hayaondoi wajibu wa kodi"


Uwezo wako mdogo sana, unakubali majibu mepesi yenye usanii mwingi

Huyo mwenyewe kila siku anabadilisha jina la timu yake ya Singida
 
Kumbe ukishaona VAT imefika usipoweza unafuta kampuni au kubadilisha usajili jina kuanza upya. Au sio
 
Uwezo wako mdogo sana, unakubali majibu mepesi yenye usanii mwingi

Huyo mwenyewe kila siku anabadilisha jina la timu yake ya Singida
🐼
 

SERIKALI KUTUMIA TIN KUDHIBITI KUKWEPA KODI KWA MAKAMPUNI YA KIGENI YANAYOBADILI MAJINA

Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akijibu swali bungeni jijini Dodoma la Mbunge wa Tarime Mjini, Mhe. Michael Mwita Kembaki, aliyetaka kujua hatua zinazochukuliwa na Serikali kwa wawekezaji wa nje ambao kila baada ya miaka kadhaa hubadili majina ya Kampuni kwa lengo la kukwepa kodi

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amesema Serikali imechukua hatua madhubuti kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi unaosababishwa na mabadiliko ya majina ya kampuni za kigeni kwa kuhakikisha Namba ya Utambulisho wa Kodi (TIN) inabaki ile ile hata kama kampuni itabadilisha jina.

Hayo ameyasema bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Tarime Mjini, Mhe. Michael Mwita Kembaki, aliyetaka kujua hatua zinazochukuliwa na Serikali kwa wawekezaji wa nje ambao kila baada ya miaka kadhaa hubadili majina ya Kampuni kwa lengo la kukwepa kodi.

Mhe. Dkt. Nchemba alisema kuwa Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Sheria ya Kampuni, Sura 212, ambayo inawataka wawekezaji kutoa taarifa kwa Msajili wa Kampuni (BRELA) wanapobadilisha jina la kampuni.

“Historia ya mabadiliko yote ya majina ya kampuni huhifadhiwa kwenye kumbukumbu rasmi ili kuhakikisha majina mapya hayawezi kutumika kuficha madeni ya kodi au kushiriki katika shughuli zisizo halali”, alisema Dkt. Nchemba.

Alisema kuwa kupitia Sheria ya Usimamizi wa Kodi, Sura 438, Serikali pia imeweka sharti kwamba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha Namba ya Utambulisho wa Kodi (TIN) inabaki ile ile hata kama kampuni itabadilisha jina kwa kuwa TIN hutumika kufuatilia historia ya ulipaji kodi wa kampuni, hivyo mabadiliko ya jina hayaondoi wala kufuta wajibu wa kodi.

Aidha, akieleza kuhusu kodi zinazotozwa wakati wa kubadili jina la Kampuni kwa watanzania na wageni, Dkt. Nchemba alisema kuwa kubadili jina la Kampuni haiathiri wala haihusiani na masuala ya kikodi.

Alisema kuwa kinachosababisha kuwepo na kodi au ukwepaji wa kodi ni mabadiliko ya umiliki kwa kuuza Hisa ambazo zitaleta kipato cha ziada ambacho kinatakiwa kulipiwa kodi kutokana na faida iliyopatikana.

“Kama mmiliki ni yuleyule ameamua kubadilisha jina la Kampuni kwa ajili ya matangazo ya kibiashara na Namba ya Mlipa Kodi ni ileile, haileti badiliko lolote kwenye kodi”, alifafanua Dkt. Nchemba.

Alisema kuna kampuni za nje ambazo zinamiliki sehemu ya kampuni nchini na hazina shughuli zaidi ya zinazofanyika Tanzania, ikitokea wamebadilishana umiliki unaozidi asilimia 50, hapo kuna kodi ambayo ni lazima ikusanywe.

Alisema Serikali imefanyia kazi kwa kiasi kikubwa suala hilo lililokuwa likijitokeza katika maeneo ya mawasiliano, madini na mengine na amewatoa hofu wabunge kuwa Serikali imeweka kwenye Sheria na inafuatilia kwa umakini panapotokea jambo hilo na kodi stahiki ya Serikali inakusanywa.
 

Attachments

  • Gi8eyj-XkAAWwG9.jpg
    Gi8eyj-XkAAWwG9.jpg
    66.4 KB · Views: 2
  • FvwdLrlXgAAMEYf.jpg
    FvwdLrlXgAAMEYf.jpg
    72.9 KB · Views: 3

SERIKALI KUTUMIA TIN KUDHIBITI KUKWEPA KODI KWA MAKAMPUNI YA KIGENI YANAYOBADILI MAJINA

Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akijibu swali bungeni jijini Dodoma la Mbunge wa Tarime Mjini, Mhe. Michael Mwita Kembaki, aliyetaka kujua hatua zinazochukuliwa na Serikali kwa wawekezaji wa nje ambao kila baada ya miaka kadhaa hubadili majina ya Kampuni kwa lengo la kukwepa kodi

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amesema Serikali imechukua hatua madhubuti kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi unaosababishwa na mabadiliko ya majina ya kampuni za kigeni kwa kuhakikisha Namba ya Utambulisho wa Kodi (TIN) inabaki ile ile hata kama kampuni itabadilisha jina.

Hayo ameyasema bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Tarime Mjini, Mhe. Michael Mwita Kembaki, aliyetaka kujua hatua zinazochukuliwa na Serikali kwa wawekezaji wa nje ambao kila baada ya miaka kadhaa hubadili majina ya Kampuni kwa lengo la kukwepa kodi.

Mhe. Dkt. Nchemba alisema kuwa Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Sheria ya Kampuni, Sura 212, ambayo inawataka wawekezaji kutoa taarifa kwa Msajili wa Kampuni (BRELA) wanapobadilisha jina la kampuni.

“Historia ya mabadiliko yote ya majina ya kampuni huhifadhiwa kwenye kumbukumbu rasmi ili kuhakikisha majina mapya hayawezi kutumika kuficha madeni ya kodi au kushiriki katika shughuli zisizo halali”, alisema Dkt. Nchemba.

Alisema kuwa kupitia Sheria ya Usimamizi wa Kodi, Sura 438, Serikali pia imeweka sharti kwamba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha Namba ya Utambulisho wa Kodi (TIN) inabaki ile ile hata kama kampuni itabadilisha jina kwa kuwa TIN hutumika kufuatilia historia ya ulipaji kodi wa kampuni, hivyo mabadiliko ya jina hayaondoi wala kufuta wajibu wa kodi.

Aidha, akieleza kuhusu kodi zinazotozwa wakati wa kubadili jina la Kampuni kwa watanzania na wageni, Dkt. Nchemba alisema kuwa kubadili jina la Kampuni haiathiri wala haihusiani na masuala ya kikodi.

Alisema kuwa kinachosababisha kuwepo na kodi au ukwepaji wa kodi ni mabadiliko ya umiliki kwa kuuza Hisa ambazo zitaleta kipato cha ziada ambacho kinatakiwa kulipiwa kodi kutokana na faida iliyopatikana.

“Kama mmiliki ni yuleyule ameamua kubadilisha jina la Kampuni kwa ajili ya matangazo ya kibiashara na Namba ya Mlipa Kodi ni ileile, haileti badiliko lolote kwenye kodi”, alifafanua Dkt. Nchemba.

Alisema kuna kampuni za nje ambazo zinamiliki sehemu ya kampuni nchini na hazina shughuli zaidi ya zinazofanyika Tanzania, ikitokea wamebadilishana umiliki unaozidi asilimia 50, hapo kuna kodi ambayo ni lazima ikusanywe.

Alisema Serikali imefanyia kazi kwa kiasi kikubwa suala hilo lililokuwa likijitokeza katika maeneo ya mawasiliano, madini na mengine na amewatoa hofu wabunge kuwa Serikali imeweka kwenye Sheria na inafuatilia kwa umakini panapotokea jambo hilo na kodi stahiki ya Serikali inakusanywa.
TIN ikibakiki hiyo hiyo , hakuzui MTU kupata nafuu ya Kodi ya uwekezaji na akumbuke TIN inatumika katika biashara ya mauzo na manunuzi ya kila siku kirahisi Una weza kusema Kodi ya mauzo, sasa nafuu ya Kodi inayoongelewa hapa ni Kodi ya faida ya makampuni, unapofunga Mahesabu ya Mwaka.
 
Wakuu,

Hapa juzi juzi tuliona Tigo imebadilisha jina kuwa Yas na kukawa na tetesi kuwa wanakwepa kodi.

Akijibu swali bungeni kuhusu makampuni yanayobadilisha majina ili kukwepa kodi Mwigulu amesema

"Kupitia sheria ya usimamizi wa kodi ya 238, serikali imeweka sharti kwamba mamalaka ya mapato Tanzania itahakikisha namba ya utambulisho wa kodi yaani TIN inabaki ile ile hata kama kampuni imebadilisha jina. TIN inatumika kufatilia historia yote ya ulipaji wa kodi wa kampuni hivyo mabadiliko ya jina hayaondoi wajibu wa kodi"


Muongo mkubwa sana huyo.

Hivi bado ana fikra potofu kwamba Wananchi wote kabisa wa Tanzania ni Wajinga wa kiasi hicho anachofikiri yeye?

Wale Watu wa 'Zidumu Fikra za Mwenyekiti' wamebaki wachache Sana, wengi wao walishatangulia mbele za haki.
Watu wengi zaidi waliopo zama hizi ni Watu wa 'Kizazi Cha Kuhoji.' Anapaswa kulitambua Jambo hili
 
Muongo mkubwa sana huyo.

Hivi bado ana fikra potofu kwamba Wananchi wote kabisa wa Tanzania ni Wajinga wa kiasi hicho anachofikiri yeye?

Wale Watu wa 'Zidumu Fikra za Mwenyekiti' wamebaki wachache Sana, wengi wao walishatangulia mbele za haki.
Watu wengi zaidi waliopo zama hizi ni Watu wa 'Kizazi Cha Kuhoji.' Anapaswa kulitambua Jambo hili
Na wewe ujuaji mwingi wakati kichwani hamna kitu

Uelewe kitu kimoja unaponunua au kuuza kampuni huwa kuna vitu vinne mnakubaliana kwenye kuuziana

Cha kwanza mnauziana mali za kampuni
Cha pili mnauziana madeni ya kampuni
Cha tatu nnauziana wafanyakazi wa kampuni
Cha nne mnauziana jina la kampuni au kwa lugha ingine mnauziana brand ya kampuni brand bei yake huwa kubwa sana sababu mtu kaijenga muda mrefu sana kuifanya biashara ifahamike sokoni

Hivyo kila kitu huwa na bei yake.Mnunuzi aweza amua kuwa nanunua mali tu za kampuni.Madeni sichukui ,wala wafanyakazi sichukui au ,wala brand au jina la kampuni sichukui nitatengeneza brand au jina langu mwenyewe

Au aweza sema nitachukua mali na wafanyakazi baadhi au wote ,madeni sichukui na jina sichukui nk

Hivyo kujua kwa nini mtu anabadili jina lazima uende ukaaangalie mkataba wa mauziano alinunua nini lakini kwa kawaida tu bei za brand huwa kubwa mno kuliko hata mali za kampuni mara ingineb.Mfano unataka kununua timu mfano Yanga au simba bei yake sio ya kitoto bei ya jina au brand itakuwa kubwa kuliko majengo na mabasi waliyonayo ndio maana wengine huamua kuanza na brand name zao mpya kama AZam ,Namungo nk

Kwa wajuzi wa biashara wanaelewa kuwa aliyenunua Tigo ni wazi aliona bei ya brand kwake mziki mrefu akaamua tu asinunue aanzishe tu brand yake ya yaas maxxc

Watanzania hasa ngozi nyeusi uzoefu wa biashara wengi uko zero kazi kuhisi hisi vitu tu kuwa ooh yule kanunua kampuni kabadili jina mwizi anatuibia kodi na unakuta anayesema hivyo maisha yake yote hajawahi uza hata peremende lakini ujuaji mwingi wa kijinga Kama wa kwa kwako huo
 
Walimkimbia Tundu hao
Ujinga mzigo mkubwa mno ulionao.Majina ya kampuni hununuliwa pia unaponunua kampuni.Waweza kataa kulipia jina ukaja na la kwako .Hivyo kupunguza gharama za kununua kampuni

Wewe hamnazo.kichwani
 
Na wewe ujuaji mwingi wakati kichwani hamna kitu

Uelewe kitu kimoja unaponunua au kuuza kampuni huwa kuna vitu vinne mnakubaliana kwenye kuuziana

Cha kwanza mnauziana mali za kampuni
Cha pili mnauziana madeni ya kampuni
Cha tatu nnauziana wafanyakazi wa kampuni
Cha nne mnauziana jina la kampuni au kwa lugha ingine mnauziana brand ya kampuni brand bei yake huwa kubwa sana sababu mtu kaijenga muda mrefu sana kuifanya biashara ifahamike sokoni

Hivyo kila kitu huwa na bei yake.Mnunuzi aweza amua kuwa nanunua mali tu za kampuni.Madeni sichukui ,wala wafanyakazi sichukui au ,wala brand au jina la kampuni sichukui nitatengeneza brand au jina langu mwenyewe

Au aweza sema nitachukua mali na wafanyakazi baadhi au wote ,madeni sichukui na jina sichukui nk

Hivyo kujua kwa nini mtu anabadili jina lazima uende ukaaangalie mkataba wa mauziano alinunua nini lakini kwa kawaida tu bei za brand huwa kubwa mno kuliko hata mali za kampuni mara ingineb.Mfano unataka kununua timu mfano Yanga au simba bei yake sio ya kitoto bei ya jina au brand itakuwa kubwa kuliko majengo na mabasi waliyonayo ndio maana wengine huamua kuanza na brand name zao mpya kama AZam ,Namungo nk

Kwa wajuzi wa biashara wanaelewa kuwa aliyenunua Tigo ni wazi aliona bei ya brand kwake mziki mrefu akaamua tu asinunue aanzishe tu brand yake ya yaas maxxc

Watanzania hasa ngozi nyeusi uzoefu wa biashara wengi uko zero kazi kuhisi hisi vitu tu kuwa ooh yule kanunua kampuni kabadili jina mwizi anatuibia kodi na unakuta anayesema hivyo maisha yake yote hajawahi uza hata peremende lakini ujuaji mwingi wa kijinga Kama wa kwa kwako huo
Usifikiri kwamba Mimi Sina akili kama ulivyo wewe.

Nazifahamu vizuri Businesses arrangements pamoja na Sheria, Kanuni mtawalia zinazosimamia masuala haya ya biashara katika nchi ya Tanzania kwa hiyo huwezi kunidanganya kuhusu masuala haya.
 
Back
Top Bottom