Mliompotosha tuambieni Ramadhani Singano yuko wapi

kibaravumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
6,634
Reaction score
7,015
Kuna mchambuzi mmoja aliyejaribu kuleta presha na kutengeneza majungu akiamini kwa njia hiyo Simba itafanya lolote alitakalo.

Mchambuzi huyo aliyepachikwa jina la "taka taka" alihusika sana kumpotosha huyo kijana na kupelekea hadi hivi ninavyoandika hapa, huyo kijana hajulikani alipo na sina uhakika na mafanikio yake.

Wasiwasi wangu ni kuwa hakustahili kuwa alipo pengine angekuwa anafaidi matunda ya soka Simba au vilabu vya nje ambavyo vingemuona akiwa Simba.

Tuambieni leo baada ya ujuaji wenu wa kiswahili, yuko wapi? Au mlimpotosha mkamtelekeza?
 
Dogo si alisajiliwa TP Mazembe pamoja na Eliud Ambokile ?
 
Dogo si alisajiliwa TP Mazembe pamoja na Eliud Ambokile ?
Hakupata nafasi, akapelekwa Nkana kwa mkopo, nao sijui wamempeleka wapi maana kwenye line-up za Nkana huwa simuoni
 
Yuko wapi Ibrahim ajibu[emoji1787][emoji1787]

Sent using Jamii Forums mobile app
Ibrahim Ajib walimdanganya akaanza kuvaa jezi za Utopolo ilihali yuko Simba. Akasajili utopolo kama takataka walivyokuwa wanabwabwaja. Akategwa na Usajili wa kurudi tena Simba akanasa tunduni kwa sasa yupo Msimbazi analambishwa matapishi yake ili akili ikae sawa.
Hasan Kessy, Pius Buswita, Malimi Busungu, Nonga nk nk woote hao walihadaika kula nauli ya Simba wakaishia kuisaliti waulizeni kilichowapata Huko Utopolo.
 
Na uzuri simba asingetemwa.

Mwenzake Ndemla yupo tu kiwango kinapanda na kushuka ila yupo tu pale simba.

Kiburi kilimponza dogo, Azam wakamtema akaokotwa na mazembe nao wamemtupa migodini zambia huko.
Yupo kule walipo akina Kakolanya na Gadiel Michael

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Kwahiyo ulitegemea dogo atacheza milele?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…