Mliomuibia mdogo wangu magunia 70 ya mahindi Singida rudisheni tafadhali

Mliomuibia mdogo wangu magunia 70 ya mahindi Singida rudisheni tafadhali

Nenda Zanzibr, Unayapata mahindi yako yote, kule kuna watu bwana. au mwendee malawi hapo.
Zanzibar sehemu gani? Kwenda kwa kubahatisha pia kuna kutapeliwa mara ya pili,na Malawi kijiji gani?
 
Mleta mada kama vile anajitekenya....usikute yeye ndo huyo dogo sasa anatafuta majibu,in short mtoa Mada ndiye kajiibia. Anatafuta majibu ya kumpa boss wake. Tusimwamini maana jf kila kitu kinawezekana
 
Mi muhuni wa Manzese trust me dogo kakupiga yaani hajui hata kudanganya

Hivi wewe unaweza kwenda sehemu huna unayemjua ukaacha mzigo ukaenda lala kwa akili ya kawaida ?


Msamehe tu kama ameiba utajua tu adhabu ya muumba ni kali sana na inaumbua utajua tu


Nitafanya upuuzi wote ila sio dhuluma manung'uniko yake tu tayari ni laana tosha
 
Kama kisa chako ni kweli!
Kuna uwezekano huyo dogo
Kakupiga au la
Sema anakupanga tu

Ova
 
Dogo naamini hana makosa kwa kukosa uzoefu wa biashara..na inaonekana dogo wako mlaini kama mkate wa boflo...chamsingi karoge mahindi yarudi...
 
Dogo naamini hana makosa kwa kukosa uzoefu wa biashara..na inaonekana dogo wako mlaini kama mkate wa boflo...chamsingi karoge mahindi yarudi...
Umenena vema,ndo maana ktk maswali yangu 3 hapo juu(japo hajajibu) nilitaka kufahamu uzoefu wa dogo ktk kusafiri,hii ingenionyesha ni kwa kiasi gani anaweza zikabili mishemishe
 
Twende taratibu,kumbuka naandika maelezo hapa na baadae yaweza kuwa ushahidi mahakamani!
1.Kwahiyo wakati unampatia mzigo ulishafahamu juu ya uwezo wake wa kusafiri sehemu za mbali na nyumbani?
2.Je,wakati unampatia mzigo ulisahau kumwambia wapi/stoo gani utahifadhiwa ama nani atampokea?
3.siku zote ukisafirisha wewe huwa unauza jumla au rejareja popote barabarani?
Nitaendelea ukishajibu haya!
1.Mara nyingi nimekuwa nikisafiri nae hvy kuhusu uzoefu Sina mashaka nae.
2.Kwa Mara zote ambazo nimekuwa nikisafirisha mzigo nilikuwa nafika kwa wakati hvy lilikuwa jukumu la mteja kuhifadhi mzigo kwani tulikuwa tunamalizana nae palepale.Shida ya huu mzigo nikwamba gari ilipata hitilafu so ikafika muda ambao mnunuzi ilibidi afike kesho yake.
3.Siuzi rejareja, huwa na sambaza/kupeleka kwa order
 
Twende taratibu,kumbuka naandika maelezo hapa na baadae yaweza kuwa ushahidi mahakamani!
1.Kwahiyo wakati unampatia mzigo ulishafahamu juu ya uwezo wake wa kusafiri sehemu za mbali na nyumbani?
2.Je,wakati unampatia mzigo ulisahau kumwambia wapi/stoo gani utahifadhiwa ama nani atampokea?
3.siku zote ukisafirisha wewe huwa unauza jumla au rejareja popote barabarani?
Nitaendelea ukishajibu haya!
Mami nauliza, mzigo wa nafaka kama huo hushushwa kwa mteja, ilikuwaje akashusha uwanjani?

Ina maana alipofika Singida hamkuwasiliana kuhusu mteja na mahali pa kushushia, nawe hukufuatilia kama amefika na mzigo ameshushia wapi?

Mteja wako hamkuwasiliana muda wote hadi mahindi yale nje, yaibiwe, hadi mdogo wako akujulishe asubuhi kwamba kakuta uwanja mweupe hamna hata punje?
 
Kwanini hakumtafuta mteja akayashusha mahindi kwake na kumkabidhi?
 
Stori ya kutunga hiyo, hata maudhui hayaendani na nia ya kupost(kutaka ushauri)! Kwanza huwezi kusafirisha mzigo mkubwa huo bila kujua anwani ya mteja,
2-mteja ndo angesema destination na kituo cha kupakulia ili iwe rahisi kupokea na kufanyia biashara zake!
3-Mara nyingi wasafiridhaji wanachukua advance tu(ya ku facilitate usafirishaji) na pesa kamili wanachukua baada ya kufikishwa, ambapo mnunuzi huwa anamlipa mletaji na mletaji anamalizana na msafirishaji!
4-Gunia 70 za mahindi ni mlima huo, ni uwanja wa nani utamwaga tu mxigo bila kukubaliana na mmiliki wa eneo!
Japo Yako mapungufu mengi ktk uwasilishaji ila safari ijayo jitahidi kidogo, ila pia maudhui ya stori kutokana na kichwa cha hbr ilikuwa kama unatoa onyo kwa wezi kabla kenda 'kuroga' lkn kumbe unataka ushauri juu ya huyo 'mdogo' wako wa kubuma! Kumbuka, uongo ukitaka ufanane na ukweli, basi weka kaualisia kidogo(kaukweli) ndiyo utapendeza! Pia, muongo mzuri ni yule mwenye kumbukumbu nzuri kuwa hapo awali alisema nini!😀 Pole kwa good idea bt bad approach!
 
Back
Top Bottom