Mlionidhihaki na Kudai Mimi ni Yanga SC pale nilipotoa Angalizo la Kiufundi kuihusu Simba SC naomba na leo endeleeni Kunidhihaki tena!

hii inatuonesha jinsi ligi yetu isivyo na uwiano sahihi kati ya timu zenye pesa na zile za kuunga unga! Unaweza kushangilia kupata matokeo ya goli 5 dhidi ya Alliance lkn mechi isikusaidie kujua ubora wa timu yako!
Simba wajipange haswa mechi za nyumbani maana kule ugenini hata wale Js Saoura nao wanaonekana wakiwa kwao sio vibonde kihivyo.
Yote kwa yote Simba wajitahidi kuwa aggressive kwenye marking wasisubiri mabeki ndio wakabe mtu kama Kotei kwa jinsi alivyo nategemea angekua mhanga wa kadi za njano kwa ajili ya kukata umeme kabla nyumba haijaungua lakini hana moyo wa kikatili.
 
Naomba majeshi yetu yaliyoko Congo yarudishwe tu huu sio ujirani mwema kabisa hawa watu wanafiq hawawezi kutufanyia hivi sisi watanzania wanasahau majeshi yako mstari wa mbele huko Congo.[emoji4][emoji4][emoji4]

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana uhusiano wetu na serikali ya Felix uendelee hii mechi ilikuwa iishe kwa 8-0 ila jamaa wakapunguza kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kona ya kwanza beki za simba zinaruhusu kipa wao abanwe na foward sumbufu za vital kisha mpigaji awe free mi nawaza mbona hii ni technic nayowafundisha wanafunzi kabisa hapa shuleni watalaamu kama wale wanashindwa vipi kuyajua haya?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Nayajua mengi kuhusu Haruna Niyonzima kuliko hata haya ' Kiduchu ' tu unayoyajua Wewe hapa na siyo huyu tu bali 85% ya Wachezaji wa Simba na Yanga ( ambao wengi wao ni Wanangu / Wana kabisa ) ila ' Kimaadili ' kabisa sijadiriki hasa kuyaweka hadharani na kwa Wewe kuyaweka hivi sidhani kama ni busara. Tujifunze kuwa na Vifua na siyo ' Wapayukaji ' hasa kwa mambo binafsi ya Mtu Mitandaoni.
 

Umeandika pointi ya msingi sana hapa...wachezaji wa kigeni karibu wote wakija Tanzania mpira wao unakwisha kwa sababu ya mijike ya kitanzania na hasa ile ya Kinondoni, Mwananyamala, Kigogo, Sinza na kwingineko...Wako wapi akina Katalay na Pitichou Kongo...Hata Bernard Mwalala naye yumo kwenye kundi hili....ukiwauliza wachezaji wenyewe wa kigeni watakwambia kuwa katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati hakuna wanawake wazuri kama wa Tanzania..Binafsi huwa nashangaa kwa kauli yao hii..yaani eti hata Rwanda tumewashinda....ila ukichunguza ni kuwa wanawake wa Kitanzania wana sifa ya ajabu mno...hapa siyo suala la hela...kiichopo ni kuwa wanawake au mijike ya Tanzania inapenda 'kuwa' na watu maarufu...utakuta rafiki yangu mchezaji kutoka Kenya alikuwa na lijike pale Sinza lenyewe ndilo linampa hata gari ya kutembelea....Lakini ukienda kwa undani hata wanaume nao ni hivyo hivyo..wanapenda kujihusisha na watu maarufu na hasa wachezaji..utamsikia mwingine akisema leo niloikuwa na Tshisshimbi tulikuwa kwenye baa fulani na nilimpa ofa ya bia...ovyo sana...yaani mashabiki ndio wanaiowaua wachezaji kwa kutoa ofa za kilevi....
 
Makosa hayo yanathibitisha tuna kocha wa aina gani, hayo ni mazoezi ya training ground week in week out.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makosa hayo yanathibitisha tuna kocha wa aina gani, hayo ni mazoezi ya training ground week in week out.

Sent using Jamii Forums mobile app
Inabdi alifanyie sana lile kosa kazi kona mbili zimetoa matunda mpigaji yuko free kabisa na kwenye kona ni kawaida kabisa kuwa yule anaewasumbua mabeki huwa sio mfungaji kabisa labda kwa bahati mbaya mfungaji huwa yuko mbali anamove na mpira unavyokuja na mara nyingi huwa ni beki au foward mrefu ukweli lile sio kosa la kuruhusu kwenye match tafu kama ile

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Washabiki sijui wapenzi wa soka msiwe namihemko hivyo, kufungwa ni moja ya matokeo ya mchezo wa soka.

Kikubwa ni kuangalia mapungufu yalikua wapi nakuyafanyia kazi, vitu viwili ndivyo vilivyosababisha Simba kufungwa magoli mengi Jana

Kucheza bila tahadhari, na ukabaji wa hovyo .sijui Mkufunzi aliwaambia nini wachezaji na sikuona game plan ya timu ilikuaje, timu ilicheza kama inacheza na Majimaji FC

Magoli mawili ya kona tuliyofungwa wachezaji wa Vita walikua huru kabisa hakuna aliekabwa wakati mipira kama ya kona nilazima kila Mtu atembee na Mtu wake

Over confidence ndio iliofanya tukacheza bila tahadhari na hatimae tukaadhibiwa goli lakwanza mpira umeshindwa kumilikiwa kwa umakini ukamtoka kotei tukaenda kuadhibiwa

Goli la penalty mpira umeshindwa kudhibitiwa na Okwi nafikiri kama sio chama umekuja golini tukatoa penalty

Kocha usikae hapo unashika kidevu tu ongea na wachezaji watekeleze majukumu yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwambie na Kagere umakini kwenye nafasi aliyoipata pengine ndio imeigharimu Simba. Kipa anakuja ameinama badala ya kupiga mpira juu (kama Messi) yeye akamlenga, that was the beginning of the fall.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata mabeki anaowatumia ugenini hawawezi kutusaidia. Gyan, Tshabalala na Wawa hawawezi kucheza mpira wa kishambuliwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ama!!
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwambie na Kagere umakini kwenye nafasi aliyoipata pengine ndio imeigharimu Simba. Kipa anakuja ameinama badala ya kupiga mpira juu (kama Messi) yeye akamlenga, that was the beginning of the fall.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna watu nilikua nikiwaambia jana ile nafasi tuliyoipoteza ndio ilituanzishia maafa mchezo ungalikua tofauti kabisa kama tungefunga lile goli

Japo tulitakiwa kukaba kwa umakini na kucheza kwa tahadhari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna watu nilikua nikiwaambia jana ile nafasi tuliyoipoteza ndio ilituanzishia maafa mchezo ungalikua tofauti kabisa kama tungefunga lile goli

Japo tulitakiwa kukaba kwa umakini na kucheza kwa tahadhari

Sent using Jamii Forums mobile app
Shida ya kocha hajui acheze vipi, wapi na timu gani. Huwezi kucheza mpira wa kufunguka kwa AS Vita tena ugenini, ndio maana tumekula 5 huku tunaongoza possession. Tatizo namba moja kwa Simba ni kocha, enzi za akina Leschante na Masoud timu ilikuwa na very good discipline kwenye marking ndio maana kuwafunga Simba ilikuwa kazi ngumu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Gentamycine, kwanza nakupa pole kwa kichapo cha hamsa. Aidha, nikupongeze kwa mawazo yako mazuri ya kulijenga soka la Tanzania. Vile vile, niungane na wewe kutahadharisha juu ya ushabiki wa Sifa za kupindukia tunazowapa wachezaji wetu hasa Simba na Yanga. Kiukweli jana wachezaji wote wa Simba walikuwa wanakabia macho. Kidogo Gyan alijitahidi kuwasumbua Wakongo wale. Ilibidi wamchape viatu vya kumnyamzisha. Mwisho naomba mkuu mmkanye Manara aache kuwapa sifa wasizositahili wachezaji, maana kuna mtakuja chapwa 10-0. Nawasilisha mkuu.
 
Kwa kweli inatia sana hasira mkuu.. lile goli hata sisi huku kitaa tunavyochezaga huwa hatufungwi goli kama lile
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…