Mliopo Dar, hali ya kibiashara ikoje sasa?

Mzee baba naona huko Kilimanjaro/Moshi wafanyabiashara 650 wameandika barua TRA ya kufunga biashara zao.

Huku dar tunaishi kiujanja ujanja tu kama kawaida yetu.
Mzee baba naona huko Kilimanjaro/Moshi wafanyabiashara 650 wameandika barua TRA ya kufunga biashara zao.

Huku dar tunaishi kiujanja ujanja tu kama kawaida yetu.
Huku hali ni tete mzee mwenzangu, mimi pia nataka nika shutdown TIN yangu isije kulimbikiziwa madeni bure.
 
Duh, gemu ndio imefikia huko mkuu wangu?
Yaani sasaivi biashara iliyobakia ni ile ya kuuza kitu cha 100,200,500 mpaka elfu tu,juu ya hapo hakuna biashara
 
Ndoo za plastiki zimepanda bei, na zimekuwa dili. Biashara njema kwa waziuzazo. Vibomba vya plastiki vya kuweka kwenye ndoo, navyo si haba. Sanitaiza. Na bidhaa zote ziendanazo na wakati uliopo, soko lake zuri kwa wachuuzi.

Levo siti imesababisha fursa ya kuchukua leseni za muda mfupi LATRA kwa wanaotaka kujiunga kutatua tatizo la usafiri. Bodaboda na Bajaji ruksa CBD. Hili ni soko zuri lengine.
 
Kwenye usafirishaji ni habari njema kwa wenye bikes na hata huko kwa sabuni na sanitizer soko litakuwa liko freshi.

Vipi katika nyanja zingine kama vyakula na soko la kariakoo?
 
Jibu Jepesi kabisa,,,Ngoma ni nzito!!

Naona madhara ya Corona yakijikita zaidi kwenye Uchumi.

Mungu atusaidie mana ikiendelea hvi tutapoteana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa mkuu ila huku nilipo ngoma ni zaidi ya nzito mkuu! Af mishe za kuganga njaa ni tight ku survive kuliko sekta ya ajira.

Huko kwenye ajira sekta binafsi ndio tumepigwa kofi. 3-6 Months notice likizo bila malipo. Ina maana kama una side business unaendelea kukimbiza ila too bad multiplier effect imeshatinga nako.

Hamna afadhali zaidi ya kucheki line mikoa mingine ambayo unaweza ishi kivyovyote.
 
Kijiji kipi utakuta hela mkuu, maana uchumi wetu unategemea international business. Vijijini ma NGO ama watalii ndio wanapelekaga hela ila kama Donors wamejifungia hela zinakujaje bongo? Bora utulie maana hamna mahali pepesi pa kuganga njaa kama DSM.
 
Kwenye usafirishaji ni habari njema kwa wenye bikes na hata huko kwa sabuni na sanitizer soko litakuwa liko freshi.

Vipi katika nyanja zingine kama vyakula na soko la kariakoo?
Gari Bandarini na mizigo mingi imepungua either kutoka Japan ama China,Kiuhalisia sie tunategemea sana mzunguko mzuri wa Biashara toka nje..

Gari ukiagiza zinachelewa kufika (Meli nyingi hazifanyi kazi kama zamani)

Wanaofuata Mzigo China sitaki ku I imagine hali wanayopitia kwa Sasa(Stock ikiisha madukani hali itakuwa mbaya zaidi



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yes Labda mkoani,, Ila mie Binafsi kwa Maneno machache "Hali ni Tete"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…