kidonto
JF-Expert Member
- Jan 5, 2014
- 1,961
- 2,918
Majuzi nimerudi toka south africa nikipita nchi za zambia na zimbabwe, kilichonishangaza ni thamani ya kwacha ya zambia kuwa juu kuliko rand ya south africa, je? Ni kweli zambia wana uchumi mzuri kuliko tanzania , kenya ama south africa? Wakati rand 1 ni sawa na t' sh. 150, kwacha 1 ni sawa na t'sh. 300, ni nini kimefanya zambia wawe juu hivi? Sababu ya shaba? Mbona south africa wana gold? Ambayo kwa uelewa wangu ni zaidi ya shaba? Mbona hata kwa muonekano lusaka huwezi kuilinganisha na dar es salaam? Achilia mbali j'burg? Nlijaribu kuwauliza wenyezi wakasema serikali ilichofanya ni kuondoa sifuri kwenye noti zao, baadala ya 10,000 wakatoa sifuri 2 ikawa 100, 5,000 ikawa 50, zamani ulihitaji kutoa kwacha 3000 kununua soda leo unatoa kwacha 3, nasikia mpaka msumbiji nao wameondoa sifuri kwenye noti zao na mitikashi yao leo sio ile ya zamani, kama issue ni kuondoa sifuri kwa nini na sisi tusiondoe sifuri na noti kubwa ikawa 100?