Niitongozwa na wanawake wawili ila wote wanatabia za hovyo.
Wakwanza alikuwa na Grocery anauza baa, alinitamkia live kipindi fulani,ila nilikuwa na faili lake kwenye kijiwe ninachokaa asilimia 80 walipiga,nikaachana nae.Baada ya miezi kama mitatu naona timbo hilo ana mimba,akajifungua baba wa mtoto hamjui kile anayempa mtoto anamkataa. Akaa kama mwaka na kurudi kwao Tanga.
Huyu wa pili ndio ilikuwa hatari anabonge la figure black beuty,mtu mzima kidogo alikuja kumtembelea mtoto wa mdogo wake,kipindi hiko nimemaliza chuo. Kuna mwana alikuwa anaduka kwenye hiyo nyumba aliyokuwa akiishi huyo mdada.Basi kuna mida huwaga naenda kupiga stori,basi yule dada lazima aje dukani akae nasi mara ajifunue mipaja hiyo imenona, baadae akanifungukia. Nikasema yaani hili zigo lote langu siliachi, basi kwenye ileile nyumba kuna mwana mwengine anakula sana bange sometimes huwaga tunataniana,mida ya night kuna mjumba mmoja mbovu hukaa na kula bange zake. Basi na kumbuka nimetoka zangu kucheki mechi ya UEFA,hapo tumebishana sana kijiweni baada ya mechi kuisha,saba kasoro huyo na rudi home.Kama kawa mwana na mkuta anakula kijiti,ananiita ile kuangalia na muona yule mdada na anakipisi chake anavuta,nikapiga nae stori kidogo huyo nikaamsha.Kesho yale na kutana na mwana ndio ananiambia yule mdada ni mke wa mtu na mumewe anaendesha malori na yy kishapiga. Nikaona hapa sipawezi kwanza demu anakula bange pili mke wa mtu,nikampotezea mazima.