ni kwa vile mbagala sikumbuki kuona mashangingi na manissan ya namba za STyakiongozana huko kupeleka wakuba na ving'ora, ingekuwa wilaya ya kinondoni wanakoishi wakubwa wa nchi hii ungeshangaa ambavyo tungepekuliwa hadi kwenye chupi kuhakikisha hakuna mabomu wa hatari iliyojificha. Ukweli hiyo si haki, walitutangazia kuwa kazi ya mabomu imeisha kamilika, wananchi warudi kuendelea na maisha yao na wakarabati nyumba zao, kumbe hawakufuatilia kabisa, hakuna alieuona huo kuwa ni uzembe unampasa mtu kuwajibika walau kwa kujiuzuri, kila mtu ameendelea na cheo chake na zaidi kanufaisha mfuko wake katika zoezi la tathmini na kugawa misaada, MUNGU awape nini, wanatamani mabomu yalipuke na kwingine wakaneemeke. MJOMBA IWAPI AHADI YAKO YA MAISHA BORA KWA KILA MTZ? MIE NATAFUTA NAULI NIKIPATA UTANIKUTA SEBLENI KWAKO IKULU NIKULETEE SALAMU ZA WALIOKUPA KURA ZAO KWA KISHINDO. I am deeply disappointed with your GOVERNMENT mr jakaya.