Mnachokifanya Simba kitawaponza kwenye mechi yenu na Raja

Mnachokifanya Simba kitawaponza kwenye mechi yenu na Raja

kwisha

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2021
Posts
1,779
Reaction score
4,982
Wakubwa wanakuambia sio kila siku ni Jumapili. Na ukitaka kujua tabia ya mke wako wewe kaa kimia tu. Najua mnamini kwa mkapa hatoki mtu ila imani yetu isuvuke mipaka.

Vile mnavyo kwenda kuandika kwenye page za wale Raja Cassablaca mnawapa ile motivation ya wao pia kujipanga kisawa sawa kama wangelicheza kwenye asilimia 50% wanapanda mpaka kwenye asilimia 100% na mwisho mnakwenda droo au mna fungwa lawama zote kwa John Bocco.

Anyway mimi sio nabii wa Mungu lakini huu ni ukweli mechi hii sioni kufunga kwa simba itakuwa droo ya bila bila.
 
Umejitahidi kujenga hoja.

Ila hapo mwisho ndio umeharibu kabisa, yani Unaleta ushauri mzuri alafu ghafla unageuka mtabiri.

Unaanza kupanga MATOKEO
Ushindwe kwa jina la Yesu.

Uzalendo kwanza.

NAZITAKIA KILA LAKHERI SIMBA NA YANGA.

Tanzania Yangu.
 
We jamaa akili iko vipi, kwa hiyo jamaa walipanga kucheza chini ya kiwango ila wanavyozodolewa mitandaoni wanaongeza mazoezi.
 
Kwahivyo walipanga kucheza kwa kiwango cha chini, ila hamasa ya mitandao itawafanya kucheza kiwango cha juu.

Hii hajawahi kutokea hapa duniani
 
Na sisi tunataka tuwafunge hao Raja wakiwa wamejiandaa 100%.

Hatutaki tuwafunge eti kwakuwa walidharau mechi au hawakuchukua tahadhari.

Tunawataka Raja wachukue tahadhari zote wanazozijua iwe nje au ndani ya uwanja ili tuwaonyeshe maana ya kwa "Mkapa hatoki mtu"
 
Wakubwa wanakuambia sio kila siku ni Jumapili. Na ukitaka kujua tabia ya mke wako wewe kaa kimia tu. Najua mnamini kwa mkapa hatoki mtu ila imani yetu isuvuke mipaka.

Vile mnavyo kwenda kuandika kwenye page za wale Raja Cassablaca mnawapa ile motivation ya wao pia kujipanga kisawa sawa kama wangelicheza kwenye asilimia 50% wanapanda mpaka kwenye asilimia 100% na mwisho mnakwenda droo au mna fungwa lawama zote kwa John Bocco.

Anyway mimi sio nabii wa Mungu lakini huu ni ukweli mechi hii sioni kufunga kwa simba itakuwa droo ya bila bila.
Ndio maana Tz watu wengi wanaonekana kama HAMNAZO"kila sehemu ni siasa tu eti kwa mkapa hatoki mtu,kama timu yako mbovu bado unasimamia hiyo kauli?ni kupeana matumaini ya kijinga tu.kwani wakiacha kuandika kwwnye hiyo page yao ndio kitawasaidia nini?au wanapoandika ?Baada ya mechi mtarudi tena hapa ohooo wale wengi wamekulia ulaya!!kwenye mpira hakuna janja janja
 
Usjali atakufa tu hakuna timu inashinda kwa mkapa hata aje bayern atakufa tu
 
Na sisi tunataka tuwafunge hao Raja wakiwa wamejiandaa 100%.

Hatutaki tuwafunge eti kwakuwa walidharau mechi au hawakuchukua tahadhari.

Tunawataka Raja wachukue tahadhari zote wanazozijua iwe nje au ndani ya uwanja ili tuwaonyeshe maana ya kwa "Mkapa hatoki mtu"
Sijaona timu ya kuifunga Raja Casablanca hapa Tanzania
 
Ndio maana Tz watu wengi wanaonekana kama HAMNAZO"kila sehemu ni siasa tu eti kwa mkapa hatoki mtu,kama timu yako mbovu bado unasimamia hiyo kauli?
na kama timu ni mbovu, ya nini basi kuhangaika na wanaosimama nayo hiyo kauli?
 
Wacha waje wanajua ndugu zao toka arabuni wakija kwa Mkapa nini kiliwakuta, wao ni nani wasitetemeke?
 
Utopolo bana..eti daima mbele nyuma mwiko..na mnajua waarabu wa monastril wanachokipenda afu eti mnawaambia nyuma mwiko...
 
Back
Top Bottom