Mnada ambao NHC wamenunua eneo la Urafiki kwa Ekari 50 kwa Bilioni 3 ulifanyika lini? Wapi? Nani walioshirikishwa?

Mnada ambao NHC wamenunua eneo la Urafiki kwa Ekari 50 kwa Bilioni 3 ulifanyika lini? Wapi? Nani walioshirikishwa?

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Nimesoma hapa JF kuhusu NHC kununua eneo la urafiki kwa njia ya Mnada kwa Shilingi Bilioni 3, nikahisi labda wamekosea au walimanisha Dola Bilioni 3, nilipoenda kwenye kurasa rasmi za NHC nikakutana na taarifa ileile.

Taarifa ya Ununuzi - NHC yanunua eneo la Urafiki lenye ekari 50 na majengo yaliyopo kwa Shilingi Bilioni Tatu

Ambacho najiuliza huu mnada ambao umeiwezesha NHC kununua ekari 50 maeneo ya Urafiki, eneo lililopo maeneo ya Ubungo kwa gharama ya Bilioni 3 ulifanyika lini? Na wapi?

Pamoja na hivyo ukichukua eneo lote la Urafiki, majengo ya viwanda na makazi na rasilimali zote za hapo, eneo la Ekari 50 lina thamani ya Bilioni 3 kweli? Tena katikati ya Mji mkubwa kama Dar es Salaam!

Hivi wangapi waliomba hiyo tenda hadi NHC wakashinda? Vipi kuhusu Wapangaji waliopo sasa, je, walijulishwa au kupewa nafasi ya wao pia kuomba kununua eneo hilo? Taasisi nyingine pia je zilijulishwa?

Sikuwahi kusikia huu mnada na hata niliouliza watu wangu wa karibu nao ambao najua ni wazee wa mjini wa kufuatilia masuala ya mnada, hawana hizo taarifa za mnada.

Hiki kinachoendelea kina tafakarisha sana, majibu ya kueleweka yanahitajika hapa.
 
tunakula kwa urefu wa kamba zetu
kama hukusikia chochote kuhusu mnada kamba yako fupi au imekatika
 
Mimi kwa tusenti twangu huwa nasikia tu wapi kuna mnada wa Mbuzi na mazao,
Sasa hiyo 3b ningekuwa nayo kwa hakika isingenipita au kuisikia
Maana kama ukiwa kwenye madili ni haraka kunusa utakacho
Ila kwa hawa naona imepitishwa chini ya carpet
 
Una hoja ya msingi sana, tangu jana nione ile habari ya NHC kununua yale majengo pamoja na eneo kwa bil 3 nikashangaa huo mnada ulifanyika lini na wapi? bilion 3 kwa lile eneo ni pesa ndogo sana, naamini lile litakuwa dili la wajanja wa hii serikali ya wapigaji.
 
Aiseeee nimeiona hii habari leo. Hadi muda huu nimechanganyikiwa b3..
Aiseeeeee
 
Hiyo taarifa siyo ya kuamini... Kwanza pale Kuna residential houses zaidi ya 30. Na Kila Moja inaweza kuwa na gharama ya 500m... Achilia mbali viwanda etc... Kuna hujuma inaendelea hapa
 
Back
Top Bottom