Wabongo ujuaji mwingi, mtu mmoja anajifanya anajua kukosoa ufundishaji, uchezaji, uchumi, n.k. hivi kabla ya ujio wa Manji, Mo na GSM hizi vilabu vilikuwa na hali gani kiuchumi, kimafanikio na kithamani? Tulikuwa tunazidiwa hadi timu za Kenya, Sudani. Leo hii GSM na Mo wamezifanya hizi timu zipande thamani, ubora na mafanikio tele Africa mnaanza majungu na fitina kuwa zinapata faida.
Je mashabiki wanataka pesa au mafanikio? Kwasababu hizo ela ambazo mnazohoji kuwa wanachukua ni matokeo ya hao hao wakina Mo na GSM kuzikuza hizo timu na mwisho kuongeza ushawishi kwa wadhamini ili kufanya wao wasipate hasara kwa kutoa pesa zao mifukoni kuendesha timu. Kabla ya ujio wa hawa watu vilabu vilikuwa vinaingiza sh ngapi kiasi kwamba tuone hivi vilabu vilikuwa na pesa za kutosha?