Mnadhibiti vipi wizi katika ujenzi?

Mnadhibiti vipi wizi katika ujenzi?

Ligaba

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2018
Posts
1,063
Reaction score
2,874
Habari kwa wote.

Ni imani yangu JF ni sehemu halisi kwa kila aina maswali yanayosumbua katika jamii. Leo naomba tupeane mbinu za kudhibiti wizi hasa wa mafundi tunaowakabidhi dhamana ya kutujengea.

Kwa muda ambao nimeshughulikia mambo ya ujenzi nimegundua pamoja na ugumu halisia wa kujenga lakini kuna sehemu inachangiwa na mafundi kuanzia msingi na boma, fundi umeme, kupaua, sijui bomba, rangi, yaani kila fundi anayehusika hukugeuza fursa akuongezee cha juu.

Mathalani nimewahi kuongea na rafiki yangu yeye ni mtu wa kupaua ni mbinu gani hutumia kupata cha juu? Alichonijibu ni kuwa watu wengi huibiwa hasa kwa mabati ya vipimo vya viwandani, fundi atakupeleka kwenye kiwanda anachokijua au hata ukimpeleka kiwanda chako ukijaribu kumpa nafasi ya kuongea na mtu wa mauzo umeumia.

Anasema Mara zote huwa wanazidisha idadi za mita na vile watu wengi hawajui hesabu za bati basi zikishakatwa atapata idadi za nyumba yako, idadi aliyozidisha anatumiwa fedha zake kwa simu na hapo huwa ameshakuibia.

Mtu wa umeme nae aliniambia hivyo hivyo, atakununulisha vifaa kibao akipanda dalini anafunga vichache, baadhi ya vile vya thamani alikusudia kuiba atatia kwenye mkoba wake atauza kwa mteja mwingine wakati mwingine.

Watu wa cement nao hivyo hivyo wanakuibia mifuko itauzwa kwa muuzaji wa jumla kwa bei ya hasara.

Je wenzangu mnatumia mbinu gani wakati wa ujenzi kuhakikishia wizi hautokei ktk site yako? Kama mpo mafundi hebu mtusaidie mbinu tofauti mnazotumia kupata cha juu?
 
Hata wewe wakati unatafuta hela ya kujengea kuna sehemu lazima ulipiga. Iwe ni ofisini bas ulifanya upigaji kwa madokezo ya uwongo na mambo kama za milungula lazma zilihusika. Kama mfanyabiashara bas ulipiga kwa namna yako hukutoa risiti, ulizidisha beii...uliuza na kununua magendo. Maisha yako hivyo, usimbane sana fundi lazima atakuibia tuuu. Japo hutakiwi ku relax ukaibiwa vingi.

Kama unaanza kujenga nyumba anza kujenga fensi kwanza kudhibiti utoroshaji wa vitu kokoto, mawe, tofali mbao, na vingine
Halafu mambo za "Matirio" inatakiwa kwenda fronti wewe "kabageini" dukani kanunue mwenyewe, fundi akisema cement kumi leta 8, bati mita 460 weka 410, marumaru box 100 weka 70.. mbao 320 weka 250... gypsum board 150 weka mia; vitu vikipelea unaongezea.
 
Huwezi kuzuia kuibiwa maana hata hela unayomlipa ni ya kupooza njaa tu
 
Utaibiwa tu. Hadi ujue ujenzi ndio mambo yatakuwa sawa. Binafsi nilijifunza ujenzi. Kama ni bati upige hesabu mwenyewe zinaingia ngapi. Ujuane na WAMILIKIWA WA HARDWARES WAAMINIFU. Kisha unawasiliana nao moja kwa moja kufanya orders. Picha utumiwe whatsapp kama haupo. Ila zaidi ya yote pata msimamizi mwaminifu. Waaminifu wapo wachache. Na waliokosa uaminifu wapo wengi zaidi. Mwizi hatakosa namna ya kukuibia hata ufanyeje.
 
Kwenye kununua mbao wanafupisha tape measure kwa sentimita kadhaa.Wanazidishia kwa kila kipimo wwnapata mihela kibao tu.Zile mita nyingi huwa zimefuposhwa kwa kiasi kinachojulikana
 
Tuendelee kutwanga maji ndani ya kinu...
Juhudi, jitihada, nguvu mali na kazi zetu hazina tija.. Baraka imetoweka!!
 
Tengeneza BOQ lipa kampuni ya ujenzi watakukabidhi funguo nyumba ikiwa imekamilika.

Labda jiulize bank wanaibaje na pesa zote zipo kwenye hesabu na kuna wasomi nguli wa mahesabu?
 
Tengeneza BOQ lipa kampuni ya ujenzi watakukabidhi funguo nyumba ikiwa imekamilika.

Labda jiulize bank wanaibaje na pesa zote zipo kwenye hesabu na kuna wasomi nguli wa mahesabu?
Hapo utaona bora akupige fundi ila sio hao jamaa. Na hela ya kuilipa kampuni wote wanaweza?
 
Ni vigumu kuzuia wizi kwa asilimia 100 ila kwa asilimia 50-75 wizi unazuilika.

Kwanza usimpe fundi uhuru wa kwenda kununua vifaa, muombe ushauri wa vifaa unavyotaka kununua kama kuna uhitaji wa nenda nae kwa ajili ya kuthibitisha vifaa husika ndio vyenyewe.

Mafundi wa Paa/bati, wizi unatokea kwenye ununuzi wa bati, mbao na misumari, fundi anaweza kukuambia nyumba inahitaji mabati 100 kumbe inahitaji bati 80, hata kama upo site unaweza kuibiwa bati mfano unaweza kwenda chooni, fundi akaiba chapu.

Dawa ya kuzuia hii labda uwe unahesabu kila bati linalopandishwa juu lakini mafundi wahuni wanaweza kukuibia huko huko juu.Ili kuzuia hii utafute fundi mwaminifu.

Wizi wa misumari wanachukua misumari wanamwagamwaga chini alafu baadae wanaokota ukiwa haupo au wanaiba kwa kukuambia imeisha kumbe wamechukua.

Epuka fundi kukununulia vifaa

Kaa site wakati mafundi wanajenga ili ujue kinachoendelea kama haupo weka mtuwaminifu asimamie

Jaribu kupita maduka tofauti kuulizia bei ya vifaa mbalimbali ili ujue bei za vifaa.

Tafuta mafundi waaminifu

Kumbuka mwizi naye ni binadamu ukipanga mbinu zako nae anapanga zake.
 
Huku kwenye rangi wanachanganya material wenyewe

Au fundi anakupeleka duka ameshafanya connection tayari

ukifika unapigwa bei na fundi anawekewa chake.

Kuibiwa hakuepukiki
 
Huko tumeshapitia yani bati, nanunua mwenyewe kwa size niliyopewa, halafu fundi akikupa hesabu yake wewe mpotezee tafuta wengine nao watoe hesabu zao utajua tu kama unapigwa.

Kuibiwa kupo ila kwa uzembe wako na uboss unapigwa sana
 
Kuna fundi wa umeme alilala mbele na waya uliobaki baada ya kukamilisha wiring, nilishtukia tu waya umeyeyuka na kwa sababu kulikuepo na mafundi wengine hujui nani wa kummuliza. Nafikiri kumwibia bosi au kusepa na material yaliyobaki huwa wanachukulia ni halali yao.....
 
Ni vigumu kuzuia wizi kwa asilimia 100 ila kwa asilimia 50-75 wizi unazuilika.

Kwanza usimpe fundi uhuru wa kwenda kununua vifaa,muombe ushauri wa vifaa unavyotaka kununua kama kuna uhitaji wa nenda nae kwa ajili ya kuthibitisha vifaa husika ndio vyenyewe.

Mafundi wa Paa/bati,wizi unatokea kwenye ununuzi wa bati,mbao na misumari,fundi anaweza kukuambia nyumba inahitaji mabati 100 kumbe inahitaji bati 80,hata kama upo site unaweza kuibiwa bati mfano unaweza kwenda chooni ,fundi akaiba chapu.dawa ya kuzuia hii labda uwe unahesabu kila bati linalopandishwa juu lakini mafundi wahuni wanaweza kukuibia huko huko juu.Ili kuzuia hii utafute fundi mwaminifu.

wizi wa misumari wanachukua misumari wanamwagamwaga chini alafu baadae wanaokota ukiwa haupo au wanaiba kwa kukuambia imeisha kumbe wamechukua.

Epuka fundi kukununulia vifaa

Kaa site wakati mafundi wanajenga ili ujue kinachoendelea kama haupo weka mtuwaminifu asimamie

Jaribu kupita maduka tofauti kuulizia bei ya vifaa mbalimbali ili ujue bei za vifaa.

Tafuta mafundi waaminifu

Kumbuka mwizi naye ni binadamu ukipanga mbinu zako nae anapanga zake.

Duuu hii inanikumbusha fundi kaniandikia idadi ya bati na bei zake inafika 7m anasema ni kwa jamaa zake atanipeleka siku tumepanga kwenda kununua nikamuacha kwenye mataa nikaendaa kiwanda kingine mwenyewe kwa Muhindi jumla nikalipa 5.6m kila kitu na bado zimebaki na bati 12 za mita 5 baada ya kumaliza kazi.
 
Kupigwa kupo pale pale !
Kama kanisani watu wanapiga sembuse fundi!

Tena ukiwabana sana ndo wanakuharibia kabisa, maana watakununulisha kila kitu ili wakukomoe!

Mara kalete misumari , Mara ongeza kitu flan ..yaan alimradi tu wakutume!
Ukikaa chini wakiwa wanaezeka wanakuangushia hata kipande cha bati kichwani ili utoke,
Kama wanachimba shimo watakurushia hata mchanga,
Kama ni mafundi gereji watajipitisha na Yale manguo yenye grisi wakuchafue!

Note! Kama humuamini fundi usimpe kazi yako!

Chagua fundi mwaminifu, halafu simamia kwenye makubaliano akukabidhi kazi!

Huwezi zuia mwizi tena kazi za kusimamia mwenyewe ndo utaumia zaidi
Mfano! Kazi ya 2mil ukimpa fundi akakupiga laki moja si mbaya sana, kuliko ukikomaa mwenyewe ukajikuta unatumia 3m kwa kununua vitu vikabaki na kuharibika

Hakuna aliyewahi kuzuia kupigwa hayupo!
Ukizuia kupigwa basi utabambikwa
 
Kama unaanza kujenga nyumba anza kujenga fensi kwanza kudhibiti utoroshaji wa vitu kokoto, mawe, tofali mbao, na vingine
Halafu mambo za "Matirio" inatakiwa kwenda fronti wewe "kabageini" dukani kanunue mwenyewe, fundi akisema cement kumi leta 8, bati mita 460 weka 410, marumaru box 100 weka 70.. mbao 320 weka 250... gypsum board 150 weka mia ..........vitu vikipelea unaongezea.

Huu ni ushauri ni ushauri zaidi
 
Kwenye kununua mbao wanafupisha tape measure kwa sentimita kadhaa.Wanazidishia kwa kila kipimo wwnapata mihela kibao tu.Zile mita nyingi huwa zimefuposhwa kwa kiasi kinachojulikana
Hili nimelikuta kwa macho yangu.
 
Utaibiwa tu. Hadi ujue ujenzi ndio mambo yatakuwa sawa. Binafsi nilijifunza ujenzi. Kama ni bati upige hesabu mwenyewe zinaingia ngapi. Ujuane na WAMILIKIWA WA HARDWARES WAAMINIFU. Kisha unawasiliana nao moja kwa moja kufanya orders. Picha utumiwe whatsapp kama haupo. Ila zaidi ya yote pata msimamizi mwaminifu. Waaminifu wapo wachache. Na waliokosa uaminifu wapo wengi zaidi. Mwizi hatakosa namna ya kukuibia hata ufanyeje.
Waaminifu tupo.
 
Tengeneza BOQ lipa kampuni ya ujenzi watakukabidhi funguo nyumba ikiwa imekamilika.

Labda jiulize bank wanaibaje na pesa zote zipo kwenye hesabu na kuna wasomi nguli wa mahesabu?
Labda jiulize bank wanaibaje na pesa zote zipo kwenye hesabu na kuna wasomi nguli wa mahesabu?



JIBU
 
Back
Top Bottom