Mnahubiri nishati safi halafu hamshushi gharama za gesi wala umeme, watu wapikie upepo?

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
9,846
Reaction score
20,319
Niwaulize kitu jamani, hivi hawa watu wanajielewa kweli? Uhamasisha nishati ya kupikia bei ya gesi ipo juu. Mtungi kapandisha kutoka kujaza elfu 17 hadi 25000 kwa mtungi wa kilo 6 halafu anahubiri nishati safi!

Nishati safi my foot? Sasa hao wananchi watapikia upepo au vinyesi vyao? Nauliza kwasababu mtu aache kununua mkaa au kuni bei chee akanunue gesi wakat gesi haishikiki? Umeme ni ghali makato kibao?

Nyie machawa ebu mshaurini, hizi project zake za nishati safi hazitofanikiwa hata kwa chembe maana hakuna ufanisi wowote, unahamasisha watu watumie umeme kupikia kwa huu umeme wa unit 23 elfu 10? Unahamasisha watu wapikie gesi mtungi mdogo kilo 6 ni 25000 ukapanda kutoka 17k hadi 25k

Mama enu amefeli kama alivyofeli kwenye kila kitu maana hana wasahauri makini.

Hii sera imebuma mapema sana!
 
Ni mwendawazimu tu anayeweza kumuelewa huyu mama. Kauli zake nyingi zimejaa mipasho ya kitaarabu; hazina uhalisia.
 
Nilikuwa ninapikia umeme Hadi sept. 30 ,2024 unit 2 Hadi 2.7 kwa siku kwa sh. 123 kwa unit. Ajabu Jana nimenunua unit 25 kwa sh. 9,000=Kwa hali hii anachohubiri Rais hakiwiani na asemayo ! Bei ya umeme ipunguzwe ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…