Mnamuonea sana Karia, ligi zetu ni bora kuliko za Misri na Algeria

kabisa unaona hata zambia msiba wa kaunda wamekataza starehe ila ligi wameruhusu iendelee kwa sharti kwamba goili likifungwa hamna kushangilia maana siku 21 ni nyingi mno mechi kama 4 zilipotea hapo
Sasa utopolo wanamwangushia bomu Karia kwa sababu Karia ndiyo anayewezuia kina Sarpong kufunga magoli.

Walivyowajinga hata vurugu za juzi watasema Karia ndiyo aliwapiga dole la kati.
 
kama ni ubora wa ligi tangu karia aingie madarakani Tanzania mara mbili imeingiza teams 4 mashindano ya CAf na ipo ranked namba 12 na Caf ni ubora gani mnasemea ?kwa hiyo misri siyo ligi ya kujilinganisha nao?tumewazidi siyo kwamba siyo level yetu?
Hebu twende taratibu league inaendeshwa na bodi ya league sio TFF, kama ubora au ubovu wakulaumiwa ni bodi ya league sio Karia. Mimi sijamtaja Karia na kama anafanya kazi nzuri tumpe sifa yake hapa issue kuwa na league kuendeshwa katika usawa bila kuwa na viporo vingi ili ushindani uwe katika ubora kuliko mtu kuwa nyuma hajacheza mechi 5 hii inampa advavantage mpinzani mmoja kuliko mwingine unaweza kuwa na game moja tofauti na itabidi uicheze milingane na wenzako mimi hakuna sehemu nimeongelea Karia sababu naamini bodi ya league ndio jukumu lake kuendesha league na sio TFF.
 
Yanga ni Janga la Kitaifa.
Msajirini Karia awafungie magoli.

Kuna goli la Yanga alilolikataa refa Karia ?
Kuweni na heshima hata japo kidogo basi.
Kocha wenu aliye waita Manyani, mmetafakari kwanini alitamka hayo maneno ?
Karinyo mchezaji mzuri sana, je amemkimbiza Karia ?

Simba ni kama mtoto wa kufikia, anaenda kama familia inavyotaka lakini.
Yanga ni kama mtoto wa familia, kutwa kuchwa ni kudeka tu.
Yanga kazeni Buti,
huu ni mdeko.

Simba mbovu ilifikaje robo fainali ubingwa wa Afrika ?
Nyinyi mlifika lini hapo.

Wakati wa Manji na Malinzi, mlifika wapi ?
Mlichukua kombe la Ubingwa miaka mitatu mfulilizo, mlifika wapi ?

Au mlizuiliwa na Karia ?
 
nawakumbusha tu hii ligi tayari bingwa ni simba sema haijulikani nani atakuwa wa pili...kuna mitambo ya yanga itaanza kushuka soon na kupokelewa airport ikishaanza kuchemsha karia anatupiwa zigo la mavi
Huu ndo utumbo uliotakiwa uandike na si mambo ya kuisha kwa ligi..
 
kama ni ubora wa ligi tangu karia aingie madarakani Tanzania mara mbili imeingiza teams 4 mashindano ya CAf na ipo ranked namba 12 na Caf ni ubora gani mnasemea ?kwa hiyo misri siyo ligi ya kujilinganisha nao?tumewazidi siyo kwamba siyo level yetu?
Ashukuliwe sana Mo kwa uwekezaji wake mkubwa kwenye timu ya Simba kuanzia kwenye swala usajili,mishahara kwa wakati,posho za kuridhisha,uongozi imara imepelekea Simba kufanya vizuri ndo kufanya ligi kuingiza timu 4 Karia hakuna alichochangia hapo hiyo ni shughuli za timu na si za Karia na TFF
 
Al Ahly walianza na mashindano ya vilabu ya dunia wakati lig yao inaendelea, Simba Kuna kipindi timu inakaa wiki mbili haijacheza Ligi eti unapewa nafasi ya kujiandaa na mechi za kimataifa.
Sasa hilo gap la games 3 leo huoni matunda yake. Mwakani wewe Uto Azam wote mnapiga hesabu za mashindano ya kimataifa je bila simba na namungo mngeota wapi ndoto hizo. muda mwingine kuweni na shukrani japo kidogo
 
Tatizo je sisi ratiba ilivyotoka league ilitakiwa kuisha lini? kama tuko ndani ya ratiba au kuna jambo lilitokea kama lile la kifo cha Rais hilo linaelezeka ila league ratiba inatoka ya mwaka mzima na mechi zote na kama ikitokea mechi viporo kwa sababu za msingi huwa zinajazwa sehemu kikubwa league inaisha kwa wakati uliopangwa.
 
Mo na simba yake wanacheza kwenye ligi inayosimamiwa na Tff,hongera kwa karia kwa kleta teams 4 kwa kuipeleka team ya taifa afcon baada ya miaka 39 kwa kupeka teams za vijana afcon,teams za wanawake kushinda mataji kama ya cosafa na kucheza afcon
Kam karia anaweza kulaumiwa kwa kina sarpong na yikpe kutofunga magoli au kina kalinyo na niyonzima kushindwa ku assit kwa nini tusimsifie kupeleka teams 4 in a span of 3 years?
 
ndiyo maana hata msiri ligi haijaisha kuna wakati ratiba inasumbua sisemi kwamba hawakoseagi? ila mfano wa simba kuwa na gepu la mechi tatu liapigiwa kelele mnooo ndipo nikatoa mfano wa misri
 
ndiyo maana hata msiri ligi haijaisha kuna wakati ratiba inasumbua sisemi kwamba hawakoseagi? ila mfano wa simba kuwa na gepu la mechi tatu liapigiwa kelele mnooo ndipo nikatoa mfano wa misri
Misri kabla league haijaanza walisema league itachelewa kuisha kwa miezi miwili kutokana na sababu za corona swali je league yetu iko kama ilivyopangwa? sababu kuwa na league haijulikani toka mwanzo itaisha lini ni gharama kwa team na hasa team zenye budget ndogo ni ngumu sana.
 
hata kama imechelewa au itachelewa hiyo miezi 2 mbona kuna gap la mechi za pyrmids na zamalek?sababu achilia mbali suala la ligi kuisha kuna watu wanalalamikia gepu la namungo na simba wanakuambia mbona wawakilishi wa nchi nyingine michezo ya afrika hawana ma gepu?
ukitoa suala la mkifo cha Jpm,korona ilipo hit mwanzo waziri mkuu alisimamisha michezo yote kama sikosei amri ilidumu kama wiki 2
 
Inabidi kujifunze kwa mataifa ambayo hawaachi gap kubwa au viporo vingi sababu hata hii CAF huwa inasimama muda pale anatakiwa mtu apige viporo vyake kama mechi 3 amalize hii sio jambo zuri kuwa na gaps na sio kwa team za juu tu hata huku chini unakuta gaps ndio maana kulianza na shutuma kuwa mbeya city kanunua baadhi ya games inaweza kuwa kweli au uwongo lakini hii inaletwa na hii hali tunayoitengeneza. Mimi bado naamini team zitacheza CAF na bado watacheza league ya home bila kujenga gaps kubwa na ndio ubora wa league kwa maana ushindani ulio sawa viporo vinaleta hisia mbaya na zinaweza kuwa hazina ukweli lakini kitaleta gumzo tu.
 
Katika kufuatilia kwako kote ligi yetu kweli ilikosa mda wa kumalizika mpk mda huu?
Na sababu gani haswa ya msingi inayopelekea ligi yetu isiishe mpk sasa?
Mkuu, sababu za ligi yetu kusimama mbona zinajulikana.

Ligi ilisimama baada ya Korona kuingia nchini baadae Magufuli aliruhusu iendelee, kisha huwa inasimama kupisha mazoezi ya Timu ya Taifa.
 
Mkuu, sababu za ligi yetu kusimama mbona zinajulikana.

Ligi ilisimama baada ya Korona kuingia nchini baadae Magufuli aliruhusu iendelee, kisha huwa inasimama kupisha mazoezi ya Timu ya Taifa.
Bado haziwezi kuwa sababu za msingi kwasababu zipo ligi zimeisha kwa sababu hizo,international break na Corona zilihusisha dunia nzima..
 
Timu hizo za taifa zimefanikiwa kwenda kwenye hayo mashindano kwasababu ya motisha na hamasa za wadau wa soka hapa nchini lkn Karia na TFF hawana strategies za kuzifanya hizo timu kufikia hatua hizo ambazo kwa jicho lingine hizo nafasi tulizipata kwa kudra za mwenyezi Mungu(zali la mentali) na si mipango..mfano angalia Simba kwa sasa ni timu inayojiendesha kimipango kufikia malengo,kwa sasa lolote mafanikio wanayopata si ya kubahatisha lkn timu ya taifa bado unga mwana tunabahatisha bahatisha
 
Mafanikio gani hayo?wakati anaingia tulikuwa wapi na sasa tuko wapi hususani, kwenye mafanikio ya timu za taifa, uinuaji vipaji, zaidi ya mizengwe tu,
 
Mafanikio gani hayo?wakati anaingia tulikuwa wapi na sasa tuko wapi hususani, kwenye mafanikio ya timu za taifa, uinuaji vipaji, zaidi ya mizengwe tu,
Timu imecheza AFCON, kwa mara ya kwanza baada ya miaka zaidi ya 30.

Timu imecheza CHAN.

Ligi ya Wanawake umestawi hadi wachezaji wameuzwa timu za nje ya nchi kama Mwanahamisi Omari.

Timu Zinafika Robo Fainali Club Bingwa Africa, imekuwa kawaida kwa sasa.

Nk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…