Mnaobeza na kukosoa milo yetu, basi tuambieni tule vyakula gani?

Mnaobeza na kukosoa milo yetu, basi tuambieni tule vyakula gani?

Cha mhimu punguza Kula Kula hovyo ....

Asubuhi unakula supu ya ng'ombe na chapatti tatu ,+peps ya baridi .........unaenda ofsin unakaa tu inazunguka kwenye kiti

Mchana unapiga ugali na samaki mkubwa ,unashushia Tena na pepsi ya baridi .....unarudi ofsin unakaa tu ....

Unatoka ofsin hata kutembea Kwa mguu mwili ufanye digestion Hakuna ...unaingia kwenye gari huyoo bar kumwagilia moyo ,bia 3 na nyama Choma nusu kilo ......unakaa tu na tumbo lako ....

Unafika nyumbani unapiga wali na nyama ,....unakaa tu kwenye sofa ,unaenda kulala....tumbo limejaa unapumulia juu juu kama nguruwe

Mazoezi hufanyi ...


Hicho chakula Hakiendani na Kazi unayofanya kiufupi kinaenda kuwa sumu mwilini ,Hakuna digestion system ....unaanza kufumuka na kuwa na tumbo kubwa ,ini ,Figo zote zinashindwa kufanya Kazi kutokana na mlundikano WA vyakula vya hovyo tu [emoji23]...sumu unajitengenezea ...hauwezi fikisha miaka 50 Kwa life style hio nakuapia Kwa mwenyezi Mungu .....
Sahihi
 
Vyakula vya kuchakata(processed) na vya kukaanga sio rafiki kwa afya. Wanga mwingi kama wewe sio mtu wa kufanya kazi ngumu ni hatari kwa afya yako. Ulevi ni hatari kwa afya yako.
 
Muungano OYEEE!!

Wakuu!
Kumekuwa na wimbi la wanaoitwa wataalamu wa afya na lishe kukosoa karibia kila aina za vyakula tunavyotumia kila siku.

Utasikia ugali ni chakula hatari sana kwa afya zetu. Wengine wanaenda mbali zaidi na kusema ugali ni chakula cha mifugo!

Profesa Janabi naye hayupo nyuma, kila kitu anapondea tu.

Lakini sasa hawasemi tunapaswa kula nini kwa matumizi ya kila siku.

Hebu tusaidieni ili na sisi tujiepushe na vyakula vya mifugo na kuboresha afya zetu.

Wasalaam....!!
Cement
 
Kula unachokula usijali maneno maneno, tafiti nyingi zimefanyika kwenye vyakula vya ulaya, na america. Hivi vyetu huwa tunavipita tu hatufanyi tafiti za kutosha, wakosoaji wengi ni wale wenye uwezo mbadala. Wananchi wengi hatuna mbadala, tunakula kinachopatikana kwa urahisi.

Familia zetu tunalima mihogo kwa ajili ya unga sio kuuza, Tunalima mahindoi kwa ajili ya unga sio ya kuchoma, Tunalima mtama, uwele, na uwele kwa ajili ya unga wa kupikia ugali sio uji.

Kanda ya ziwa tulikuwa tunavua samamki kwa ajili ya kitoweo, mboga za majani tunakula za kienyeji sio chineese, cabbage au michicha.

Tukifika mijini tunaanza kusikia utakulaje ugali asubuhi, au utakulaje ugali maharage kila siku, au unakula wanga sana, asubuhi uji, mchana ugali na usiku ugali.

Sisi tulikuzwa tunakula hivyo, kama sio uji na viazi au mihogo, basi unaweza kula chochote hata kipolo cha ugali asubuhi kama kifungua kinywa.

Tumekua tumeishi vizuri na tuna afya nzuri tu, hatuna magonjwa kama visukari, wala blood pressure.
Sasa wao wanao kunywa chai na mikate, wanataka nasisi tule kama wao, au chai na mandazi,vitumbua au chapati.
Binafsi nakunywa uji na viazi vya kuchemsha ua mihogo ya kuchemsha na sioni shida yoyote.

Kwasababu sipati mboga za kienyeji ndio nakula hizi sukuma wiki, michicha na cabbage, pia samaki, dagaa, au samaki wa kuanikwa kwa jua au moshi kule kanda ya ziwa tunawaita vibambara.

Ukiwafiuata hawa kwanza budget inakuwa kubwa na unaweza ushindwe kumudu maisha yako.
Kiafya wanavyokula wao ndio hatari zaidi kuliko tulivyozoea sisi.

wao wanakula sukari kwenye chai, mikate,cake, vitumbua na mandazi. Mimi kwenye viazi sipati sukari.
Nisiandike meengi ila nilichotaka kusema.

Kula upendavyo na uwezavyo, vyakula vingi vya mijini vina matatizo kiafya kula vyetu vya kiasili, usijali maneno yao.
 
Muungano OYEEE!!

Wakuu!
Kumekuwa na wimbi la wanaoitwa wataalamu wa afya na lishe kukosoa karibia kila aina za vyakula tunavyotumia kila siku.

Utasikia ugali ni chakula hatari sana kwa afya zetu. Wengine wanaenda mbali zaidi na kusema ugali ni chakula cha mifugo!

Profesa Janabi naye hayupo nyuma, kila kitu anapondea tu.

Lakini sasa hawasemi tunapaswa kula nini kwa matumizi ya kila siku.

Hebu tusaidieni ili na sisi tujiepushe na vyakula vya mifugo na kuboresha afya zetu.

Wasalaam....!!
Unaweza kula chochote kile but in moderation, si kula kama anavyofakamia vyakula Shilole na baadhi ya mademu wengine wa Kibongo. Unakuta mtu anakula utafikiri hajala mwaka mzima na hapo hapo anashushia na soda au juice which is a no no kwa Afya ya mwanadamu.
 
Quran na Biblia zimeelezea uharamu wa kitimoto kisayansi?
Qur'an ipi hiyo, ni hii ya shetani inayosema Muddy aliugawa mwezi mara mbili (kukata) na watu wanaamini mpaka leo hii japo hakuna ukweli?
 
Kipande cha muhogo wa kuchemsha na punje kumi za karanga au njugumawe kwa siku
 
Back
Top Bottom