Kama mchangiaji alivyosema upo general sana, ila mi nitashare kwa experience niliyonayo.
Zipo njia nyingi zinazozalisha kipato kwenye tovuti.
1. Monetization
-tovuti inatengeneza pesa kupitia ads network kama adsense, propeller, revenuehit etc.
-affiliate marketing programs.
Tovuti inaingiza pesa pindi mtu akinunua bidhaa kupitia link uliyoweka kwenye post yako.
Affiliate programs kubwa ni kama amazon, click bank na alibaba hizo ni baadhi.
2. Kuuza bidhaa au huduma kwenye tovuti yako.
Bidhaa inaweza ikawa digital products eg e-books, course, apps, softwares, templates etc
Au physical products, Tafuta uzi
https://www.jamiiforums.com/threads...nzisha-tz-na-uka-dominate-soko.1581329/page-8 kuna ideas nyingi tu.
3. Donation - tovuti huingiza kipato kwa njia za michango, mfano jf kuna platnumz member ambao hupata hiko cheo kwa kuchangia.
4. Kutengenezea watu webs au apps
5. kuuza website kwenye mtandao wa flipper.
Nk.
Tukija kwenye apps.
1. Ads
2. Subscription fees - wateja wanalipa kiasi cha pesa kila mwezi.
3. In app purchase - unaongeza advance feature ambazo zitamfanya mtu alipie ili apate access na hizo feature.
Kwa mfano una apps inayoelezea hadithi za kiswahili, then ukaongeza feature ya kuibadilisha post ya hadithi kuwa pdf ili mtumiaji aweze kusoma akiwa hata offline sasa kuunlock hiyo feature itamlizimu alipie.
Kikubwa unatakiwa ufanye tafiti maana ushindani ni mkubwa, baadhi niches hazina faida, kulenga audience ambayo ina purchasing power kubwa.
Halafu unajua nini, kufeli ni nje nje tu kama hutpweka muda stahiki mpaka hiyo product yako ianze kutengeneza faida, na pia kama lengo lako KUBWA NI PESA kwenye hatua za mwanzo.