Ndugu zangu,
Hili limenitokea napenda kuwapa tahadhari wale wote wanaofikiria kwenda kununua mbao buguruni wawe makini. Mimi nilikubaliana bei vizuri na muuzaji na kweli mzigo ulikuwa mzuri, pia bei ilikuwa nzuri tena ya kuvutia. Kazi ya kupima mbao ilipoanza ndipo nilipobaini wizi unaofanyika.
Jamaa wanatumia tape measure ambayo ni wizi mtupu.
Nilishtuka kuana mbao ya urefu wa kawaida, tape measure inasoma ft 24, hapo ndipo nilipogutuka nikaanza kuiangalia ile tape measure vzr, kumbe wameruka vipimo ili kuongeza idadi ya futi ili wapate faida zaidi...mfano ile tape measure inasomeka 1, 2, 3, 4, 5, 10, 11, 12, 13, 14, 15, 17, 18, 19, 22, ......... utaona jinsi kulivyo na gap kati ya 5-10, 15-17, 19-22...
Kwa mwendo huu unakuta jamaa wanaiba futi zaidi ya saba kwa mbao moja. Huu ni wizi mkubwa ukipiga hesa ya 300 kwa kila futi kwa zile mbao ndogo kabisa 2x2, ikiwa ni mbao inayouzwa futi 700/900 utashangaa umeibiwa hela nyingi mno.
Nikaja kuwakamata tena kwenye kujumlisha idadi ya futi zote baada ya kuhesabu mbao zote. Wanatumia calculator abayo ni famba!! yenyewe ikiandika 18.7 haiweki nukta inaingiza number nzima tu, hivyo 18.7 inakuwa 187. Walipomaliza kujumlisha nikashangaa kuona idadi kubwa mno ya futi ambazo ni sawa na hela nyingi mno!! nilipoanza kujumlisha mwenyewe kwa calculater ya simu yangu, nilibaini tofauti (wizi) wa laki tatu kwa mzigo mdogo wa laki 8.
Nimeona niwape hii wadau msijeingia vibaya. Jamaa wanakula kiulaini wasijue tunataabika sana kuitafuta hela ya kujengea...