Mnaokaa Uswahilini (Wilaya ya Temeke) Mungu awafanyie wepesi ndugu zangu. Jana machozi yalinitoka

Mnaokaa Uswahilini (Wilaya ya Temeke) Mungu awafanyie wepesi ndugu zangu. Jana machozi yalinitoka

Simao Latino

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2025
Posts
477
Reaction score
608
Mimi ninakaa Wilaya ya Ilala. Jana nilikuwa Wilaya ya Temeke (mtoni kwa Aziz Ally) nilishuhudia mida ya mchana badala ya mama kuwapikia watoto (watoto walitoka kucheza wakaja kulalamika njaa inawauma) akawapa 500 wote wawili wakanunue bagia na askrimu (ice cream) na ndio imetoka hiyo mpaka Usiku, kulingana na maelezo ya mwenyeji wangu. Sema na mimi nilikuwa majalala, nilibakiwa na nauli tu 2,000, laiti kama ningekuwa na kitu chochote ningeweza kuwaongezea hata 500 nyingine aisee.

Kama hauna pesa ya kumsaidia mtoto masikini, basi mkumbuke hata wakati wa sala au swala.

Daah, uswahilini panatisha wadau, hususan kwa watoto wadogo.

UPDATE LEO JANUARY 28, 2025 SAA 15:50
======
Nimegundua watanzania wengi wanapenda sana kusaidia wenye uhitaji kisha kujitangaza.

Laiti kama ningesema niliwasaidia wale watoto, mngenirushia tena mawe "KWA HIYO NDIO UMEKUJA KIJITANGAZA JF ILI UONEKANE UNA ROHO NZURI??" Hahahahaa wabongo wengi jau sana..
 
Mimi ninakaa Wilaya ya Ilala. Jana nilikuwa Wilaya ya Temeke nilishuhudua mida ya mchana badala ya mama kuwapikia watoto (watoto walitoka kucheza wakaja kulalamika njaa) akawapa 500 wote wawili wakanunue bagia na askrimu (ice cream) na ndio imetoka hiyo mpaka Usiku, kulingana na maelezo ya mwenyeji wangu. Sema na mimi nilikuwa majalala, nilibakiwa na nauli tu, laiti kama ningekuwa na kitu chochote ningeweza kuwaongezea hata 500 nyingine aisee.

Kama hauna pesa ya kumsaidia mtoto masikini, basi mkumbuke hata wakati wa sala au swala.

Daah, uswahilini panatisha wadau, hususan kwa watoto wadogo.
Hivi Tandale ipo wilaya gani
 
Back
Top Bottom