Mnaombeza Prof. Ndalichako, amesoma PhD University of Alberta Canada

Vipi kuhusu maprof wa Kihindi wanavyo ongea
Vipi wa Kinaijeria
Kweli Bongo nyoso tembea muone
Uliowataja changamoto kwao ni lafudhi au matumizi ya kiingereza cha ukanda.Lakini wanaongea kiingereza kizuri kwa minajili ya kuwasiliana vema.
 
Huyu profesa sijawahi kumsikia hata akitoa mastaplan hewa ya elimu ya Tanzania kama wenzie walivyo na mimastaplan hewa kibao kwenye sekta zao. Lukuvi kila siku na mastaplan zake zisizofika mwisho kwenye land, wa utalii hayuko nyuma kututangazia watalii hewa, wa uwekezaji, biashara aliamdulilai. Yeye tu kimya.

Atokelezee kwenye cameras day moja aseme amepata miskolaship 10000 Marekani na Canada ila sifa uwe na 1 ya point 3 lakini kutoka shule za Kata. 😄😄
 
Kwa majirani zetu Kenya, Uganda, Zambia na Rwanda itakuwa ilikuja na ndege.
mfumo wa elimu wa Tanzania na majirani zake NI tofauti.
NI kuulize swali unawaona watoto wa English medium wanavyopiga ngeri?
kiingereza ni lugha Kama lugha nyingine zinahitaji mazoezini kuongea.
Ndo maana Mimi nalaani Sana mfumo wa kufundisha kwa KISwahili shule za msingi za serikali alafu mtoto akienda secondary anaanza kiingereza.
 
Sasa kuliko kuendelea kuwa kituko ni vizuri tuamue kusuka au kunyoa. Kama ni Kiswahili iwe hivyo kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu kama ni Kingereza iwe hivyo pia.
 
Sasa kuliko kuendelea kuwa kituko ni vizuri tuamue kusuka au kunyoa. Kama ni Kiswahili iwe hivyo kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu kama ni Kingereza iwe hivyo pia.
Bora iwe hivyo.
Ujue mtoto Ana uwezo mkubwa Sana wa kushika vitu.lakini akishakuwa hauwezi Tena kumshikisha vitu.
Mimi naendaga beach nakutana na watoto wanapiga ngeri mpaka naona aibu..maana ananishinda.
KISwahili iwe lugha ya taifa lakini lugha ya kufundishia iwe kiingereza mwanzo mwisho.kiswahili kibaki ni somo moja wapo.
 
Bado hana kitu. Alisoma Canada lakini hakuelewa.
 
Pamoja na yote anaongea kingereza kama cha Umber Ruty Madam Super Wowowo.
 
Wewe tayari umejikubali kuwa ni mjingamimi huwezi kuwa mtu sahihi kuchangia mjadala huu. Ndiyo maana hata watoto wa kindergarten wanakushinda
 
denooJ
unaijuwa PhD wewe? Kwa mtu aliyesoma Primary School yenye English language kama somo la lazima, then O-Level somo la lazima plus language of instructions kwa masomo mengine yote. Halafu A-level, Bachelor, Master's to PhD language of instructions ni hiyo hiyo. Hakuna MSAMAHA wa kutojuwa kuandika na kuongea kiingereza.

Suala ni je Ndalichako alitetea vipi miswaada yake ya Msc na PhD?
 
Prof. Ndalichako amesoma ni kipanga sawa hakuna ubishi juu ya hilo. Alitakiwa aendelee kuzungumza lugha ya hesabu na takwimu kwa wanazuoni, alitakiwa ajirudi na kujitenga na mafarisayo kwenye vyuo vikuu na taasisi ya juu.

Ameshindwa kujitofautisha na wengine kuwa yeye ni msomi ameumiza maprofesa wengi waliopingana naye siku za nyuma. TCU waliokiona cha moto, NACTE na taasisi zingine za elimu ya juu. Siyo kwa kuziboresha lakini kuwakomoa waliomwambia tupishe njia tusonge mbele. Muda ni mwalimu utasema turudi darasani tukafundishe Hesabu na Takwimu kwa kuwa kuna tija ya kudumu katika kufundisha takwimu kuliko kukomoa kwa sababu tumetofautiana kifalsafa, kimtazamo na njia yako uitakayo tupite tumeisusia na kuikataa....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…