Mnaotaka kufanya kazi na wanaojiita Nickshine Media Production kuweni makini sana

Mnaotaka kufanya kazi na wanaojiita Nickshine Media Production kuweni makini sana

Master Legendary

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
576
Reaction score
876
Habari za asubuhi wanajamvi

Siandiki waraka huu kuharibu Biashara ya mtu au kwa chuki ila kwa nia njema kuepusha wanajamvi wenzangu kutokewa na yaliyonitokea.Na hata kama itatafsirika vibaya ila wameyataka wenyewe kwa kuharibu siku za watu.

Hawa vijana kwa wasiowafahamu ni wapiga picha za Video na Mnato hasa kwenye sherehe mbalimbali na Maharusi,Wanatumia Media sana kujitangaza sana kuwa ni wabunifu na wameweza kufanya lobying na kuchukua tuzo mbalimbali kitu ambacho kimewajengea kuaminika na kufuatwa na watu wengi sana.

Ila niwatahadharishe wanajamvi na Wengine wenye nia njema msije mkaingia kwenye mkumbo wa hawa wahuni na vijana wa mjini mkaharibiwa shughuli zenu msiamini kabisa kwamba kuna wanadamu wana roho za ajabu na kushindwa kuwa na utu kiasi hicho.

Ninaongea kwa yaliyonikuta mimi binafsi baada ya ukaidi,Niweke wazi nilitahadharishwa lakini nikajenga imani kwa kuangalia namna wanavyojitangaza na kupewa tuzo nikajua ndivyo walivyo,nikawapa siku yangu muhimu kabisa maishani ya kufunga ndoa yangu wanifanyie kazi ya Still picture na Video.

Aisee hawa vijana ni wahuni walichukua hela zangu wakaniharibia siku yangu walivuruga kazi zote pamoja na gharama kubwa walizochaji karibu vitu vingi wanavyoweka kwenye vipeperushi vyao ni utapeli havifanyiki na hivyo vichache wanavyoamua kuvifanya wao kwa matakwa yao huvipati utafuatilia miaka mimi nimeamua kuwaachia lakini nikiwa nimeumia sana.

Changamoto niliyoipata mimi sikuingia nao Mkataba nilikuwa nafanya malipo tu wananipa virisiti vyao vya Vitabu kwasababu ni wakwepa kodi pia nikashindwa hata kuwashtaki ila kwa jinsi walivyoniharibia shughuli yangu ningewapeleka mahakamani kama ningekuwa na Mkataba,Niwashauri wenye shughuli zenu ingieni tu Mkataba wa kisheria na Mavendors.

Kilichoniuma nilikuta watu wengi sana pale Ofisini kwao kila nikienda wanalalamika kufanyiwa vitu tofauti na makubaliano,kushindwa kupatiwa kazi zao,kuharibiwa shughuli zao nk niliumia sana kwasababu na mimi niliambiwa na dada mmoja nje wakati naenda kuwa ni wasumbufu nikakaidi baada ya kuwasikiliza manake wana sound balaa ikala kwangu.

Narudia nimeandika kwa nia njema ya kuzuia wengine wasitapeliwe au yasiwakute yaliyonikuta mimi,sherehe yangu ya harusi ambayo niliipanga kwa gharama kubwa sana na ndiyo siku yangu ya kipekee baada ya hapo ni kifo iliharibiwa na hawa wahuni,na kumbukumbu sina hadi leo kama mnavyojua picha ndiyo kumbukumbu zinazobakia.

Kwa jinsi nilivyoumia sipendi mtu mwingine aumie kama mimi au afanyiwe nilivyofanyiwa nimeona nina wajibu wa kutoka kushare na wenzangu.

Naruhusu povu kwa wenye upeo mdogo na watu wa kuchukulia mambo negative nimeshawasamehe ila wenye kuniona positive hii post itawasaidia.
 
Mimi nilishangaa walipoandika kwenye channel Yao YouTube et Harmonize amwapia Diamond hamuwez Kwa uchawi...!! Mara et Harmonize aelezea namna Diamond anavyomroga allikiba ...!! Aiseee hawa ni zaidi ya wahuni
 
Pole sana kaka sio wewe tu hata mimi imenikuta situation kama yako hivyo hivyo ila sio kwa nickshine ni kwa mpiga picha mwingine wa hapa hapa, aliharibu mnomno na hela nyingi tulimlipa, nikikaa sawa nitakuja nieleZe ila situations ni kama wewe kabisa.
 
Sisi tulitamani ata siku ijirudie
Hatukusain mkataba mwisho kwenye kufatilia kazi alipoona tumekua serious akatuambia kwanza ata mkataba hamjasain, ilhali sisi hatukusain kwasababu ya imani kwamba tunafanya kazi na mtu mwenye utu, risiti ya mashine hawatoi eti alitujibu yeye huwa anatoa kwa corporate client tu( hakua anajua kwamba na sisi tunauelewa wa izi risiti alfikiri anadanganya layman)( ILA SISI HAKUA NICKSHINE)
Ni vendor mwingine wa hapa hapa dar, ni wahuni sana hawa watu
 
Nachokiona kama point ni ufike shekilango toka ubungo mataa ila umezungukia ubungo>mwenge>bamaga>sinza>shekilango!

Umezunguka sana yani make your point clear...

Umelipa hujapewa picha? Picha zmepigwa vibaya? Baadhi ya vitu kama Tv Screens setups hazikuwepo ukumbini?
 
Pole sana kaka sio wewe tu hata mimi imenikuta situation kama yako hivyo hivyo ila sio kwa nickshine ni kwa mpiga picha mwingine wa hapa hapa, aliharibu mnomno na hela nyingi tulimlipa, nikikaa sawa nitakuja nieleZe ila situations ni kama wewe kabisa.

IMG_9739.jpg
 
Nachokiona kama point ni ufike shekilango toka ubungo mataa ila umezungukia ubungo>mwenge>bamaga>sinza>shekilango!

Umezunguka sana yani make your point clear...

Umelipa hujapewa picha? Picha zmepigwa vibaya? Baadhi ya vitu kama Tv Screens setups hazikuwepo ukumbini?

Hadi ikukute ndio utaelewa kaka, yani kwanza kama hawa vendor tuliotumia sisi walisisitiza tuwalipe malipo yote ndio mkataba unasema ivyo( ingawa hatukuusain alituambia atatutumia kwa email tusain kutokana na wingi wa mambo zile siku za mwisho tukasahau kusain ingawa oia hakuutuma na tuliona tunadeal na watu professionals wenye ethics za kazi kumbe ni sifuri) na tulikua recommended kwao na mtu credible ambaye wamefanya nae kazi, kitu nilichogundua ni hwa watu wenye majina huwa wanajali zaidi macelebrities ili wawa tangazie kuliko sisi tusio na majina ambapo sasa, sisi tusio na majina ndio sehemu kubwa ya wateja wao na wao bila kujua wanapoteza wateja kwa kutumisstreat sisi
 
Hii imewahi nikuta nilikubaliana na mtu kuhusu kunipiga picha na video futi, kilichonikuta na kosa nililofanya nikuwapa hela yote, kanitolea picha mbaya, photo album hajaleta mpaka leo, Hawa vijana wapiga picha ni wajinga they don't think about future wao wakilipwa wanajiona wamefika na wanao waharibia ni hao wateja wao.
 
Hadi ikukute ndio utaelewa kaka, yani kwanza kama hawa vendor tuliotumia sisi walisisitiza tuwalipe malipo yote ndio mkataba unasema ivyo( ingawa hatukuusain alituambia atatutumia kwa email tusain kutokana na wingi wa mambo zile siku za mwisho tukasahau kusain ingawa oia hakuutuma na tuliona tunadeal na watu professionals wenye ethics za kazi kumbe ni sifuri) na tulikua recommended kwao na mtu credible ambaye wamefanya nae kazi, kitu nilichogundua ni hwa watu wenye majina huwa wanajali zaidi macelebrities ili wawa tangazie kuliko sisi tusio na majina ambapo sasa, sisi tusio na majina ndio sehemu kubwa ya wateja wao na wao bila kujua wanapoteza wateja kwa kutumisstreat sisi
Ni kosa kuwalipa hela zote maana huwa wanaingiwa na tamaa hao wanakuwa na watu wengi hafu kingine picha zao huwa na quality mbovu kuliko za Tecno kikubwa ni wao kutoa mkataba wao na kuwalipa kidogo ulimaliza yote utaumia
 
Hadi ikukute ndio utaelewa kaka, yani kwanza kama hawa vendor tuliotumia sisi walisisitiza tuwalipe malipo yote ndio mkataba unasema ivyo( ingawa hatukuusain alituambia atatutumia kwa email tusain kutokana na wingi wa mambo zile siku za mwisho tukasahau kusain ingawa oia hakuutuma na tuliona tunadeal na watu professionals wenye ethics za kazi kumbe ni sifuri) na tulikua recommended kwao na mtu credible ambaye wamefanya nae kazi, kitu nilichogundua ni hwa watu wenye majina huwa wanajali zaidi macelebrities ili wawa tangazie kuliko sisi tusio na majina ambapo sasa, sisi tusio na majina ndio sehemu kubwa ya wateja wao na wao bila kujua wanapoteza wateja kwa kutumisstreat sisi
Ungewataja na jina kabisa
 
Naona wote huko juu mna andika taarabu tu na hamsemi ni kipi mlicho fanyiwa tujue.Mki ulizwa mlifanyiwa nini mna jibu vingine tu...kuna mdau hapo juu kauliza swali la msingi [emoji116]

Umelipa hujapewa picha? Picha zmepigwa vibaya? Baadhi ya vitu kama Tv Screens setups hazikuwepo ukumbini?

Lakini still mna lalamika bila reasonable point semeni hayo matatizo[emoji35]
 
Naona wote huko juu mna andika taarabu tu na hamsemi ni kipi mlicho fanyiwa tujue.Mki ulizwa mlifanyiwa nini mna jibu ujinga tu...kuna mdau hapo juu kauliza swali la msingi [emoji116]

Umelipa hujapewa picha? Picha zmepigwa vibaya? Baadhi ya vitu kama Tv Screens setups hazikuwepo ukumbini?

Lakini still mna lalamika bila reasonable point semeni hayo matatizo[emoji35]

Soma screenshot niliyotuma apo,picha na video mbovu na nyingine zilizokuwepo kwenye package hakudeliver, hata kudeliver tu izo mbovu ilikua patashika, alafu walikua wanatujibu mbovu, emagine wanatuambia mkataba hamkusain mkitaka nendeni popote na risiti walitoa mannual, izi weakness za kwetu za kutokusain na kupokea risit manual hatukuzizingatia sana maana hatukuwaza wanaweza kuwa na usumbufu na inefficiency kubwa kias icho
 
Soma screenshot niliyotuma apo,picha na video mbovu na nyingine zilizokuwepo kwenye package hakudeliver, hata kudeliver tu izo mbovu ilikua patashika, alafu walikua wanatujibu mbovu, emagine wanatuambia mkataba hamkusain mkitaka nendeni popote na risiti walitoa mannual, izi weakness za kwetu za kutokusain na kupokea risit manual hatukuzizingatia sana maana hatukuwaza wanaweza kuwa na usumbufu na inefficiency kubwa kias icho

Ata ivyo ni vile tu aliyeturect kwao ni mtu tunaheshimiana la sivyo tungefikishana mbali na risiti yake ya mannual kutokana ns ubabe aliyotufanyia.
 
Kuna haja ya kufanya kazi na ma underground tu. Hawa wenye majina wana pesa ya uhakika tayari ndio wamejawa viburi yani!

weakness kubwa kwetu ilikua kuignore mkataba, ingawa ata tungefanya enforcement yoyote bado kwetu pasingekua na msaada kwasbb demage iliyokwishafanyika haiwezi kuwa recovered, emagine video ya harusi lakini matukio na wahusika wanaoonekana ni bw na bi harusi tu( camera zilikua attentive kwao tu audience kwa ujumla na matukio muhimu mengine hamna
 
Back
Top Bottom