Mnaotamani Mbowe aachie uenyekiti, mnaweza kuja kumkumbuka ikitokea anarithiwa na kiongozi mwingine ambae hatokubali kuvumilia uonevu huu unaondelea

Mnaotamani Mbowe aachie uenyekiti, mnaweza kuja kumkumbuka ikitokea anarithiwa na kiongozi mwingine ambae hatokubali kuvumilia uonevu huu unaondelea

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Baadhi ya watu wa chama cha kijani wanatumia nguvu kubwa na muda wao mwingi kufanya kila waliwezalo kuhakikisha Mbowe harudi madarakani iwapo ataamua kugombea tena uenyekiti wa CHADEMA Taifa.

Binafsi watu hawa nawasikitikia sana kwani huenda hawajui walitendalo mithili ya wale Wyahudi waliomsulubisha Yesu msalabani ambao nao walikuwa hawajui walitendalo.

Na vita hii dhidi ya Mbowe bila shaka ina baraka za watu wakubwa tu walioko katika chama cha hawa wenzetu na pengine wana lengo la kutaka kutumia uchaguzi huo kuweka pandikizi lao katika nafasi ya mwenyekiti wa CHADEMA Taifa kwa masilahi yao ya kisiasa kama wanavyotuhuimiwa kuweka mapandikizi katika baadhi ya taasisi au vyama na kuzifanya taasisi au vyama hivyo kuwa ni taasisi butu/mfu.

Mimi nawashauri watu hawa wajue tu kuwa ikitokea Mbowe harudi madarakani kwa yeye mwenyewe kutogombea au vinginevyo, huku jitihada za kuweka mwenyekiti pandikizi zikifeli na badala yake CHADEMA wakafanikiwa kupata mwenyekiti mpya atakaekuja na misimamo na mitazamo tofauti katika kuiongoza CHADEMA ikiwamo kukataa kuvumilia uonevu huu unaoendelea dhidi ya wana-CHADEMA na upinzani kwa ujumla,basi watu wa chama cha kijani wajue tu wanaweza kuja kukumbuka sana Mbowe na wanaweza kuja kujuta na kusema bora Mbowe angebaki tu kuiongoza CHADEMA.

Busara na uvumilivu wa Mbowe, hamtaweza kuviona sasa mpaka pale mtu mwingine atakapochukua nafasi yake ingawa teyari Spika hivi karibuni alikiri kuwa Mbowe ni mtaratibu akimlinganisha na Lissu aliemuoma ni mtu mkorofi/mwenye kiburi.

Turejee maneno ya wahenga: "mtoto akililia wembe,mpe".
 
Pandikizi Ni Sumaye

Ila Mbowe Apumzike Inatosha.

Umbogo Wa Mbowe Ndio Umetufikisha Apa Tulipo.

Kuna Watu Makini Ndani Ya Chadema Tundu Lissu, John Heche Na Wengine Wasio Na Makando Kando Ya Tuhuma !

Magufuli Anahitaji Mtu Aina Ya Lissu.
 
Mbowe akiachia ngazi, chadema itakufa haraka sana, akiendelea na uongozi chadema itakufa taratibu, tunavhtaji wapinzani halisi sa hv waigizaji tumewachoka

eti.....??.... ongeza sauti
 
Pandikizi Ni Sumaye

Ila Mbowe Apumzike Inatosha.

Umbogo Wa Mbowe Ndio Umetufikisha Apa Tulipo.

Kuna Watu Makini Ndani Ya Chadema Tundu Lissu, John Heche Na Wengine Wasio Na Makando Kando Ya Tuhuma !

Magufuli Anahitaji Mtu Aina Ya Lissu.
Siwezi kukupinga unayoyasema,ila nawakumbusha watu wa chama cha kijanii kuwa uvumilivu huu unaoendelea kwa sehemu kubwa ni matokeo ya Mbowe kama mwenyekiti kutotaka kuongoza kwa style ya kulipa visasi ila wajue tu akipatikana kiongozi mwingine atakaekuja na mbinu tofauti za kujibu mapigo na kutafatu haki zinazominywa,basi ni hawa hawa ambao leo hii wanataka Mbowe aondoke ndio watakuwa wa kwanza kusema CHADEMA imepata kiongozi anaetaka kuvuruga amani ya nchi na ni afadhali Mbowe.

CHADEMA ikipata mwenyekiti wa tofauti na kwa haya yanayoendelea,basi yale ya Aquilina yanaweza kuja kuwa ni ya kila siku kama sio ya kila wakati.

Time will tell.
 
Ni kweli mbowe ni mvumilivu je njia mbadala ni ipi kuifanya ccm itoke madarakani
Njia mbadala zinafahamika ila siku akiingia kiongozi mwingine wa CHADEMA na atakaeamua liwalo na liwe,basi hizo mbinu zitakuwa wazi hata kwa vipofu na viziwi.
 
Kwa maana nyingine tofauti na Mbowe wengine wote wana elements za kuwa mapandikizi?

Kumbe hata hamuaminiani!

Mbowe hana busara na uvumilivu wowote sema kadhibitiwa tu,hata Slaa na Mamvi mlikuwa mnajifaragua hivihivi.

Hata Mangestu Haile Mariam alikuwa anapiga propaganda hizihizi kwamba bila yeye hakuna Ethiopia alipokuja Zenawi Ethiopia ikastawi kuliko wakati wote.

Hizo ni porojo tu za kuhalalisha kung'ang'ania madaraka na madikteta wote hufanya hivyo.

Hakuna jipya hapo.
 
Kwa maana nyingine tofauti na Mbowe wengine wote wana elements za kuwa mapandikizi?

Kumbe hata hamuaminiani!

Mbowe hana busara na uvumilivu wowote sema kadhibitiwa tu,hata Slaa na Mamvi mlikuwa mnajifaragua hivihivi.

Hata Mangestu Haile Mariam alikuwa anapiga propaganda hizihizi kwamba bila yeye hakuna Ethiopia alipokuja Zenawi Ethiopia ikastawi kuliko wakati wote.

Hizo ni porojo tu za kuhalalisha kung'ang'ania madaraka na madikteta wote hufanya hivyo.

Hakuna jipya hapo.
Mapandikizi wanatengenezwa na hawana tofauti na wale walioasi upinzani kwa kisingizio eti cha kuunga mkono juhudi hivyo kila kitu kinawezekana as long as mna pesa za kununua watu au kuwapa vyeo na madaraka.
 
Watakupinga, lakini ndio ukweli. Sasa hivi matukio ya uvunjifu wa amani mitaani no ajabu kuwa yanaratibiwa na chama tawala tofauti na ilivyo zoeleka nchi nyingi kuwa chama kikuu cha upinzani ndio huratibu matukio machafu kupinga utawala.
Kwa nini? Ni kwa sababu kiongozi mkuu wa upinzani kajawa hekima, moyo usio wa kisasi na kukulia mazingira ya kistaarabu yenye kujali utu wa mtu.
Sasa Mbowe atoke kisha uenyekiti apewe kamanda Heche kwa mfano, sio kuwa Heche sio mstaarabu bali asili ya kwao neno kuvumilia ujinga halipo mnategemea nini?
Kama kwenye mkutano wa hadhara anapandishiana na rais Magufuli hadi ananyang'anywa mic unadhani wa mchezo huyo akiwa ofisini peke yake? CCM mnalitafuta jini lililo kwenye chupa kwa kusuka mipango ya kumtoa Mbowe.
Sio kwamba mbinu zenu zitafanikiwa, lahasha Bali Mbowe kama binadamu na mwenye familia yake anaweza kuchoka akajisemea bora nika jipumzikie.
 
Watakupinga, lakini ndio ukweli. Sasa hivi matukio ya uvunjifu wa amani mitaani no ajabu kuwa yanaratibiwa na chama tawala tofauti na ilivyo zoeleka nchi nyingi kuwa chama kikuu cha upinzani ndio huratibu matukio machafu kupinga utawala.
Kwa nini? Ni kwa sababu kiongozi mkuu wa upinzani kajawa hekima, moyo usio wa kisasi na kukulia mazingira ya kistaarabu yenye kujali utu wa mtu.
Sasa Mbowe atoke kisha uenyekiti apewe kamanda Heche kwa mfano, sio kuwa Heche sio mstaarabu bali asili ya kwao neno kuvumilia ujinga halipo mnategemea nini?
Kama kwenye mkutano wa hadhara anapandishiana na rais Magufuli hadi ananyang'anywa mic unadhani wa mchezo huyo akiwa ofisini peke yake? CCM mnalitafuta jini lililo kwenye chupa kwa kusuka mipango ya kumtoa Mbowe.
Sio kwamba mbinu zenu zitafanikiwa, lahasha Bali Mbowe kama binadamu na mwenye familia yake anaweza kuchoka akajisemea bora nika jipumzikie.
Kwa hoja hizi mfu ccm bado itakuwepo miaka mingi sana
 
Watakupinga, lakini ndio ukweli. Sasa hivi matukio ya uvunjifu wa amani mitaani no ajabu kuwa yanaratibiwa na chama tawala tofauti na ilivyo zoeleka nchi nyingi kuwa chama kikuu cha upinzani ndio huratibu matukio machafu kupinga utawala.
Kwa nini? Ni kwa sababu kiongozi mkuu wa upinzani kajawa hekima, moyo usio wa kisasi na kukulia mazingira ya kistaarabu yenye kujali utu wa mtu.
Sasa Mbowe atoke kisha uenyekiti apewe kamanda Heche kwa mfano, sio kuwa Heche sio mstaarabu bali asili ya kwao neno kuvumilia ujinga halipo mnategemea nini?
Kama kwenye mkutano wa hadhara anapandishiana na rais Magufuli hadi ananyang'anywa mic unadhani wa mchezo huyo akiwa ofisini peke yake? CCM mnalitafuta jini lililo kwenye chupa kwa kusuka mipango ya kumtoa Mbowe.
Sio kwamba mbinu zenu zitafanikiwa, lahasha Bali Mbowe kama binadamu na mwenye familia yake anaweza kuchoka akajisemea bora nika jipumzikie.
Hawa jamaa wana vichwa vibovu/vizito na zaidi huwa hawaoni mbali until it is too late!!

Dunia itawafunza na watajua kuwa upole na uvumilivu wa Mbowe ndio ulikuwa msingi wa amani na utulivu tulionao leo hii kisiasa.
 
Hawa jamaa wana vichwa vibovu/vizito na zaidi huwa hawaoni mbali until it is too late!!

Dunia itawafunza na watajua kuwa upole na uvumilivu wa Mbowe ndio ulikuwa msingi wa amani na utulivu tulionao leo hii kisiasa.
Kuitoa ccm itabidi tusubiri mpaka mbowe afe hivyo ndo nilivyoelewa
 
Mbowe kafanya makubwa sana. Anastahili heshima na pongezi kwa aliyoyafanya.

Lakini wana- CHADEMA mnatakiwa kutambua kuwa binadamu anaweza kufaa sana kwa mazingira fulani kwa kazi fulani kwa wakati fulani lakini siyo lazima afae wakati wote kwa mazingira yote. Na siyo sahihi kwa sababu kiongozi alifanya vizuri sana wakati fulani aendelee wakati wote hata kwenye mazingira na nyakati asizozimudu kama shukrani kwa mazuri aliyoyafanya.

Ni kama CCM, ilitufaa wakati fulani kwa kazi fulani za wakati huo lakini kwa mazingira ya sasa haitufai tena. Ndiyo maana unakuta watu kama akina Kabudi, hata wakipewa nafasi ya kuongea, wanakazania kuongelea historia tu. Ni kwa sababu walionekana ni wasomi wazuri nyakati hizo lakini kwa nyakati hizi, wakiongea wanaonekana ni watu wasiojua kitu na waliopitwa na Ulimwengu uliopo.

Kwa mazingira ya sasa na kwa wakati huu, kwa kuyatazama mazingira ya siasa ya sasa, na hali ya CCM kwa sasa na uongozi wa CCM na serikali uliopo sasa, tunahitaji sana mbinu mpya, mtazamo mpya, fikra mpya na pengine viongozi wapya wenye ujasiri mpya.

CCM haitufai tena kwa mazingira ya sasa lakini kuiondoa kunahitajika mipangilio mipya kabisa. Siyo ile ya kale.
 
Ni kweli mbowe ni mvumilivu je njia mbadala ni ipi kuifanya ccm itoke madarakani
Tuache ugoigoi huwezi mtegemea mwenyekiti peke yake aitoe ccm madarakani.Enzi zile unahamasisha kura nyumba kwa nyumba unasimamia uchaguzi unasimamia kura zisiibiwe unasimamia tangazo la mshindi bila woga kwa ujasiri.
Vijana siku hizi ni kulia lia tuu katika mitandao
 
Mbowe kafanya makubwa sana. Anastahili heshima na pongezi kwa aliyoyafanya.

Lakini wana- CHADEMA mnatakiwa kutambua kuwa binadamu anaweza kufaa sana kwa mazingira fulani kwa kazi fulani kwa wakati fulani lakini siyo lazima afae wakati wote kwa mazingira yote. Na siyo sahihi kwa sababu kiongozi alifanya vizuri sana wakati fulani aendelee wakati wote hata kwenye mazingira na nyakati asizozimudu kama shukrani kwa mazuri aliyoyafanya.

Ni kama CCM, ilitufaa wakati fulani kwa kazi fulani za wakati huo lakini kwa mazingira ya sasa haitufai tena. Ndiyo maana unakuta watu kama akina Kabudi, hata wakipewa nafasi ya kuongea, wanakazania kuongelea historia tu. Ni kwa sababu walionekana ni wasomi wazuri nyakati hizo lakini kwa nyakati hizi, wakiongea wanaonekana ni watu wasiojua kitu na waliopitwa na Ulimwengu uliopo.

Kwa mazingira ya sasa na kwa wakati huu, kwa kuyatazama mazingira ya siasa ya sasa, na hali ya CCM kwa sasa na uongozi wa CCM na serikali uliopo sasa, tunahitaji sana mbinu mpya, mtazamo mpya, fikra mpya na pengine viongozi wapya wenye ujasiri mpya.

CCM haitufai tena kwa mazingira ya sasa lakini kuiondoa kunahitajika mipangilio mipya kabisa. Siyo ile ya kale.
Umeeleweka vizuri sana mkuu kwa kila mwenye akili na mwenye uwezo wa kusoma katikati ya mistari.
 
Mbowe kafanya makubwa sana. Anastahili heshima na pongezi kwa aliyoyafanya.

Lakini wana- CHADEMA mnatakiwa kutambua kuwa binadamu anaweza kufaa sana kwa mazingira fulani kwa kazi fulani kwa wakati fulani lakini siyo lazima afae wakati wote kwa mazingira yote. Na siyo sahihi kwa sababu kiongozi alifanya vizuri sana wakati fulani aendelee wakati wote hata kwenye mazingira na nyakati asizozimudu kama shukrani kwa mazuri aliyoyafanya.

Ni kama CCM, ilitufaa wakati fulani kwa kazi fulani za wakati huo lakini kwa mazingira ya sasa haitufai tena. Ndiyo maana unakuta watu kama akina Kabudi, hata wakipewa nafasi ya kuongea, wanakazania kuongelea historia tu. Ni kwa sababu walionekana ni wasomi wazuri nyakati hizo lakini kwa nyakati hizi, wakiongea wanaonekana ni watu wasiojua kitu na waliopitwa na Ulimwengu uliopo.

Kwa mazingira ya sasa na kwa wakati huu, kwa kuyatazama mazingira ya siasa ya sasa, na hali ya CCM kwa sasa na uongozi wa CCM na serikali uliopo sasa, tunahitaji sana mbinu mpya, mtazamo mpya, fikra mpya na pengine viongozi wapya wenye ujasiri mpya.

CCM haitufai tena kwa mazingira ya sasa lakini kuiondoa kunahitajika mipangilio mipya kabisa. Siyo ile ya kale.
Katibu MKUU awe Jacob Meya wa ubungo.Mwenyekiti Mbowe.Urais Lissu
 
Back
Top Bottom