Mnara wa Kumbukumbu ya Marubani wa Ndege vita ya JWTZ

Mnara wa Kumbukumbu ya Marubani wa Ndege vita ya JWTZ

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Mnara huu upo kaskazini mashariki mwa Uwanja wa Taifa, ni mnara wa kumbukumbu ya marubani wawili wa ndege vita ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ambao ndege yao ilianguka wakati wa maonyesho ya ndege hizo tarehe 01/09/1980.

Mara baada ya kuibuka na ushindi katika vita ya Kagera, wanajeshi wa Tanzania, waliandaliwa sherehe za kuwapongeza ambazo kwa Dar Es Salaam, zilifanyika uwanja wa Uhuru, na ndipo kukawa na maonyesho ya ndege vita.

Wakati wa maonyesho hayo, ikatokea hitalafu katika ndege moja wapo, hivyo kupeleka marubani wa ndege hiyo kushindwa kui-control.

Ndipo walipochukua uamuzi wa kishujaa kwa kuamua kuielekezea ndege hiyo nje ya uwanja ili kuepusha umati wa raia waliojitokeza kuwalaki mashujaa wao wasipatwe madhila hayo.

Marubani wale wakafa kishujaa, na mnara ukawekwa kama kukumbuka ushujaa wao! Walipambana vitani wakafia kwenye sherehe! Nitaleta majina yao hapo baadae!

Daima tunawakumbuka!

Adjustments.JPG
Adjustments.JPG
 
nilikuwepo uwanjani ingawa nilikuwa mdogo wale marubani baada ya kugundua ndege ina hitilafu waliiepusha kuangukia uwanjani na kwenda kuitupa pembeni walipewa nishani za ushujaa ikiwemo na yule askari aliyelala juu ya bomu mtwara ili kuwaokoa wenzake kwenye mafunzo na yeye kupoteza maisha
 
Majina muhimu sana,ila nilichogundua hapa ni kuwa moiga picha bado hajapata historia ya kutosha na hata majina ya wahusika,ila endelea kupambania angalau hata tuyapate kuyafahamu.
 
nilikuwepo uwanjani ingawa nilikuwa mdogo wale marubani baada ya kugundua ndege ina hitilafu waliiepusha kuangukia uwanjani na kwenda kuitupa pembeni walipewa nishani za ushujaa ikiwemo na yule askari aliyelala juu ya bomu mtwara ili kuwaokoa wenzake kwenye mafunzo na yeye kupoteza maisha
Wakati huo watu walikuwa na uzalendo was kweli siyo sasa
 
nilikuwepo uwanjani ingawa nilikuwa mdogo wale marubani baada ya kugundua ndege ina hitilafu waliiepusha kuangukia uwanjani na kwenda kuitupa pembeni walipewa nishani za ushujaa ikiwemo na yule askari aliyelala juu ya bomu mtwara ili kuwaokoa wenzake kwenye mafunzo na yeye kupoteza maisha

Tupe mawili matatu mkuu
 
Majina muhimu sana,ila nilichogundua hapa ni kuwa moiga picha bado hajapata historia ya kutosha na hata majina ya wahusika,ila endelea kupambania angalau hata tuyapate kuyafahamu.

Majina yao yapo hapo hapo kwenye mnara, ila nilisahau kuya-note, nikirudi tena ntawaletea hapa
 
Back
Top Bottom