Mnazipendea nini hidden roof house?

Mnazipendea nini hidden roof house?

Half american

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
38,283
Reaction score
97,793
Ni nyumba za kisasa lakini bado hatuna mafundi wazuri wa kuweza kuzifanya ziendane na hali zote, zimekuwa ni nyumba nzuri sana kipindi cha kiangazi, kipindi cha mvua nyingi ni majanga matupu zinavuja mno lakini bado watu wanajenga sana nyumba kwa mtindo huo ambao sio rafiki hasa kipindi cha mvua.

Kuna mwenye nyumba hapa kila ikinyesha mvua lazima umuone fundi kapanda juu ya bati(navyotype tayari kuna fundi juu ya bati) na wapangaji wake wanalalamika sana maji kuingia ndani na kulowanisha vitu. Kila akiendelea kujenga style ni hiyo hiyo lawama nyingi akiziangushia kwa mafundi wake.

Mafundi upi ushauri wenu juu ya hili?
Upi ni mtindo mzuri wa kupaua nyumba kwa mazingira ya huku kwetu na aina ya mafundi tulionao mitaani?
images (7).jpeg
 
Sio kila fundi aweza kujenga contemporary, ubahili wenu ndio unawafikisha hapo.

Fundi hajui hata kuna kitu kinaitwa DUCT...mnaishia kuwekewa mabomba ya inch 4 eti yavune maji yote kweli?

1. Hakuna duct ya kushusha maji
2. Slop ndogo
3. Hakuna mfereji mkubwa wa kuvuna maji
4. Ukutani kwenye maungio hakuna bitumen maalum

Unategemea isivuje?
ephen_
 
Wewe umepaua vip mkuu.hizo ukitaka hasa kuziwezea nakushaur weka slope moja usifunike upande mmoja
Kwenye joint ya bat na ukuta kuna jamaa wapo insta siku hizi wanafanya metal flashing.ukiweka hio kuvuja inaanzaje?
 
Sio kila fundi aweza kujenga contemporary, ubahili wenu ndio unawafikisha hapo.

Fundi hajui hata kuna kitu kinaitwa DUCT...mnaishia kuwekewa mabombavya inch 4 eti yavune maji yote?

1. Hakuna duct ya kushusha maji
2. Slop ndogo
3. Hakuna mfereji mkubwa wa kuvuna maji
4. Ukutani kwenye maungio hskuna bitumen maalum

Unategemea isivuje?
Nachokiona kwa hapa tatizo ni 2 na 4
 
KUBWA UKIACHA KUWA NA MVUTO ILA NASIKIA UJENZI HUO UNAPUNGUZA GHARAMA SANA.
NI UJENZI ULIOCHIPUKIA KWA KASI MIAKA HII LAZIMA UWE NA CHANGAMOTO KAMA HIZO HASA KWA KUWA MAFUNDI PIA NDIYO WANAJIFUNZA.
HII HAINA TOFAUTI NA KUPAUA ILE PAA LINAKUWA REFU SANA NI MITINDO YA SASA ILA NDIYO HIVYO INA KUJA NA ATHARI ZAKE.
 
Wewe umepaua vip mkuu.hizo ukitaka hasa kuziwezea nakushaur weka slope moja usifunike upande mmoja
Kwenye joint ya bat na ukuta kuna jamaa wapo insta siku hizi wanafanya metal flashing.ukiweka hio kuvuja inaanzaje?
Naomba link ya hao mafundi mkuu, maana kuna kakibanda ka wapangaji nafikiria nitumie hii design ili kuokoa gharama. Shida niliskia hizi habar za maji kuingia nikaanza kughairi
 
KUBWA UKIACHA KUWA NA MVUTO ILA NASIKIA UJENZI HUO UNAPUNGUZA GHARAMA SANA.
NI UJENZI ULIOCHIPUKIA KWA KASI MIAKA HII LAZIMA UWE NA CHANGAMOTO KAMA HIZO HASA KWA KUWA MAFUNDI PIA NDIYO WANAJIFUNZA.
HII HAINA TOFAUTI NA KUPAUA ILE PAA LINAKUWA REFU SANA NI MITINDO YA SASA ILA NDIYO HIVYO INA KUJA NA ATHARI ZAKE.
Naona pia kuna changamoto ya kulimaliza tatizo jumla, maana haiwezekani mwezi uliopita fundi aje kufanya marekebisho halafu baada ya mwezi hali iwe ile ile tena.
 
Back
Top Bottom