Mnazipendea nini hidden roof house?

Mnazipendea nini hidden roof house?

tatizo wabongo wanaiga sana. wanasema kwenda na fashion wenyewe. tunapanda hearsay .."flani kwake kafanya hivi na hivi", hatufanyi tafiti, tukiona dualis kesho kila mtu anataka dualis ..tukiona sienta kila mtu kesho anataka sienta.
Hili nalo ni tatizo kwenye jamii yetu ya kibongo, kwa sababu fulani kafanya acha na mimi nifanye, matokeo yake ndio hayo.
 
Swali lako umeshalijibu kwenye paragraph ya kwanza kwamba
"Ni nyumba za kisasa lakini bado hatuna mafundi wazuri wa kuweza kuzifanya ziendane na hali zote"
Kipi kifanyike ili kupata ubora halisi wa hizi nyumba? Nyumba unajenga haipiti hata mwaka inavuja
 
Ni nyumba za kisasa lakini bado hatuna mafundi wazuri wa kuweza kuzifanya ziendane na hali zote, zimekuwa ni nyumba nzuri sana kipindi cha kiangazi, kipindi cha mvua nyingi ni majanga matupu zinavuja mno lakini bado watu wanajenga sana nyumba kwa mtindo huo ambao sio rafiki hasa kipindi cha mvua.

Kuna mwenye nyumba hapa kila ikinyesha mvua lazima umuone fundi kapanda juu ya bati(navyotype tayari kuna fundi juu ya bati) na wapangaji wake wanalalamika sana maji kuingia ndani na kulowanisha vitu. Kila akiendelea kujenga style ni hiyo hiyo lawama nyingi akiziangushia kwa mafundi wake.

Mafundi upi ushauri wenu juu ya hili?
Upi ni mtindo mzuri wa kupaua nyumba kwa mazingira ya huku kwetu na aina ya mafundi tulionao mitaani?
View attachment 2805821
Hii ni hatari na nusu 😂
 

Attachments

  • TikTok_7295804132701539589.mp4
    2.5 MB
Ni nyumba za kisasa lakini bado hatuna mafundi wazuri wa kuweza kuzifanya ziendane na hali zote, zimekuwa ni nyumba nzuri sana kipindi cha kiangazi, kipindi cha mvua nyingi ni majanga matupu zinavuja mno lakini bado watu wanajenga sana nyumba kwa mtindo huo ambao sio rafiki hasa kipindi cha mvua.

Kuna mwenye nyumba hapa kila ikinyesha mvua lazima umuone fundi kapanda juu ya bati(navyotype tayari kuna fundi juu ya bati) na wapangaji wake wanalalamika sana maji kuingia ndani na kulowanisha vitu. Kila akiendelea kujenga style ni hiyo hiyo lawama nyingi akiziangushia kwa mafundi wake.

Mafundi upi ushauri wenu juu ya hili?
Upi ni mtindo mzuri wa kupaua nyumba kwa mazingira ya huku kwetu na aina ya mafundi tulionao mitaani?
View attachment 2805821
Hapo juu imekaa kama beseni yani mvua ikinyesha inabeba maji kuingiza maji ndani ni rahisi hata kama kuna outlet ya kutolea maji, pia joto jua likpiga vizuri humo ndani hamkae bila ac
 
Sasa iwe ni usiku, alafu hali kama hiyo inatokea. watoto watahangaika sana dah!.
Alafu kuwe na baridi inakera mno. Kuna jamaa alikuwa anasema kapasi zake nguo fresh tayari kwa interview siku inayofuata, mvua ikanyesha usiku anaamka asubuhi akakuta nguo zote zimelowana. Interview ikaishia hapo
 
Back
Top Bottom