Yesu Anakuja
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 12,675
- 25,924
sio bara, bali viongozi wa bara, nao wanang'ang'ania kwa kuogopa, wanahofu hata ya kujadili. ila kama wangekusanya maoni ya wengi, ungeshangaa wananchi ambacho wangekisema.Kiuhalisia bara ndio imeng'ang'ania mungano sana kuliko wazanzibar, kumbuka hata Nyerere ndie alieenda kumbebeleza Mzanzibar tuwe na muungano, ilibidi kumpa vitu vitamu tamu kama hivi viavyolalamikiwa ili muungano uwepo.
Akikutajia nishtue mkuuWana ubalozi nchi gani ya nje?!
ongeza sauti mkuu,....Refer Kenya vs Somalia.
Kwa taarifa yako, Zanzibar wameshafanya mambo mengi sana kuzidi Tanganyika kwenye kuvunja muungano ikiwemo makongamano, vyama vya siasa kama cuf, kuomba msaada wa umoja wa mataifa, n.k Lakini kwa kuwa wengi wao hawana nguvu za kimadaraka, inakuwa ngumuTengua kauli ni viongozi wenye maslahi binafsi ndio waliong'ang'ania muungano sisi wananchi wa bara hatuutaki muungano mpka kesho
Tunachukua jeshi letu tunawatoa wote wa wa Zanzibar kama wapo kwenye system na tunaliondoa.kule Zanzibar
Tunachukua umeme wetu
Tunachukua ardhi yetu
Kwenye utumishi, uongozi tunawatoa wajitegemee.wao
Tuwaone sasa na hayo ni machache
Kuna jambo moja tu ambalo linafanya hali iwe ilivyo mpaka sasa:View attachment 2029458
Naombeni wenye jicho la ziada mnitoe ujinga maana huu ujinga nilionao ndio unanifanya niwe napatwa na hasira kwa maono mafupi yanayonifanga nione Zanzibar inatunyonya
Kwa upeo wangu mfupi najionea mambo haya, Naombeni mnipe maarifa, huenda mtazamo wangu haupo sawa.
Mambo ya huku bara lazima yawe na mchanganyiko wa mtanganyika na mzanzibari kuanzia ajira, uongozi, jeshini, mahakama, n.k kwenye uongozi kukiwa na msaidizi wa bara basi mkuu inabidi awe wa Zanzibar, kwenye ajira nako katika kila ajira 100 basi 21 za wazanzibar, jeshini huko wapo wengi pia sana sana polisi na jwtz, ila sasa huko kwao mambo yao ni ya wao hawataki mchanganyiko, hapa Tanganyika tunanufaika kivipi????
Ukija kwenye ardhi, wazanzibari kibao wanamiliki mashamba makubwa na viwanja huku bara lakini mtanganyika harusiwi kufanya hivyo, Je tunanufaika kivipi??
Ukija kwenye Power, hakuna kabila wala kundi linalowafikia wala kuwasogelea wazanzibar, yani si mchaga wala msukuma wala kabila lolote unaloweza kulifikiria, hawa wenzetu wapo wachache lakini wamesambazwa si mchezo kwenye vyeo vizito. kuna mawaziri, wakuu wamikoa, wakuu wa wilaya, ma rpc, vyeo vikubwa jwtz, mabalozi wa nchi za nje, majaji wa mahakama, maprofesa vyuoni, waajiriwa kwenye mashirika yenye mishahara minono kama bandarini, Bot, Tanapa, Tra, Nssf, n.k hii ni kwasababu muungano unahitaji mchanganyiko wa pande mbili.
Mtanganyika hana nafasi kwenye serikali ya zanzibar kuanzia kwenye uongozi, ajira, mahakama, n.k Wana serikali yao kwajili yao kuanzia uraisi, makamu wa raisi, spika wa bunge, n.k hawa inabidi wawe wa zanzibar. pia wana taasisi zao kama Zff ambayo ni kama tff ya huku, Zrb ambayo ni kama Tra ya huku, Zssf ambayo ni kama Nssf ya huku, Jku ambayo ni kama jkt ya huku, yani taasisi zipo kibao kwakweli, hizo taasisi zinatoa ajira kwa wazanzibar tu, mtu wa Tanganyika huna sifa, lakini cha ajabu mzanzibar anaweza kupata ajira pande mbili za bara na huko kwao, vya bara ni vya wote ila vya zanzibar ni vya wao pekee, Patamu happ aisee 🤔🤔
Kwa maono yangu haya ambayo ni kwasababu ya kukosa maarifa, najionea tunapigwa nje ndani mbele ya macho yangu.
Wataalam wa haya mambo mnipe maelezo ili nipate ahueni.
Tanganyika mlishoboka tu....ndo mkome. Na bado...kofia zote Zanzibar na kwenu tumezi hold
Hii comment yako inaonyesha mahaba uliyo nayo kwenye nchi yakoKwa taarifa yako, Zanzibar wameshafanya mambo mengi sana kuzidi Tanganyika kwenye kuvunja muungano ikiwemo makongamano, vyama vya siasa kama cuf, kuomba msaada wa umoja wa mataifa, n.k Lakini kwa kuwa wengi wao hawana nguvu za kimadaraka, inakuwa ngumu
Hilo jeshi (JWTZ) ni jeshi la pande mbili Tanganyika na Zanzibar, kwa taarifa yako wapo wazanzibar wengi wa kutosha huko jeshini.
Jeshi lipo chini ya amiri jeshi mkuu ambae ni Raisi wa nchi, hio kauli yako ya kusema " tunachukua jeshi letu" haina mantiki.
Yaonekana hata elimu ya kawaida kabisa ya civics inakupiga chenga mkuu, Ni jambo inalowezekana kutamatisha muungano ila inabidi taratibu maalum zifatwe, sio kirahisi rahisi tu kama unavyofikiria.
Si afadhali ya huyu kaonesha mahaba na nchi yake kuliko wewe ulioshindwa kunyesha mahaba Kwa nchi yako,ukaonesha chuki kwa kuwaita machotara, karne hii unapanda basi la ubaguziHii comment yako inaonyesha mahaba uliyo nayo kwenye nchi yako
Mkuki kwa ngurue kwa binadamu mchungu. Kinchokukera wewe kinawakera Wazanzibari pia.Angefosi kuwe na serikali moja hizi drama zote zisengekuwepo.
Utakubali Dar iende zenj?,,, Unadhani kwanini Dodoma ikawa mji mkuu?wakoloni walileta haya ndo maana tuko hivi yaani sijui kwaninn huu muungano usivunjwe tukabaki watanganyika kwetu na wao kwao
Labda kwenye taasisi za muungano zilizopo Zanzibar kama Polisi, Air Tanzania, n.k. huko kwengine kwenye mambo ya serikali yao ni ngumu, wamewekwa wachache sanawanaohesabika ili kuzuga tu.Mkuu una uhakika mbara hawa ajiliwi?
Dar iende Zenji kwa kipi haswa ??Utakubali Dar iende zenj?,,, Unadhani kwanini Dodoma ikawa mji mkuu?
Muulize Lukuvi atakujibu, alikwishalisema hilo kanisaniView attachment 2029458
Naombeni wenye jicho la ziada mnitoe ujinga maana huu ujinga nilionao ndio unanifanya niwe napatwa na hasira kwa maono mafupi yanayonifanga nione Zanzibar inatunyonya
Kwa upeo wangu mfupi najionea mambo haya, Naombeni mnipe maarifa, huenda mtazamo wangu haupo sawa.
Mambo ya huku bara lazima yawe na mchanganyiko wa mtanganyika na mzanzibari kuanzia ajira, uongozi, jeshini, mahakama, n.k kwenye uongozi kukiwa na msaidizi wa bara basi mkuu inabidi awe wa Zanzibar, kwenye ajira nako katika kila ajira 100 basi 21 za wazanzibar, jeshini huko wapo wengi pia sana sana polisi na jwtz, ila sasa huko kwao mambo yao ni ya wao hawataki mchanganyiko, hapa Tanganyika tunanufaika kivipi????
Ukija kwenye ardhi, wazanzibari kibao wanamiliki mashamba makubwa na viwanja huku bara lakini mtanganyika harusiwi kufanya hivyo, Je tunanufaika kivipi??
Ukija kwenye Power, hakuna kabila wala kundi linalowafikia wala kuwasogelea wazanzibar, yani si mchaga wala msukuma wala kabila lolote unaloweza kulifikiria, hawa wenzetu wapo wachache lakini wamesambazwa si mchezo kwenye vyeo vizito. kuna mawaziri, wakuu wamikoa, wakuu wa wilaya, ma rpc, vyeo vikubwa jwtz, mabalozi wa nchi za nje, majaji wa mahakama, maprofesa vyuoni, waajiriwa kwenye mashirika yenye mishahara minono kama bandarini, Bot, Tanapa, Tra, Nssf, n.k hii ni kwasababu muungano unahitaji mchanganyiko wa pande mbili.
Mtanganyika hana nafasi kwenye serikali ya zanzibar kuanzia kwenye uongozi, ajira, mahakama, n.k Wana serikali yao kwajili yao kuanzia uraisi, makamu wa raisi, spika wa bunge, n.k hawa inabidi wawe wa zanzibar. pia wana taasisi zao kama Zff ambayo ni kama tff ya huku, Zrb ambayo ni kama Tra ya huku, Zssf ambayo ni kama Nssf ya huku, Jku ambayo ni kama jkt ya huku, yani taasisi zipo kibao kwakweli, hizo taasisi zinatoa ajira kwa wazanzibar tu, mtu wa Tanganyika huna sifa, lakini cha ajabu mzanzibar anaweza kupata ajira pande mbili za bara na huko kwao, vya bara ni vya wote ila vya zanzibar ni vya wao pekee, Patamu happ aisee 🤔🤔
Tukubali kwamba wazanzibar WALITUZIDI AKILI na sasa wanafaidi dili nono la muungano
Kwa upeo wangu nimegundua Karume alimzidi akili Nyerere, Alipoona kwamba Nyerere anambembeleza sana kuwe na muungano, Karume akatumia nafasi hii kumbana Nyerere aipe Zanzibar upendeleo kama huu tunaouona ama sivyo hauna muungano, Pia akaongezea kipengere kwamba endapo kukiwa na muungano basi Zanzibar iwe kwajili ya Zanzibar lakini Tanganyika ibanwe iwe kwajili ya wote, Mhh naandika huku achozi yananilenga aisee!! Kwa lugha nyepesi "changu ni changu ila chako tutagawana" matokeo yake leo Tanganyika tunashuhudia inapigwa nje ndani na wazanzibar licha ya malalmiko kuwa eti wao ndo wanaonewa