Mnijuze: Nani alikuwa bora kati ya Peter Manyika na Mohamed Mwameja?

kipa huwa mzuri akiwa na beki imara..unamaanisha mwameja hakuwahi kufungwa na timu zingine zaidi ya yanga!?..na kama alifungwa na nyota nyekundu au pilsner basi gulamali alihusika!!?..acheni hizo..mwameja kafungwa hadi na bule salehe wa amka ya nzega!!
 
 
afadhali wangemfananisha hats na Steven nemes sio manyika.
 
Wasifu mkuu wa Pondamali kitaani ilikuwa ni fujo fujo na ubabe kuliko hata nafasi yake ya golikipa.

Pamoja na kwamba Pondamali alikuwa mdogo kidogo, yeye enzi na level zake ni kina Mahadhi na Mambosasa. Pondamali inasemekana hakuvuta bangi, ila utundu wake ulifanya afikiriwe hivyo. Kumbuka yuko benchi la Yanga mpaka sasa. Angekuwa kweli mchomaji, kwa uchumi wa Bongo, leo angekuwa wapi?
 
Makipa hatari kwa mfuatano na umaarufu ni Juma Pondamali,Mwameja, Kaseja na sasa Aishi
 
Mkuu embu endelea, malizia Mkuu...
 
Mkuu embu endelea, malizia Mkuu...
Ha ha haa! Siku ile ya El Mereikh pambano lilikuwa kali ni balaa! Hata hilo goli moja walilopata El Mereikh hakika halikuwa bao, kwani mpira wa faulo uliopigwa na mchezaji wa El Mereikh uliingia kupitia wavu mdogo wa pembeni ukitokea nje, lakini mwamuzi Juma Ali David wa Zanzibar akaona tu mpira upo wavuni, akaweka kati! Haikuwa rahisi kwa Simba ile ya Mwameja kukubali goli hivi hivi, kwani mpira ulisimama kwa zaidi ya dakika tano Simba wakipinga goli, huku Mwameja akiwa kiongozi wa kukataa bao, huku akiwa ameukumbatia mpira (ukiwa mmoja uwanjani) akikataa usiwekwe kati. Akiwa amejisahau, Ramadhani Lenny Kaingilila Maufi akauchukua na kuanza kuupeleka kati, Mwameja akashtuka kuona uelekeo wa Lenny, akamkombiza na kumkaba kisha kuuchukua tena, kuendeleza ubishi. Baadaye joto likapoa Simba wakakubali liwe goli tu. Hata hiyo faulo ilitokana na nidhamu mbovu ya Mwameja, maana alikuwa ameudaka, akataka kuupiga mbele lakini mchezaji mmoja wa Mereikh akawa anazuia zuia kila mara. Basi Mwameja akasogea kidogo akaupiga mbele na kuusindikiza mguu (teke) kwa mchezaji huyo. Refarii Juma Ali David akaamuru ipigwe faulo, na kwa kuwa ilikuwa karibu na lango, wachezaji kama sita walijipanga kwenye mstari wa goli halafu wakamweka Mwameja mbele yao!
 
kipa mzuri ni mzuri tu mkuu, hakuna suala la beki wala nini, mfano mzuri ni david de gea wa manchester utd
 
Ni bora hata ungemuacha mwameja kwani huyu manyika hata akina Patrick mwangata. Ofen martin, Paul rwechungura, athuman msumali hawapati sembuse mwameja?
 
Ukiacha wazee kina Omary Maadhi bi Jabir Athman Mambosasa Idd Pazi father, Tanzania bado haijapata golikipa wa kariba ya Mwameja Mohamed Mwameja mpaka sasa.Mwameja ni bora kwa mbali sana kumzidi Manyika
 
Makipa hatari kwa mfuatano na umaarufu ni Juma Pondamali,Mwameja, Kaseja na sasa Aishi
simba mwenzangu hapa kwa Aishi nakataaaa

simba wamepita magolikipa bora wengi sana Kuanzia mambosasa, pazi , katuba mackenzie ramadhani, mwameja, nemes,

kule kwa mtani alikuwepo hamis kinye na sahau kambi huyu juma pondamali alisifika kwa mbwembwe tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu sikupingi ila nauliza tu, hivi kipindi Stella Abijan wakiifunga simba na Bolizozo akawa maarufu zaidi ya raisi wa Tz golikipa wa Simba alikuwa nani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…