Binafsi ninge penda tu kujuwa kama kuna sheria inayo zuia taasisi za kijamii, vyama vya siasa na wengineo kuifanya kazi hiyo ya kuwa hamasisha wananchi; au hata kuwapa tu taarifa/elimu kuhusu umuhimu wa uchaguzi huo.Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, ameishutumu Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kutoshughulikia ipasavyo suala la kutangaza na kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwaajili ya uchuzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kuanza tarehe 11 hadi 20 Oktoba, 2024, kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao utafanyika Novemba 27, 2024.
Akizungumza katika Ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA, Mikocheni, Dar es Salaam Mnyika amesema: “Tumetathmini na kuona kwamba TAMISEMI, ambayo ina mamlaka ya kuandaa uchaguzii, haina jitihada za kutosha za kuhamasisha wananchi kujiandikisha, wakati zikiwa zimebaki takribani siku tatu.”
Aliongeza, “Ikiwa jambo muhimu kama hili halipati uzito wa uhamasishaji mitaani, vijijini na kupitia vyombo vya habari, ni wazi kuwa ni mkatati na mnyororo wa ushirika haramu na kidharimu baina ya TAMISEMI na CCM"
Soma, Pia:
• Zoezi la uandikishaji wa wapiga kura (INEC) halijaamasishwa sana, isipokuwa kwa viongozi wa CCM waliwaambia wanachama wao wahakikishe wanatimiza zoezi
• Mchakato wa kuandikisha wananchi kwenye daftari la wapiga kura Zanzibar Umepoa mno. Kwanini influencers hawatumiki kama kwenye Kizimkazi Festival?
Hivi CHADEMA wakipanga kuwa na mikutano nchi nzima kuwafahamisha wananchi, watakuwa wamekiuka sheria?