Pre GE2025 Mnyika aitupia lawama TAMISEMI, adai ni Mpango wa CCM na TAMISEMI kutohamasisha Uandikishaji wa Wapiga Kura

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Binafsi ninge penda tu kujuwa kama kuna sheria inayo zuia taasisi za kijamii, vyama vya siasa na wengineo kuifanya kazi hiyo ya kuwa hamasisha wananchi; au hata kuwapa tu taarifa/elimu kuhusu umuhimu wa uchaguzi huo.

Hivi CHADEMA wakipanga kuwa na mikutano nchi nzima kuwafahamisha wananchi, watakuwa wamekiuka sheria?
 
Watapewa kesi ya uchochezi na ugaidi.
 
Hapo atakuwa kakosea kabisa kweli tovuti ya tamisemi kila kukicha wanaweka update ya mambo ya uchaguzi pia kwenye website za halmashauri ukipita unaona hamasa zinavyo fanyika
 
Nyie watu muwe serious aisee! Yaani mnategemea TAMISEMI ndio wawahamasishie watu wenu kujiandikisha? Bona hao sisiemu kila siku kiguu na njia kuwahamasisha watu wao wakajiandikishe? Aisee maajabu hayatakuja kuisha
 
Mpuuzi ni wewe
 
Tunayo haki ya kufanya hivyo lakini sisi sasa ni waoga tumebaki kudeka na kudemka tu
 
CHDADEMA ndo imefika huku!?🤔
 
Wasipoandikishwa ccm watanufaikaje?

Ukiona kutaoatapa kumeanza wewe.jua tuu ni dalili ya mvua ni mawingu 😁😁😁😁

Chadema si muhamasishe wenyewe au?
 
Kwani CHADEMA tumekatazwa kueleimisha na kuhamasisha wananchi na wachama wetu kujiandikisha kupiga kura? Huu ni upuuzi kabisa...Mnyika aseme ameshindwa kazi aliyopewa
Ok sawa, lakini pia nimezungumzia “voter suppression”

Mambo ama masharti ambayo yanatokea kuwa kikwazo kwa mpiga na mpigiwa kura.

Kumbuka wengi waliwahi kuzuiliwa kupiga kura na wengine kuenguliwa huku wa ccm wakipita bila kupingwa.

Sidhani kama upo kwenye hicho chama kama unavyojinadi.
 
kwenda kumuambia mtu wa chadema kuwa hakikisha unajiandikisha kupiga kura ni sawa na kumpigia kampeni ashinde waaacheni hivyohivyo ccm wanahamasisha watu wao chadema wacha wasubiri tamisemi wawahamasishie watu wao mtahenya
Nimezungumzia pia “voter suppression”, au hujaelewa?
 
Hata mm nashangaa!! Huu ni muda wa chama kuhamasisha wanachama wao. Sasa kuwalaumu TAMISEMI, ndio huo ujinga unaopelekea kushindwa uchaguz na kuanza, lawama kumbe ni upuuzi wao.
 
Watapewa kesi ya uchochezi na ugaidi.
Sikutegemea jibu la aina hii mkuu 'WALOLA VUNZYA', lakini kama hivyo ndivyo, basi hakuna njia ya kufanya chochote.

Hata huyo Mnyika awe mwangalifu anapo sema hayo aliyosema hapo; kwani ndio "uchochezi" wenyewe huo.
 
Tunayo haki ya kufanya hivyo lakini sisi sasa ni waoga tumebaki kudeka na kudemka tu
CHADEMA imebadilika sana miaka hii. Kuna wakati hiki chama kilikuwa hakiishii kulia lia hivi.
Nadhani kuna jambo limejificha kati ya vyama hivi viwili CCM na CHADEMA.

Hata kuelimisha wananchi kuhusu chaguzi liwe jambo la kuililia serikali, ambayo inajulikana maslahi yake yapo wapi?

Napata shaka sana na CHADEMA hii ya sasa.
 
Tupige kampeini na kuelimisha umma kamanda..ila tunahitaji wagombea wa form six basi
 
Ifikie wakati kupiga kura iwe lazma kwa mujibu wa sheria

tume inatumia pesa nyingi alafu watu wanadharau umuhimu wa kupiga kura
Sio kudharau... Kukata tamaa na uongozi thulumati... Nipigie kura wakati sina Imani na. Matokeo yajayo! Bora. Nitafute ugali wa watoto wangu...
mtu kesha weka msimamizi wakee Kuna haki hapo... 😁 😁
 
Dhana sahihi: Wanaotakiwa kuhamasiswa ni wananchi; Watanzania wote kwa ujumla wao, na si wanachama wa vyama vya siasa. Ni mushkeli mkubwa sana kufikiri kuwa wapiga kura wa nchi hii wote ni wanachama wa vyama vya siasa. Ni kukosa uelewa kukubwa sana na ni ujinga (ignorance) wa kiwango chake.

Kwa msingi huo, taasisi yenye muundo rasmi na inayoshikilia rasilimali ya taifa iliyotengwa kuimarisha demokrasia katika serikali za mitaa nchini ina jukumu la msingi (primary responsibility) na haina budi kuongoza juhudi za kuhamasisha wananchi wote kushiriki kikamilifu kwenye zoezi la uchaguzi kitaifa. Hiyo ni Serikali, TAMISEMI, specifically kwa uchaguzi wa serikali za mitaa.

Vyama vya siasa, asasi na taasisi nyingine za kijamii vinapaswa kushiriki ku-ongeza nguvu katika kazi hiyo - kwa kadiri ya uwezo wao. Katika kazi hii, vina secondary responsibility.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…